Hakuna mtu ambaye anaweza kufanikisha jambo bila msaada wa mtu au watu wengine. Tunaishi kwa kutegemeana. Unachokitafuta wewe kipo kwa mtu mwingine.
Katika dunia yetu ya kidigitali, ni rahisi kuwa sehemu ya msaada mkubwa kwa wajasiriamali wanaotafuta kukuza biashara zao mtandaoni. Unaweza kufanya hivyo bila hata ya kutumia pesa.
Jinsi ya kusaidia kukuza biashara ya mjasiriamali mtandaoni
Follow page yake ya biashara. Inaweza kuwa ni instagram, twitter au facebook – popote unapoona unaweza kumfolllow fanya hivyo. Hii haigarimu pesa yoyote.
Toa Comment , Like au Share post za bidhaa zake ili zipate kuonekana kwa wengi. Kumbuka wewe binafsi una followers ambao nao wana followers, hivyo ukishare au kucomment kweny post ya mjasiriamali huyu, unaipa nafasi post yake kufika mbali zaidi. Hii nayo haikugarimu hela.
Toa maoni, reviews auratings kuhusu huduma yake kwenye page yake Google My Business, kwenye App yake playstore, au kwenye listing directories zingine.
Weka picha ya eneo au bidhaa yake na shiriki kuhakiki (verify) taarifa zake kwenye ramani za google.
Pia wajuze marafiki zako juu ya bidhaa zake.
Cha mwisho, acha kuponda biashara ya mtu mtandaoni. Kama kuna kitu unaona anakosea ni busara kumtumia ujumbe inbox na kumweleza.
Ukifanya yote haya, utakuwa umetumia kiasi cha shilingi SIFURI!
Lakini utakua umemwezesha mtu kufikisha bidhaa yake kwa walengwa hivyo kujipatia kipato cha kuendesha maisha yake. Si lazima uwe na pesa kusaidia, japo ni vizuri zaidi kutoa ukiwa na uwezo huo.
Kama somo limeeleweka, naomba follow page za Tanzlite Digital kwenye mtandao wa LinkedIn, Facebook, Twitter na Instagram. Pia nenda kafanye hivo kwenye biashara ya mjasiriamali unayemjua.
Kugusa maisha ya watu wengine si lazima uwe Bill Gates. Kusaidia kukuza online visibility ya biashara ya mtu ni aina nyingine ya philanthropy!. Tuendelee kuinuana. Usisahau kushare post hii 🙂
Idadi ya Watanzania wanaotumia internet imefikia milioni 27. Katika mamilioni haya ya watu, kuna wateja wengi sana kwa ajili ya biashara yako. Lakini UNAWAPATAJE? Au wanakupataje? 🤔
Kabla hujaanza kutumia njia yoyote ya kidigitali kupata wateja mtandaoni, ni vyema ukafahamu makundi matatu ya wateja wanaopatikana mtandaoni. Itakusaidia kuandaa mpango (digital strategy) utakaoleta matokeo mazuri.
Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni
1.Wateja wanao kufahamu: hawa ni wale ambao tayari wanajua biashara yako. Wanaweza kuwa ni followers kwenye account zako za mitandao ya kijamii, au una email list yao au wame-subacribe kupata huduma yako.
Hawa ni rahisi kuwauzia bidhaa yako. Watu wakikufollow ujue tayari wamevutiwa na unachokifanya.
Kazi yako ni kuwapa huduma bora ili wakakutangaze kwa wenzao. Fanya kila uwezalo kuhakikisha hili kundi haliondoki (Customer Retention)
2. Kundi la pili ni wateja wanaohitaji bidhaa yako lakini hawakujui. Hawa wanaweza kuwa wanapata bidhaa hiyo kutoka kwa mtu mwingine au hawajui wapi pa kuipata.
Kama wanaipata bidhaa hiyo kutoka kwa mtu mwingine maana yake tayari una mshindani. Hapa unakuwa na kazi ya ziada ya kumchunguza mshindani wako. Anatumia mbinu gani kupata wateja na bidhaa yake ni bora kiasi gani kulinganisha na yakwako.
