Njia Bora Ya Kujenga na kukuza Jina Mtandaoni

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted August 13, 2023

Haijalishi kuwa wewe ni mtoto wa mkulima, huna connection, umetafuta kazi umekosa, watu hawakujui au upo kwenye harakati za kujitafuta. Chukua simu yako zama mtandaoni huko ndiko fursa zilipo.

The universal does not belong to anyone group of people, everyone story is potentially universal it just need to be told well by Chimamanda Adichie

Tupo kwenye ulimwengu wa kidigitali ambao kila mmoja wetu anatumia mitandao ya kijamii kama Linkedin, Twitter, Instagram na Facebook ambapo kuna uwezekano mkubwa wa kujipenyeza nakujenga jina katika majukwaa hayo.

Imebaki kwako, kama Joti anajulikana kwa kuchekesha, wewe utajulikana katika lipi?

Kuna umuhimu gani wa kujenga jina mtandaoni?

Swali zuri, haujengi jina peke yake bali unajitengenezea mazingira mazuri ya kuondokana na kile wanachokiita unemployment na kuwa kwenye uwanja mzuri wa wajasiriamali.

Uwanja ambao hata kama baadae ukija kuanzisha biashara yako iwe ni rahisi kuaminiwa na kupata wateja kwa urahisi. 

Kutengeneza jina mtandaoni ni sawa na kuwa na bima ambayo itakusaidia wewe usihangaikei pindi mambo yatakapoenda ndivyo sivyo.

Saivi ni kawaida mtu kumaliza chuo na kurudi nyumbani kwenda kulima viazi, mwajiriwa kuendelea kutegemea mshahara, kuendelea kujitolea kwa sababu hakuna namna nyingine itakayomfanya apate pesa. 

Ulishawahi kusikia watu wanafanya kazi kama freelancer, yaani mtu aliyeko Washington Dc anampa kazi mtu aliyeko Tanzania? Huko ndiko kuzisaka fursa mtandaoni.

Unaikumbuka hii sauti “Tunakufungulia dunia kuwa unachotaka” au “Dunia ipo kiganjani mwako”

Ni njia zipi zitakazokusaidia kujenga na kukuza jina mtandaoni?

Unataka kuwa nani?

Hata nchi yenyewe huwa inaweka malengo ya muda mrefu na ya muda mfupi. Pasipo malengo ni sawa na kuendesha gari huku umesinzia. 

ALSO READ:  Mambo Matano Mwanachuo Anaweza Kufanya ili Kukwepa Unemployed Baadae

Kama tayari unajua baada ya miaka mitano unataka kuwa mtu fulani ni vizuri zaidi na kama bado hujajua chukua kalamu yako, andika malengo yako pembeni, njia hizo zisipo fanya kazi basi jitafute mpaka ujipate. Mali bila daftari huisha bila kujua. 

Je kweli umeandika? Hii itakusaidia pale unapoanza kukuza jina lako mtandaoni kwa kuangalia zaidi malengo yako yanasemaje, isije ikawa unatwanga maji kwenye kinu.

Unataka ujulikane katika lipi?

Watu wakianza kusema napenda unavyoongea, napenda idea zako n.k maana yake umeweza kujitofautisha na wengine.

Ukisikia diamond, Patrick lumumba amearikwa kwenye tamasha, unafikiri ni nini kitaenda kufanyika? Vipi ukisikia Elon Musk, Steve Job au putin?.

Hivyo ndivyo inabidi ujulikane katika mitandao, inakuwa ni rahisi watu kukujua na kukufuatilia. Mtu akiona tu profile yako anajua huyu ni fulani anazungumzia vitu fulani, simple like that.

NB: Hapa kidogo inahitaji juhudi na uvumilivu kwa sababu mwanzoni utahangaika sana, hakuna likes, hakuna comment yoyote, hakuna mtu anayeonekana kukusupport lakini kumbuka malengo yako yanasemaje na endelea kusonga mbele. Kitu kizuri lazima ukihangaikie. Ukweli ni kwamba watu wanaona na kusoma post zako kila siku.

Ni mitandao ipi uwepo?

Kulingana na malengo yako chagua majukwaa yasiyozidi matatu ili uwe na uwezo wa kuyahimili mfano Linkedin, Youtube, Twitter, Instagram. 

Kukuza jina katika majukwaa haya kama nilivyo sema ni shughuli kidogo inakubidi ujitume kuwa active, onyeshe uhai wako kwa kupost, kushiriki kwenye post za watu wengine. Jinsi watu wanavyoona profile yako kila siku ndivyo wanavyozidi kukumbuka.

ALSO READ:  Usalama Mtandaoni ni nini? Umuhimu na Jinsi Ya Kuwa Salama.

Ni maudhui gani upost?

Post chochote kama profile yako inavyojieleza hakikisha post zako ziwe kwenye mazungumzo yaani mtu akiwa anasoma awe kama vile anaongea na wewe tofauti na hapo post zako zitaonekana zimeandikwa na Chatgpt, hazina mguso. 

Hakikisha unatumia style mbali mbali katika kuwasilisha maudhui yako ili usiwachoshe wasomaji mfano tumia image, graphics, texts au short video kama ni itakupendeza.

Kitu kinachokufanya uonekane tofauti na wengine ni historia yako pamoja na vitu unavyovifanya katika hadhara ya mamilioni ya watu, wataalamu wa sales and marketing wanasema ujiuze.

Social media is indeed the best way to build an audience as it’s reach is global and connecting is as easy as  few clicks ~ Jules Marcoux

Post yako lazima iwe

  • Inalenga mtu au kundi fulani la watu
  • Inatatua changamoto fulani
  • Inaelimisha jambo fulani na 
  • Siyo, from no where umekula zako sangala unaenda kujipost. 

Fahamu hadhira yako.

Watu wote mtandaoni hawawezi kuwa hadhira yako, ni lazima uchague aina fulani ya watu ambao ndiyo target yako. Mtandaoni kuna watu wa kila aina, siyo lazima kila mtu akujue okay! au wewe umewahi kwenda kununua nguo buchani?

Kujenga jina maana yake ni kujenga mahusiano mazuri na watu unaowalenga, watakao furahia uwepo wako na walioko tayari kupokea kile utakachowapatia. 

Watu hununua bidhaa au maarifa kutoka kwa watu wanaowajua na kuwaamini. Soko ni watu na watu wako mtandaoni, wafuate huko huko waliko.

Ni matumaini yangu umejifunza kitu. Ahsante ndugu.


Naitwa Anthony Charles, Mwandishi katika blogu za Tanzlite

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite