Jinsi Ya Kumsaidia Mjasiriamali Mdogo Kukuza Biashara Yake Mtandaoni

Jinsi Ya Kumsaidia Mjasiriamali Mdogo Kukuza Biashara Yake Mtandaoni

Hakuna mtu ambaye anaweza kufanikisha jambo bila msaada wa mtu au watu wengine. Tunaishi kwa kutegemeana. Unachokitafuta wewe kipo kwa mtu mwingine.

Katika dunia yetu ya kidigitali, ni rahisi kuwa sehemu ya msaada mkubwa kwa wajasiriamali wanaotafuta kukuza biashara zao mtandaoni. Unaweza kufanya hivyo bila hata ya kutumia pesa.

Jinsi ya kusaidia kukuza biashara ya mjasiriamali mtandaoni

Follow page yake ya biashara. Inaweza kuwa ni instagram, twitter au facebook – popote unapoona unaweza kumfolllow fanya hivyo. Hii haigarimu pesa yoyote.

Toa Comment , Like au Share post za bidhaa zake ili zipate kuonekana kwa wengi. Kumbuka wewe binafsi una followers ambao nao wana followers, hivyo ukishare au kucomment kweny post ya mjasiriamali huyu, unaipa nafasi post yake kufika mbali zaidi. Hii nayo haikugarimu hela.

Toa maoni, reviews auratings kuhusu huduma yake kwenye page yake Google My Business, kwenye App yake playstore, au kwenye listing directories zingine.

Weka picha ya eneo au bidhaa yake na shiriki kuhakiki (verify) taarifa zake kwenye ramani za google.

Pia wajuze marafiki zako juu ya bidhaa zake.

Cha mwisho, acha kuponda biashara ya mtu mtandaoni. Kama kuna kitu unaona anakosea ni busara kumtumia ujumbe inbox na kumweleza.

Ukifanya yote haya, utakuwa umetumia kiasi cha shilingi SIFURI!

Lakini utakua umemwezesha mtu kufikisha bidhaa yake kwa walengwa hivyo kujipatia kipato cha kuendesha maisha yake. Si lazima uwe na pesa kusaidia, japo ni vizuri zaidi kutoa ukiwa na uwezo huo.

Kama somo limeeleweka, naomba follow page za Tanzlite Digital kwenye mtandao wa LinkedIn, Facebook, Twitter na Instagram. Pia nenda kafanye hivo kwenye biashara ya mjasiriamali unayemjua.

Kugusa maisha ya watu wengine si lazima uwe Bill Gates. Kusaidia kukuza online visibility ya biashara ya mtu ni aina nyingine ya philanthropy!. Tuendelee kuinuana. Usisahau kushare post hii 🙂

Natumaini makala hii imekusaidia. Naitwa Shukuru, ni mwandishi na mtaalamu wa Digital Marketing. Nipate kupitia mtandao wa WhatsApp hapa.

Fahamu Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni (na Jinsi ya Kuwapata)

Fahamu Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni (na Jinsi ya Kuwapata)

Idadi ya Watanzania wanaotumia internet imefikia milioni 27. Katika mamilioni haya ya watu, kuna wateja wengi sana kwa ajili ya biashara yako. Lakini UNAWAPATAJE? Au wanakupataje? 🤔

Kabla hujaanza kutumia njia yoyote ya kidigitali kupata wateja mtandaoni, ni vyema ukafahamu makundi matatu ya wateja wanaopatikana mtandaoni. Itakusaidia kuandaa mpango (digital strategy) utakaoleta matokeo mazuri.

Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni 

1.Wateja wanao kufahamu: hawa ni wale ambao tayari wanajua biashara yako. Wanaweza kuwa ni followers kwenye account zako za mitandao ya kijamii, au una email list yao au wame-subacribe kupata huduma yako. 

Hawa ni rahisi kuwauzia bidhaa yako. Watu wakikufollow ujue tayari wamevutiwa na unachokifanya. 

Kazi yako ni kuwapa huduma bora ili wakakutangaze kwa wenzao. Fanya kila uwezalo kuhakikisha hili kundi haliondoki (Customer Retention

2. Kundi la pili ni wateja wanaohitaji bidhaa yako lakini hawakujui. Hawa wanaweza kuwa wanapata bidhaa hiyo kutoka kwa mtu mwingine au hawajui wapi pa kuipata. 

Kama wanaipata bidhaa hiyo kutoka kwa mtu mwingine maana yake tayari una mshindani. Hapa unakuwa na kazi ya ziada ya kumchunguza mshindani wako. Anatumia mbinu gani kupata wateja na bidhaa yake ni bora kiasi gani kulinganisha na yakwako. 

Je anatumia influencers? Maudhui yake ni bora kiasi gani? Ni mtandao gani wa kijamii amejikita zaidi? Ukifahamu haya na mengine utaweza kuja na mkakati (digital strategy) imara wa kukuza biashara yako. 

Kwa kuwa kundi hili ni la watu wenye UELEWA juu ya wanachohitaji, wengi hutumia search engines kutafuta bidhaa hiyo (they are actively searching online). Hivyo njia nyingine ya kuwapata ni kuwa na mpango imara wa SEO (Search Engine Optimization) au kutumia matangazo ya Google Ads

3.Kundi la tatu ni la wale ambao wangependa kutumia bidhaa yako lakini hawajui kama wanahitaji (they don’t know if they need it). Hapa sasa inabidi uwe vizuri kwenye kitu tunaita Content Marketing. Kundi hili la wateja wanahitaji kuelimishwa sana kabla hawajafanya maamuzi ya kutoa hela yao kununua huduma yako. Wanahitaji elimu juu ya tatizo walilo nalo na kwamba kuna suluhu ya tatizo hilo ambayo ni hiyo bidhaa yako. 

Mara nyingi ukiwa umegundua solution mpya juu ya tatizo fulani, tuseme ni software, tiba lishe au kitu chochote —watumiaji wa solution yako mara nyingi wanakuwa kwenye hili kundi la tatu. Wanahitaji maudhui ya kutosha kuwafundisha tatizo lililopo, madhara ya tatizo hilo na faida za kutumia bidhaa yako. 

Hitimisho

Kumbuka biashara ni watu. Kufahamu makundi ya wateja na tabia zao mtandaoni itakusaidia kuandaa mpango wa digitali wenye kuleta mafanikio katika biashara yako. Hasa upande wa maudhui kwani makundi haya matatu yanahitaji aina tofauti ya maudhui.

Ukiwapa huduma bora wateja waliopo kwenye kundi la kwanza hapo juu, wanaweza kuwa mabalozi wazuri kwa wateja wa kundi la pili na la tatu.

Natumaini makala hii imekusaidia. Naitwa Shukuru, ni mwandishi na mtaalamu wa Digital Marketing. Nipate kupitia mtandao wa WhatsApp hapa

Jinsi ya Kupata Wateja Mtandaoni Kupitia Matangazo Mguso (PPC Advertising)

Jinsi ya Kupata Wateja Mtandaoni Kupitia Matangazo Mguso (PPC Advertising)

Kukua kwa matumizi ya internet nchini Tanzania kumerahisha uwezekano kukuza biashara yako na kufikia wateja wengi mtandaoni. Zipo njia nyingi za kuweka biashara yako kwenye mtandao ikiwemo tovuti, mitandao ya kijamii, kupitia WhatsApp, email na nyingine nyingi.

Katika zama hizi za digitali, watu hufanya utafiti wa bidhaa wanayotaka kununua kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Utafiti wao mwingi unahusisha kutafuta (Search – au kugugo) kwenye injini za utafutaji pamoja na kusikiliza ushauri wa watu ambao wamewahi kutumia bidhaa hiyo.

Kwa wenye biashara zenye website, ipo njia ya kunasa wateja kwa haraka. Njia hii ni kutumia matangazo mguso (PPC ads). Njia hii huitaji kusubiri miezi kadhaa kuanza kupata watembeleaji kwenye tovuti yako kama ilivyo  kwenye mpango wa SEO.

Ukiwa mfanyabiashara, kuonekana kwenye matokeo ya utafutaji (search results) ni fursa kubwa ya kutangaza bidhaa au biashara yako ili watumiaji hawa wa mtandao (internet) waweze kuona biashara yako. 

Maana yake kama hauko online, watafutaji hawa watakukosa na mshindani wako aliyeko online atapata fursa ya kunasa hawa wateja.