Je anatumia influencers? Maudhui yake ni bora kiasi gani? Ni mtandao gani wa kijamii amejikita zaidi? Ukifahamu haya na mengine utaweza kuja na mkakati (digital strategy) imara wa kukuza biashara yako.
Kwa kuwa kundi hili ni la watu wenye UELEWA juu ya wanachohitaji, wengi hutumia search engines kutafuta bidhaa hiyo (they are actively searching online). Hivyo njia nyingine ya kuwapata ni kuwa na mpango imara wa SEO (Search Engine Optimization) au kutumia matangazo ya Google Ads.
3.Kundi la tatu ni la wale ambao wangependa kutumia bidhaa yako lakini hawajui kama wanahitaji (they don’t know if they need it). Hapa sasa inabidi uwe vizuri kwenye kitu tunaita Content Marketing. Kundi hili la wateja wanahitaji kuelimishwa sana kabla hawajafanya maamuzi ya kutoa hela yao kununua huduma yako. Wanahitaji elimu juu ya tatizo walilo nalo na kwamba kuna suluhu ya tatizo hilo ambayo ni hiyo bidhaa yako.
Mara nyingi ukiwa umegundua solution mpya juu ya tatizo fulani, tuseme ni software, tiba lishe au kitu chochote —watumiaji wa solution yako mara nyingi wanakuwa kwenye hili kundi la tatu. Wanahitaji maudhui ya kutosha kuwafundisha tatizo lililopo, madhara ya tatizo hilo na faida za kutumia bidhaa yako.
Hitimisho
Kumbuka biashara ni watu. Kufahamu makundi ya wateja na tabia zao mtandaoni itakusaidia kuandaa mpango wa digitali wenye kuleta mafanikio katika biashara yako. Hasa upande wa maudhui kwani makundi haya matatu yanahitaji aina tofauti ya maudhui.
Ukiwapa huduma bora wateja waliopo kwenye kundi la kwanza hapo juu, wanaweza kuwa mabalozi wazuri kwa wateja wa kundi la pili na la tatu.
Mtandao wa WhatsApp umetutoa mbali sana. Kutoka kwenye status za kuandika mpaka status za picha na video. Kutoka kwenye magrupu yenye ukomo wa watu 60 mpaka sasa magrupu ya watu nyomi hadi 257.
Ni wazi kwamba mtandao wa WhatsApp umezidi kuwa bora ili kuendelea kuwafurahisha watumiaji wake. Bora ukose application zingine kwenye simu lakini si WhatsApp.
WhatsApp imekuwa zaidi ya sehemu ya kuchat na kutumiana jumbe zenye kufurahisha (meme), bali ni fursa ya kibiashara kwa wajanja.
Watu wanataka kuuza, watu wanataka kujiweka karibu na wateja wao. Wengine ndio kwanza wanafungua biashara zao wakitafuta namna ya kujitangaza. WhatsApp imekuwa kimbilio la wajasiriamali wengi wa kitanzania.
Watu wameanzisha magrupu ya WhatsApp kwa lengo la kuendesha semina na mafunzo mbalimbali. Kuendesha vikundi vya kukopeshana, maarufu kama ‘vikoba’. Vilevile magrup haya yanatumika kuhamasisha watu kujumuika kwenye matamasha na warsha mbalimbali.
Siku hizi hata vikao vya Sendoff na harusi vinaendeshwa kwenye magrupu ya WhatsApp. Kama bado umejiunga kwenye magrupu ya kipuuzi, basi umebaki wewe tu na wapuuzi wachache. Wenzako tunasaka fursa!
Yani siku hizi kupata namba ya mtu ni rahisi sana kwa sababu anajua baadaye utaona matangazo ya biashara yake kwenye status. Wala si kwa ubaya, ni katika harakati za kutafuta masoko na kujipatia riziki. Wewe ambaye huna cha kutangaza usione kero.
Hatufahamu ni mazuri yapi mengine wamiliki wa mtandao wa WhatsApp wametuandalia, lakini kizuri kimojawapo ni kuhusu application ya WhatsApp Business.
