Jinsi AI Inavyoweza Kutumia Sauti Yako Kuzungumza na Mtu Mwingine

Jinsi AI Inavyoweza Kutumia Sauti Yako Kuzungumza na Mtu Mwingine

Baada ya Yombo kusikia neno AI linatamkwa sana huku mtaani ikabidi  amuulize jamaa yake Kadozo ili apate kujua zaidi. 

Hivi ndivyo Mazungumzo yalivyokuwa.

(Kadozo na Yombo ni vijana wanaosoma chuo, BBM)

Yombo: Je, unafahamu chochote kuhusu teknolojia ya AI?

Kadozo: Ndiyo, na nimekuwa nikisoma vizuri kuhusu maendeleo ya kuvutia yanayoletwa na AI, kama ulishawahi kusoma the discovery of fire basi hii ni discovery of AI.

Labda kabla hatujaendelea nikuulize, hivi unajua kwamba AI sasa inaweza kutumia sauti yako kuanzisha mazungumzo na mtu mwingine?

Yombo: Hapana? Mbona hii ni ya kushangaza! Inakuwaje na Inafanyaje kazi?

Kadozo: Vizuri, mifumo ya AI inaweza kuchambua, kuiga sauti ya binadamu au rekodi za sauti ili kuunda mfano wa sauti itayotumika na AI.

Mfano, sauti hii ninayoitoa kama itarekodiwa, AI inaweza kukopi na kutumia sauti hii hii kuzalisha maneno yaliyosanifishwa ambayo katika kuongewa kwake yatafanana sana na sauti yangu.

Yombo: Oooh! Very interesting, Lakini inaanzishaje mazungumzo na mtu mwingine?

Kadozo: Mara tu AI inapokuwa imesanifisha sauti, inaweza kutumia algorithms za usindikaji wa lugha asili kuchambua na kuelewa maudhui ya mazungumzo yenu kisha kuzalisha majibu yanayofaa na kushiriki katika mazungumzo na mtu mwingine. Yaani kama AI itaanza kwa kusema hello! na wewe ukajibu-

Hapo ndipo mazungumzo yanapoanzia kwa sababu itakuwa inajibu na kuuliza maswali kulingana na majibu yako. Kumbuka hapa itatumika tu kama imetengenezwa kwa lengo la kuongea na mtu mwingine.

Cha kuongezea tu ni kwamba ni kivipi sauti yako inaweza kuchukuliwa na AI?

Moja kati ya njia ni kutumia kumbukumbu za sauti yako iliyonakiliwa awali, kama vile sauti zilizorekodiwa za mahojiano au hotubaKisha, AI inatumia teknolojia ya kujifunza ili kujenga mfano wa sauti yako na kuitumia.

Moja ya njia zinazotumika kurekodi sauti yako ni voice cloning . Njia nyingine ni kutumia sauti yako inayopatikana kwenye mitandao ya kijamii.

Kadozo: Kwa hivyo, AI inaweza kimsingi kutumia sauti ya mtu na kuwa na mazungumzo yenye maana na watu wengine?

Kadozo: Ndio, hilo halina ubishi. Unaambiwa huwezi kumnasa samaki aliyefumba mdomo kwa kutumia ndoano.

Kwa hiyo AI inaweza kusikiliza kile mtu anasema, kuiga habari hiyo na kujibu kwa njia ambayo inasimulika kama mazungumzo yanayofanana na ya binadamu.

Yombo: Duh! hii mpya, Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza. Napata kujiuliza maswali mengi sana ya usalama?

Kadozo: Maswali gani hayo tena Mr. Yombo?

Yombo:  Sasa kama ni hivyo mfano si AI inaweza kutumiwa ili kupata taarifa zangu binafsi za shule kama itaiga sauti ya registration officer?

Kadozo: Bila shaka. Matumizi ya AI kufananisha sauti ya mtu yanazua wasiwasi kuhusu faragha, wizi wa utambulisho, na matumizi mabaya ya habari binafsi.

Lakini nikwambie kwamba katika ulimwengu tuliopo usimwamini mtu yeyote anayehitaji taarifa zako, pia tumia “multifactor authentication” ili kama humwelewi umwambie atumie njia ya pili kuwasiliana na wewe.

Kwa kawaida AI ukiiuliza wewe ni ni nani itasema Mimi ni kompyuta program niliyeundwa blablaa.

Hapa chini tulipata kumuuliza ChatGPT na alitoa majibu yafuatayo.

Sasa karibia kila aina ya AI huweza kujitabulisha kulingana na ilivyopangiliwa. Hapa ni rahisi sana kujua kumbe unaongea na AI. 

Mfano, Assume ChatGPT ingebatizwa kwa jina lako la Yombo, hapo juu ingesema “Mimi ni Yombo blablaa” chukulia ndiyo unaongea nayo kwenye simu, hapo si ni rahisi kuamini unaye ongea nae ndiye bwana Yombo? Hivyo ndivyo mambo yanavyoenenda ndugu yangu.

Tunaishi katika wakati ambapo teknolojia inabadilika kwa kasi, na AI inachukua jukumu kubwa katika mapinduzi hayo. Lazima tuwe wazi na tayari kukabiliana na changamoto na masuala mengine yanayoweza kujitokeza.

Yombo:  Hiyo ni uhakika. Nashukuru sana ndugu yangu kwa kunitoa gizani, siku nyingine nitakutafuta tuangazie mambo mengine kwa undani zaidi.

Kadozo: Haina noma mshikaji wangu.

Unaweza ukawa unajua kuwa watu wote wanajua kumbe hawajui. Kama una swali lolote dondosha coment yako hapo chini utajibiwa.

Mbinu Mpya Ya Kupata Kazi Ukihitimu Chuo

Mbinu Mpya Ya Kupata Kazi Ukihitimu Chuo

Soko la ajira limekuwa ni changamoto kubwa kwa wanafunzi wengi wa vyuo vikuu.

Kupata kazi baada ya kuhitimu ndiyo lengo kuu muhimu ambalo wanafunzi karibia wote hujitahidi kulifikia.

Hata hivyo, kupenya kwenye soko la ajira ni jambo linalohitaji juhudi, ujuzi na utayari. Katika makala hii, tutaangazia jinsi mwanachuo anavyoweza kupenyeza kwenye soko la ajira.

Je, ni nini unachoweza kufanya kama mwanachuo ili kuongeza uwezekano wa kupata ajira?

Mchakato wa kutafuta kazi unapaswa uanze mapema, hata kabla ya kuhitimu. Wewe ni mwanachuo?

Ndiyo, basi unaweza kuanza kutafuta fursa za ajira mapema mtandaoni au kwa kushiriki katika programu, kujitolea katika makampuni, miradi, seminar na kujenga uhusiano na wataalamu wa tasnia anayotaka kufanya kazi.

Kupata uzoefu wa kazi mapema itakusaidia kujenga ujuzi na uzoefu unaohitajika kwenye soko la ajira.

Ivi ulishawahi kusikia au kuulizwa hili swali, unauzoefu wa miaka mingapi? na  hapo ndio tu umemaliza chuo, Anza mapema ili baadae swali hili lisikusumbue.

Ni nini kinachotarajiwa kutoka kwako katika soko la ajira?

Unaweza kujenga mtandao wako wa kijamii (networking) kwa kuwa na uhusiano mzuri na walimu, wanafunzi wenzako na wataalamu wa tasnia yako. Kupitia mtandao huo, utaweza kupata taarifa za fursa za ajira pale zinapopatikana.

Muhimu: Kwa dunia tuliyopo kama mwanachuo ataamua kuitumia vizuri mitandao ya kijamii yaani social media platforms kama Linkedin katika kujiuza (personal branding) basi mtu huyu hatakuwa anatafuta kazi bali kazi zitakuwa zinamtafuta by Shukuru Amos.

Jinsi gani unaweza kuboresha ujuzi wako na kupata uzoefu unaohitajika katika tasnia uliyopo?

Technolojia inabadilika kwa kasi sana hivyo unaweza kutumia mitandao ya kijamii kufuatilia mabadiliko yanayotokea katika tasnia yako na kujifunza ujuzi mpya kupitia kozi za mtandaoni.

Chuoni utapewa Mwongozo tu hivyo kuna kila sababu za kutafuta maarifa zaidi. “Kama elimu ya chuo itashindwa kukufanya kuwa unachotaka basi Professor Youtube na msaidizi wake Google wanaweza”. Utajiuliza ni kivipi Youtube au google inaweza kukusaidia kutimiza ndoto zako? Fuatilia Makala zetu.

Ni hatua zipi muhimu ambazo unatakiwa kuzingatia wakati wa kuomba kazi na kuandaa wasifu wako?

Kutengeneza wasifu wako mtandaoni kunaweza kusaidia sana katika kupata kazi. Wasifu huo unapaswa kuwa na taarifa zako za kibinafsi, elimu yako, uzoefu wa kazi na ujuzi wako.

Unapaswa pia kuweka taarifa za mawasiliano yako, pamoja na anwani ya barua pepe na nambari ya simu.

