Fahamu Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni (na Jinsi ya Kuwapata)

Fahamu Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni (na Jinsi ya Kuwapata)

Idadi ya Watanzania wanaotumia internet imefikia milioni 27. Katika mamilioni haya ya watu, kuna wateja wengi sana kwa ajili ya biashara yako. Lakini UNAWAPATAJE? Au wanakupataje? 🤔

Kabla hujaanza kutumia njia yoyote ya kidigitali kupata wateja mtandaoni, ni vyema ukafahamu makundi matatu ya wateja wanaopatikana mtandaoni. Itakusaidia kuandaa mpango (digital strategy) utakaoleta matokeo mazuri.

Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni 

1.Wateja wanao kufahamu: hawa ni wale ambao tayari wanajua biashara yako. Wanaweza kuwa ni followers kwenye account zako za mitandao ya kijamii, au una email list yao au wame-subacribe kupata huduma yako. 

Hawa ni rahisi kuwauzia bidhaa yako. Watu wakikufollow ujue tayari wamevutiwa na unachokifanya. 

Kazi yako ni kuwapa huduma bora ili wakakutangaze kwa wenzao. Fanya kila uwezalo kuhakikisha hili kundi haliondoki (Customer Retention

2. Kundi la pili ni wateja wanaohitaji bidhaa yako lakini hawakujui. Hawa wanaweza kuwa wanapata bidhaa hiyo kutoka kwa mtu mwingine au hawajui wapi pa kuipata. 

Kama wanaipata bidhaa hiyo kutoka kwa mtu mwingine maana yake tayari una mshindani. Hapa unakuwa na kazi ya ziada ya kumchunguza mshindani wako. Anatumia mbinu gani kupata wateja na bidhaa yake ni bora kiasi gani kulinganisha na yakwako. 

Je anatumia influencers? Maudhui yake ni bora kiasi gani? Ni mtandao gani wa kijamii amejikita zaidi? Ukifahamu haya na mengine utaweza kuja na mkakati (digital strategy) imara wa kukuza biashara yako. 

Kwa kuwa kundi hili ni la watu wenye UELEWA juu ya wanachohitaji, wengi hutumia search engines kutafuta bidhaa hiyo (they are actively searching online). Hivyo njia nyingine ya kuwapata ni kuwa na mpango imara wa SEO (Search Engine Optimization) au kutumia matangazo ya Google Ads

3.Kundi la tatu ni la wale ambao wangependa kutumia bidhaa yako lakini hawajui kama wanahitaji (they don’t know if they need it). Hapa sasa inabidi uwe vizuri kwenye kitu tunaita Content Marketing. Kundi hili la wateja wanahitaji kuelimishwa sana kabla hawajafanya maamuzi ya kutoa hela yao kununua huduma yako. Wanahitaji elimu juu ya tatizo walilo nalo na kwamba kuna suluhu ya tatizo hilo ambayo ni hiyo bidhaa yako. 

Mara nyingi ukiwa umegundua solution mpya juu ya tatizo fulani, tuseme ni software, tiba lishe au kitu chochote —watumiaji wa solution yako mara nyingi wanakuwa kwenye hili kundi la tatu. Wanahitaji maudhui ya kutosha kuwafundisha tatizo lililopo, madhara ya tatizo hilo na faida za kutumia bidhaa yako. 

Hitimisho

Kumbuka biashara ni watu. Kufahamu makundi ya wateja na tabia zao mtandaoni itakusaidia kuandaa mpango wa digitali wenye kuleta mafanikio katika biashara yako. Hasa upande wa maudhui kwani makundi haya matatu yanahitaji aina tofauti ya maudhui.

Ukiwapa huduma bora wateja waliopo kwenye kundi la kwanza hapo juu, wanaweza kuwa mabalozi wazuri kwa wateja wa kundi la pili na la tatu.

Natumaini makala hii imekusaidia. Naitwa Shukuru, ni mwandishi na mtaalamu wa Digital Marketing. Nipate kupitia mtandao wa WhatsApp hapa. Au jiunge na group letu la Wafanyabiashara wadogo mtandaoni kwa Tsh 7500.

COVID 19 Response, here’s what we are doing to help small businesses in Tanzania

COVID 19 Response, here’s what we are doing to help small businesses in Tanzania

The COVID 19 pandemic has brought a new awakening to big and small businesses in Tanzania. It has been obvious now that undergoing digital transformation is the only way to keep your business going. 

In fact, businesses that did not have a digital presence of any kind are the ones losing the most during this pandemic.

And the reality is that things are not going to get back to normal! In fact, things were already beginning to change even before the pandemic.

Before Covid19, the digital landscape in Tanzania was already taking significant growth (over 26 million Tanzanians were using the internet by the end of 2019). So it is fair to say COVID 19 has brought the future early.

It was only a matter of time before businesses were forced to undergo digital transformations. 

Welcome to the new digital Darwinism: If you don’t adapt, you are left behind and forgotten.

There is a big need for businesses to rethink how they operate in the world that is increasingly becoming digital. Not to mention recurring uncertainties.

Undergoing significant digital transformations can help you stay relevant and connected with your customers.

By saying digital transformations for businesses we mean, among other things, having infrastructures such as being able to collaborate online (remote work), knowing the best tools to use, leveraging online platforms such as websites, and social channels to grow brand awareness, as well as staying abreast with current trends in the digital world.

The way forward here is to adapt – so that you won’t risk being run over by your competitor in the disruptive digital communication’s race.

So, what are we doing to help?

Knowing the challenges small businesses and entrepreneurs go through on the journey of taking their business online, we have decided to be part of the help. Here is what we are doing to offer help during this pandemic.

  • Content creation (that is customer-focused) and content promotion tactics to help establish themselves as thought leaders in their niche.
  • Using data to measure digital success
  • Providing resources such as content calendars, social media posting ideas, and other resources. This includes changing the focus of our blog articles into helping readers on how to grow their businesses in the digital world.
  • Creating websites at affordable prices everyone can manage (we know these are hard times financially) plus a dedicated SEO strategy to help startups get noticed on the web just like we did on our business. 

AND HERE’S A GIFT FOR YOU: Download our list of social media posting ideas that can help you to increase engagement on your social channels. We use these exact ideas for our clients and they have proved to boost engagement especially on Instagram and Facebook.

And the best part of all, we are open to giving a dedicated Digital Marketing consultation to small business owners. This includes giving our best secrets that helped put us on top of Google in less than six months.

Wouldn’t you want to jump in front of your customers right at the moment when they are looking for you? Feel free to contact us HERE.