Mbinu Mpya Ya Kupata Kazi Ukihitimu Chuo

Mbinu Mpya Ya Kupata Kazi Ukihitimu Chuo

Soko la ajira limekuwa ni changamoto kubwa kwa wanafunzi wengi wa vyuo vikuu.

Kupata kazi baada ya kuhitimu ndiyo lengo kuu muhimu ambalo wanafunzi karibia wote hujitahidi ili walifikie.

Hata hivyo, kupenya kwenye soko la ajira ni jambo linalohitaji juhudi, ujuzi na utayari. Katika makala hii, tutaangazia jinsi mwanachuo anavyoweza kupenyeza kwenye soko la ajira.

Je, ni nini unachoweza kufanya kama mwanachuo ili kuongeza uwezekano wa kupata ajira?

Mchakato wa kutafuta kazi unapaswa uanze mapema, hata kabla ya kuhitimu. Wewe ni mwanachuo?

Ndiyo, basi unaweza kuanza kutafuta fursa za ajira mapema mtandaoni au kwa kushiriki katika programu, kujitolea katika makampuni, miradi, seminar na kujenga uhusiano na wataalamu walioko kwenye tasnia anayotaka baadae ukufanyie kazi.

Kupata uzoefu wa kazi mapema itakusaidia kujenga ujuzi na uzoefu unaohitajika kwenye soko la ajira.

Ivi ulishawahi kusikia au kuulizwa hili swali, unauzoefu wa miaka mingapi? na  hapo ndio tu umemaliza chuo. Anza mapema ili baadae swali hili lisikusumbue.

Ni nini kinachotarajiwa kutoka kwako katika soko la ajira?

Unaweza kujenga mtandao wako wa kijamii (networking) kwa kuwa na mahusiano mazuri na walimu, wanafunzi wenzako na wataalamu wa tasnia yako. Kupitia mtandao huo, utaweza kupata taarifa za fursa za ajira pale zinapopatikana.

Muhimu: Kwa dunia tuliyopo, kama mwanachuo ataamua kuitumia vizuri mitandao ya kijamii yaani social media platforms kama Linkedin katika kujiuza (personal branding) basi mtu huyu hatakuwa anatafuta kazi bali kazi zitakuwa zinamtafuta by Shukuru Amos.

Soko linahitaji vijana wenye maarifa ya kufanya kazi fulani, haijarishi unacheti au la! kikubwa uwe na uwezo wa kufanya jambo fulani amazing.

Jinsi gani unaweza kuboresha ujuzi wako, kupata maarifa yanayohitajika katika tasnia uliyopo?

Technolojia inabadilika kwa kasi sana hivyo unaweza kutumia mitandao ya kijamii kufuatilia mabadiliko yanayotokea katika tasnia yako na kujifunza ujuzi mpya kupitia kozi za mtandaoni.

Chuoni utapewa Mwongozo tu hivyo kuna kila sababu za kutafuta maarifa zaidi. “Kama elimu ya chuo itashindwa kukufanya kuwa unachotaka basi Professor Youtube na msaidizi wake Google wanaweza”. Utajiuliza ni kivipi Youtube au google inaweza kukusaidia kutimiza ndoto zako? Fuatilia Makala zangu.

Je ni sahihi kuweka CV/wasifu wako mtandaoni?

Kutengeneza wasifu wako mtandaoni kunaweza kukusaidia sana katika kupata kazi. Wasifu huo utakuwa hewani 24/7 unasomwa na watu wa aina tofauti tofauti ikiwemo waajiri. Hivyo ni vyema kuweka mawasiliano yako, barua pepe na nambari ya simu ili watu wakikuhitaji iwe rahisi kukupata.

Wasifu wako mtandaoni unaweza kuwa fursa nzuri kwa waajiri kujua zaidi kuhusu wewe na uwezo wako. Mtandao unaofanya vizuri kwa sasa ni Linkedin.

Nifanye nini ili nitambulike na niweze kupata kazi?

Kujitangaza ni muhimu sana katika ulimwengu wa kigitali hasa unapokuwa kwenye harakati za kutafuta kazi. Wewe Mwanachuo unapaswa kuwa na ujuzi wa kujielezea mwenyewe katika majukwaa ya aina yoyote iwe kwa maandishi au kwa kuongea.

Kujifunza jinsi ya kuwa mbele kiujuzi na kimaarifa kunaweza kumsaidia mwanachuo kuwa na ujasiri, uwezo wa kushawishi waajiri wakupe fursa za ajira.

Asilimia 90 ya mazungumzo mtandaoni huwa ni kwenye maandishi hivyo ni bora kuwa vizuri zaidi kwenye uandishi.

Bonus: Mtu awaye yote, mwenye kutafuta afueni ya maisha yake, yambidi afanye bidii na juhudi zote katika kutatua matatizo yanayoisibu tasnia yake.