Wasifu wako mtandaoni unaweza kuwa fursa nzuri kwa waajiri kujua zaidi kuhusu wewe na uwezo wako. Mtandao unaofanya vizuri kwa sasa ni linkedin.com

Jinsi gani unaweza kujifunza namna ya kuandaa wasifu wa kuvutia na kufanya mahojiano ya kazi kwa ufanisi?

Kujitangaza ni muhimu katika kutafuta kazi. Kama Mwanachuo unapaswa kuwa na ujuzi wa kujielezea mwenyewe katika majukwaa ya aina yote.

Uwe na uweza kutumia mitandao ya kijamii kuwasiliana na wataalamu wa tasnia yake na kuuliza maswali kuhusu jinsi ya kujitangaza vizuri kwenye soko la ajira.

Kujifunza jinsi ya kuwa mbele kiujuzi na kimaarifa kunaweza kumsaidia mwanachuo kuwa na ujasiri na kuweza kushawishi waajiri kumpa fursa ya ajira.

Asilimia 90 ya mazungumzo ya mtandaoni huwa ni kwenye maandishi hivyo ni bora kuwa vizuri zaidi kwenye uandishi.

Bonus: Mtu awaye yote, mwenye kutafuta afueni ya maisha yake, yambidi afanye bidii na juhudi zote katika kutatua matatizo yanayoisibu tasnia yake.

Je, ChatGPT Inaweza Kudukua Taarifa Zako?

Je, ChatGPT Inaweza Kudukua Taarifa Zako?

Hapana. ChatGPT haiwezi kudukua taarifa za watumiaji wake. Zana hii ya AI (Artficial Intelligent) ipo kwa lengo la kukusaidia kufanya kazi zako kama vile kuandaa maudhui kwa uharaka na ufanisi mkubwa.  

Pia ChatGPT, amabaye kimsing ni roboti unayeweza kufanya mazungumzo naye, anaweza kukupatia majibu ya maswali yako yoyote utakyouliza.

Hizo ndizo kazi za ChatGPT. Siyo kukusanya au kudukua taarifa zako.

Kama ulishawahi kutumia ChatGPT utajiuliza kwanini upande wa kushoto mwa smartphone au desktop yako ukiwa ume-login huwa kuna record za maswali yote uliyokwisha kumuuliza ChatGPT?  

Ni kwamba mazugumuzo yote ambayo unafanya na ChatGPT hurekodiwa kwenye (hifadhidata) database ya OpenAI. Hii inakuwezesha wewe kuweza kuona mambo yote uliyowahi kuchati naye. Lakini pia inakupa option ya Ku-delete kama huhitaji mazungumzo yaendelee tena kuligana na mada uliyokuwa unachat naye.

Pia huisaidia ChatGPT kukumbuka nini mnazungumzia hasa mazungumzo yakiwa ni endelevu.  Hapo tunapata hili Swali hapa chini:

Endapo hifadhidata ya OpenAI itakuwa-attacked, je, taarifa za mtu zinaweza kudukuliwa?

Hilo liko wazi; kama uliwahi kutoa taarifa zako binafsi (sensitive data) kwa ChatGPT basi hautakuwa katika mikono salama tena katika kipindi ambacho hifadhidata ya OpenAI itakuwa attacked.

Steve Mills, mtaalamu wa masuala yahusuyo AI na Maadili anasema “then you have lost control of that data and somebody else have it.” Ndio maana unaambiwa usimshirikishe ChatGPT taarifa zako binafsi.

Fuatilia katika hii link https://www.openai.com/blog/march-20-chatgpt-outage

Je, matumizi ya ChatGPT yanaweza kusababisha kuvuja kwa taarifa za kampuni?

Ndiyo, kama kuna mmoja kati ya wafanya kazi katika kampuni anatumia ChatGPT katika shughuli zake na kwa namna moja ama nyingine alihusisha au huhusisha taarifa nyeti za kampuni pindi akiwa anawasiliana na ChatGPT, Mtu huyu anaweza kusababisha security breaches of the network endapo tu akaunti yake ya ChatGPT itakuwa hashed/known na kuwapa uwanda mpana watu wengine kupata network datails alizoshare na ChatGPT akiwa anachat.

Hapa kwenye hashing itategemeana na urefu, ugumu wa nenosiri, kifaa anachotumia n.k.  Kumbuka hapo pia kuna Man in the middle attack.

Samsung waliliona hili na hivyo kuzuia wafanyakazi wake wasitumia generative AI kama ChatGPT ili kulinda usalama wa kampuni.