 

Injini za utafutaji kama vile Bing, Google na Yahoo zina huduma ya kuweka matangazo kwenye matokeo ya utafutaji (search results) 

Kitaalamu inaitwa Paid Per Click Advertising (PPC). Ni aina ya kutangaza bidhaa au huduma kwa kununua maneno maalum (keywords) yanayohusu biasha yako ambapo utaweza kuonekana endapo mtumiaji akitafuta kwa kutumia maneno hayo. Maana ya jina Pay Per Click ni kwamba unalipa endapo mtu atabofya tangazo lako na kuzuru tovuti yako.

Matangazo haya hukaa mwanzoni mwa ukurasa wa matokeo ya utafutaji (search engine result page), yakifuatiwa na matokeo ya kawaida (organic results). Pia yanaweza kuonekana sehemu nyingine ndani ya results page.

Tazama picha ifuatayo:

Ufafanuzi kuhusu picha ya juu.

  1. Ni uwanja wa kutafutia (search bar) ambapo mtu ametafuta ‘stuffed animals’
  2. Vertical navigation (hapa unachagua uone matokeo ya Picha, Bidhaa, Video, Maeneo au Habari)
  3. Taarifa kuhusu matokea ya utafutaji (search results information)
  4. Haya ndiyo matangazo mguso (PPC Ads) 

PPC Inafanyaje Kazi? 

Matangazo haya hutolewa kwa ushindani au mnada. Wenye biashara hushindania maneno kwa kuweka dau kubwa juu ya mwenzake ili apate kuonekana  endapo mtu ‘atagugo’  kwa kutumia maneno hayo. 

Hivyo, mambo mawili ni muhimu kuzingatiwa;

  1. Dau lako kulinganisha na dau la mwenzako (auction) 
  2. Ubora na uhalisia wa huduma yako (quality and relevance) 

Hebu tuangalie mfano ili upate kufahamu zaidi:

Tuseme unamiliki hoteli na unataka kutangaza kupitia matangazo mguso. Washindani wako wengine kama kampuni mbili hivi  nazo  zinataka kutangaza. Hapo 

  • Best hotels in Serengeti
  • Serengeti National Park 
  • Tanzania adventures 
  • Best hotels in Tanzania
  • Luxury resorts in Tanzania

Tuseme wote mmechagua maneno hayo juu. Wewe ukaweka dola mbili per click, mshindani wako akaweka dola nne kwa kila mtu atakapo bofya tangazo. Hapa maana yake mwenzako atakuwa anaonekana zaidi kuliko wewe kwenye paid search results

Mara nyingi gharama za malipo per click hupanda kutegemea na ushindani na eneo unalotaka kutangaza. Kwa mfano, wewe ni Hosting company au Insurance company katika jiji la New York, hapo ushindani kwenye keywords utakuwa mkubwa hivyo utalazimika kuweka pesa nyingi.

Lakini kwa nchi kama Tanzania, makampuni mengi hawatumii PPC advertising, hivyo linaweza kuwa chimbo zuri kwako wewe kunasa wateja. Unaweza kujikuta ni wewe tu unayetangaza katika sekta yako.

Lakini pia kuna vigezo vya ubora na uhalisia wa maudhui na jinsi tovuti yako ilivyoundwa. Hivi vinaweza kuathiri uwezekano wa kuonekana kwenye matokeo ya utafutaji. Ikumbukwe lengo la google ni kutoa matokeo sahihi kwa watumiaji wake na kuhakikish user experience ni ya kuridhisha. Hivyo unaweza kuwa na dau dogo kuliko mwenzako lakini bado ukaoneka.

Vipi kuhusu ufanisi wake? 

Ufanisi wa aina hii ya matangazo ni bora zaidi kwasababu hapa unatangaza kwa watu ambao tayari wako interested na biashara yako. Yaani unalenga wateja ambao tayari wanatafuta huduma yako (customers who are actively searching for your product or service). 

Kupata umaarufu (awareness and recogntion) wa biashara yako mtandaoni inachukua muda kutegemea na maarifa na jitihada ulizo wekeza. Lakini kwa kutumia matangazo mguso (PPC) unaweza ukajulikana na kuanza kuvutia wateja kwa muda mfupi sana. Ni jambo la siku au masaa tu. 

Unahitaji kufahamu zaidi au kufanyiwa huduma hii kwenye biashara yako? Wasiliana nasi HAPA