Hauhitaji tena Kwenda Bank kufungua akaunti ili upate kadi itakayokuwezesha kufanya malipo mtandaoni, ili mradi tu una akaunti ya M-Pesa. Au una kadi yako ya CRDB/NMB lakini hutaki kuitumia kufanyia malipo mtandaoni?
Chukua simu yako, tengeneza VISA Kadi leo kwani hakuna gharama yoyote utakayotozwa na haichukui zaidi ya dakika moja unakuwa tayari una kadi yako.
M-Pesa Visa Kadi ni nini?
Hii ni kadi mbadala ambayo humwezesha mtu kufanya malipo mtandaoni pindi anapokuwa ananunua bidhaa au huduma kwa kutumia akaunti yake ya M-Pesa.
Kadi hii inaruhusu kutumia pesa zako zilizopo M-Pesa kufanya malipo yoyote ya kigitali bila hata ya kuhamisha pesa Kwenda Bank.
M-Pesa Visa Kadi siyo kadi ya mkopo bali ni kadi ya malipo inayotengenezwa kupitia njia ya Mpesa yaani STK, USSD au App.
Baada ya kutengeneza M-Pesa Visa Kadi utapokea ujumbe wenye taaarifa zote kuhusu kadi yako ikiwemo kadi namba, tarehe itakayo-expire, CVV (Card Verification Value) namba.
Ili uweze kufanya malipo mtandaoni ni lazima uweke pesa kwenye kadi yako mara tu baada ya kuitengeneza au pale unapotaka kununua kitu.
CVV ni nini?
CVV ni namba za usalama ambazo huwasaidia wamiliki wa tovuti kuhakiki kama kweli wewe ni mmiliki halali wa hiyo kadi, pia husadia kupunguza udanganyifu unaoweza kufanyika kutoka kwenye kadi yako ya M-Pesa.
CVV zinafanya kazi ndani ya dakika 30 za mwanzo baada ya kufanya malipo. Hii husaidia kadi yako isitumiwe na mtu mwingine ambaye kwa bahati mbaya anaweza kujua taarifa za kadi yako na pia asiweze kubadilisha CVV namba. Hizo CVV zikishabadilishwa basi huwezi tena kuitumia hiyo kadi yako. Kuwa nazo makini.
Jinsi ya Kutengeneza M-Pesa Visa Kadi Nchini Tanzania.
Fuata hizi hatua kufanikisha zoezi hili,
- Bofya *150*00#.
- Chagua namba 4 LIPA kwa M-PESA.
- Chagua namba 6 M-Pesa VISA Card.
- Chagua namba 1 Tengeneza Kadi.
- Baada ya kufanikisha kutengeneza kadi, utapokea ujumbe wenye taarifa kuhusu kadi yako.
Jinsi ya Kuangalia Huduma Mbalimbali Kwenye Kadi Yako
- Bofya *150*00#.
- Chagua namba 4 LIPA kwa M-PESA.
- Chagua namba 6 M-Pesa VISA Card.
- Baada kuchagua namba sita utaona list ifuatayo (Tengeneza kadi. Taarifa za kadi. Weka Pesa kwenye Kadi. Salio la Kadi. Kadi Yangu. Msaada.)
Kwenye M-Pesa App
- Fungua M-PESA APP.
- Chagua Services tab.
- Chagua M-PESA Visa Card.
- Bofya Tengeneza M-PESA Visa Card.
- Baada ya hapo utapokea ujumbe wenye taarifa zako za kadi.

Huduma hii ya M-Pesa na Visa nchini Tanzania inaondoa kabisa haja ya kuwa na akaunti ya benki ili kuwa na kadi, na hivyo kufanya malipo kimataifa.
Kwa usalama zaidi, inashauriwa kurekodi maelezo ya kadi yako mahali salama na kufuta ujumbe wa nakala za Visa Kadi ya Mpesa kutoka kwenye Simu yako!
M-Pesa inaweza kupanua mtandao wake ikiwa na Visa. Ushirikiano huu utawawezesha watumiaji wa M-Pesa kufanya malipo ya kidijitali kupitia mtandao wa Visa wenye zaidi ya wafanyabiashara milioni 100. Awali, watumiaji wa M-Pesa walikuwa wamezuiliwa kufanya malipo ndani ya mtandao wa wafanyabiashara kwa mfumo wa M-Pesa.
Ushirikiano wa M-Pesa na Visa unaweza kuongeza matumizi ya mfumo huo kwa kutoa mtandao mpana wa ununuzi kwa watumiaji, ambao pia husaidia kuongeza uwezo wa mapato ya mfumo.
Ahsante kwa kusoma Makala hii.
Naitwa Anthony charles Mwandishi katika makala za Tanzlite.