WhatsApp Business ni nini na ina tofauti gani na WhatsApp ya Kawaida?
Kwanza kabisa, WhatsApp Business ni application halali inayomilikiwa na kampuni ya WhatsApp Inc. Hii sio kama zile WhatsApp GB na zinginezo (not a third-part App) ambazo huwa zinakataliwa. Hii ni maalumu kwa wafanya biashara na wajasiliamali wanaotaka kupromote biashara zao pamoja na kuimarisha mahusiano na wateja wao. Lakini hata wewe usiye na biashara unaweza kuitumia kwa mawasiliano ya kawaida.
Makampuni kama Bloomberg na Mwananchi wanatumia WhatsApp Business API (huduma advanced hii ni huduma ya kulipia) kutuma updates kwa subscribers wao moja moja kwenye inbox zao.
Sasa tuiangalie WhatsApp Business kiundani zaidi. Vitu ambavyo utavipata ndani yake ni kama ifuatavyo;.
Business profile
Ujumbe automatic wa salamu
Customer Management
Takwimu/statistics
Majibu ya haraka (quick replies)
Business Profile
Ukiangalia profile ya mtu anayetumia WhatsApp Business utaona ina muonekano tofauti na ile ya kawaida. Hapa utaona vitu kama jina la biashara, maelezo ya biashara (business description), location pamoja na siku na masaa anayofungua biashara yake. Hivi ni vitu ambavyo huwezi kuviona kwa mtu anayetumia WhatsApp ya kawaida.
Customer Management
Hapa unaweza kuchambua na kupangilia namba za WhatsApp ulizonazo katika makundi mbalimbali ya wateja. Kwa mfano unaweza kumwekea alama (label) kama vile mteja mpya, aliyelipa, asiyelipa, aliyetoa oda mpya na aliyemaliza oda yake.
Ujumbe Automatki wa Salamu
Hapa unaweza kutengeneza ujumbe wa salamu utakao kuwa ukitumwa kwa kila anayekutumia meseji. Ili kuondoa kero na usumbufu, ujumbe huu hutumwa endapo tu hamjawasiliana kwa kipindi cha siku 14. Ujumbe huu wa salamu unaweza kuwa unaelezea kwa ufupi juu ya shughuli unayofanya. Ni namna ambavyo wewe utapenda iwe.
Takwimu
Katika application ya WhatsApp Business, unaweza kupata takwimu kuhusu meseji ulizotuma. Utaweza kuona idadi ya meseji ulizotuma, zilizofika na zilizosomwa.
Quick replies and away message
Sikushauri utumie sana hii feature kwani humfanya mtu ajisikie kama ana wasiliana na roboti badala ya mtu. Kama namba yako ya mawasiliano ya kawaida ndiyo hiyo hiyo unatumia kwa biashara zako bora usitumie hii setting kwani si kila mtu ni mteja wako.
Jinsi ya kuwezesha WhatsApp Business
Ni rahisi sana kuseti business profile kwenye application ya WhatsApp Business. Unachotakiwa kufanya ni kwenda Playstore ama Appstore na kudownload WhatsApp Business. Baada ya hapo fungua application na uende kwenye Settings.
Kama unatumia android bofya kwenya vidoti vitatu upande wa juu kulia >Settings > Business settings > Hapo utaona setting zote unazotaka kufanya.
Mwisho…
Dunia ya sasa ni dunia ya kujiuza (simaanishi kujiuza unakofikiria wewe). It is all about branding yourself. Kama hutokuwa na ujasiri wa kusimama na kuonyesha ujuzi na maarifa yako, unataka nani akufanyie hivyo?
WhatsApp ni moja kati ya jukwaa zuri kuji-brand. Mara moja moja si mbaya kupost utani (meme) lakini isiwe kila siku wewe ni wa kupost upuuzi tu. Usifikiri ni utani tu, people are more likely to associate you with the things you post online. Jenga taswira chanya ili uweze kuvuta fursa zije upande wako.