Mambo Matano Mwanachuo Anaweza Kufanya ili Kukwepa Unemployed Baadae

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted June 17, 2023

Hakuna muda mzuri wa kukabiliana na unemployment kama muda ambao uko chuo.

Wengi huja kulifahamu hili tayari jua limeshazama, muda huo upo nyumbani, pengine hata kupata fedha ya kujikimu au ya vocha ni kipengele yaani kuipata ile buku mbili mpaka uende ukafanye kazi za vibarua ndio uipate.

Kitu kizuri ni kwamba leo hii upo chuo, unapokea boom, tukiongelea suala la bando kwako saivi siyo shida basi tumia muda huu kufanya mambo ambayo baada ya kumaliza chuo usihangaike kutafuta kazi.

Haya ndiyo mambo matano ambayo Mwanachuo unaweza kufanya ili kukwepa Unemployed baadae

1. Jiunge na mitandao ya kijamii muhimu kama vile Linkedin na Twitter

Linkedin au Twitter ndiko maarifa yalipo, huko utakutana na waajiri mbalimbali (Recruiters/Employers). Watu kama hawa inawezekana usiwaone kipindi unaanza ila jinsi utakavyozidi kuonyesha uwepo wako kwenye majukwaa hayo, ndivyo utakavyojiweka katika nafasi nzuri ya kupata fursa. 

Huko utapata kujifunza mambo kadha wa kadha yanavyoenenda kwenye tasnia yako, pia itakusaidia kuelewa mapema ni nini ufanye ili baadae usije kupishana na gari la mshahara.

Itakusaidia kuelewa jinsi mambo yanavyofanyika kwenye industry unayosomea. Siyo unamaliza chuo, unaambiwa nafasi zipo na zinahitaji mtu anayejua vizuri Microsoft Access, ndiyo ukute na wewe ulivipuuzia kipindi upo chuo.

Katika ulimwengu tuliopo simu au laptop yako ni siraha tosha inayoweza kubadilisha historia ya maisha yako, itategemea tu unaitumia kwa namna gani. Jambo la kufanya install app ya Linkedin na Twitter sasa hivi.

ALSO READ:  Usalama Mtandaoni ni nini? Umuhimu na Jinsi Ya Kuwa Salama.

2. Ongeza maarifa kupitia Online Courses

Internet imerahisisha maisha, leo hii unaweza kusoma popote ulipo na cheti ukitaka unapewa.

Course yoyote unayoitaka inapatikana mtandaoni ni suala la kuchukua simu na kuingia youtube, andika course unayotaka usome, mfano, Project Management full course, kwa click moja unamaliza course ukiwa na maarifa ya kutosha. Youtube inatoa course bure kabisa.

Pia kuna majukwaa mengi ambayo unaweza kuchukua course unayoitaka kama vile Linkedin learning, simplilearn, CompTIA+, Udemy, Coursera n.k huku unafundishwa real life experience tofauti na mwalimu darasani anaekufundisha ili amalize syllabus.

3. Kuwa vizuri kwenye lugha (written and spoken)

Asilimia 90% ya mazungumzo mtandaoni hufanyika kwa njia ya maandishi, hivyo ni vizuri ukajinoa zaidi katika kuandika na kuwasilisha maudhui/ujuzi wako kwa watu.

Njia nzuri ya kujinoa ni kuanza leo kwa kuandika mawazo uliyonayo kichwani kwenye notebook au applikesheni yoyote ikiwezekana uwe unapost hata kama kiingereza au kiswahili kimekaa upande. Practice makes more perfect.  

Ukiwa chuoni jitahidi kupost kila siku au mara mbili kwa wiki kama vipindi vitakuwa vimebana, ule muda unamaliza chuo, utakuwa na kundi kubwa la watu wanaokuhitaji ufanye nao kazi au uwafanyie baadhi ya kazi zao.

ALSO READ:  Ifahamu kazi ya Social Media Manager na majukumu yake

Muhimu: Post vitu vya msingi ambavyo mtu akisoma aseme kweli huyu kijana au huyu dada anajua.

4. Anza kufanya kazi ukiwa bado upo chuo (freelancing au virtual internship)

Tafuta kazi ambazo unaweza kufanya ingali bado unasoma, huu ndio muda wa kujitolee kwenye taasisi, kampuni mbalimbali. Fanya kazi as a freelancer kwenye majukwaa mbalimbali kama vile Upwork, Freelancer, Fiverr, Remototask.

Muda mwingine vitu unavyofundishwa darasani nitofauti kabisa na vile vinavyofanyika kwenye industry, hivyo ni bora kuyajua haya mapema na kuyafanyia kazi ili pindi utakapomaliza chuo isiwe changamoto kwako. 

Usisubiri mpaka umalize chuo ndio uanze kuomba kazi, najua unajua kule nyumbani hali ilivyo yaani kupata kazi ni mtiti, ukimaliza chuo ukaenda nyumbani, ndiyo imeisha hiyo.

5. Kuwa mtu mwenye haiba (personality) ili umma wa digitali uvutiwe na wewe

Kila siku jitahidi kuwa mtu wa tofauti na wengine, fanya vitu ambavyo watu wengi hawavifanyi ilimradi unaviamini, ni halali na hivyo utaonekana kuwa ni mtu wa pekee, na kwa upekee huo utajinyakulia fursa kedekede. Kuwa mtu wa kujifunza kila kukicha kwa kusoma vitabu, articles, hudhuria mikutano, seminar au online events. 

Hakuna chuo kinachoweza kukufanya ukwepe unemployed baadae, zaidi ya kuweka juhudi zako binafsi katika kuitengeneza kesho yako. Hatima ya maisha yako ipo mikononi mwako.

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite