Ajira Ni Tatizo: Fanya Mambo Haya Ukiwa Chuoni

Ajira Ni Tatizo: Fanya Mambo Haya Ukiwa Chuoni

Changamoto kubwa inayosumbua vijana wengi ni tatizo la ajira. Kila sehemu utasikia ajira hakuna ila kazi zipo.

Umekuwa wimbo unaovunja rekodi kila siku kuanzia juu hadi ngazi ya familia.

Wimbo huu unaongoza kwa kuimbwa na wahitimu wengi wa vyuo hapa nchini na kuna wengine wamegeuza tatizo hili kuwa ajira. Jambo ambalo ni zuri.

Ukiwa chuo usikae tu kizembe jaribu kufanya mambo mbalimbali yatakayokusaidia kukwepa Unemployment baada ya kumaliza chuo. Ni bora kujiandaa mapema kuliko kusubiri hatima usiyoijua.

Kukabiliana na janga hili kuhusu mbinu gani utumia kutafuta kazi, kwanza inabidi ujiulize wewe kama mwanafunzi unataka kuwa nani? Mpaka sasa unafanya nini kuhakikisha unakuja kuwa huyo mtu?

Vijana wengi husema acha kwanza nimalize itajulikana mbele kwa mbele. Mbele ipi wakati ukimaliza chuo unaenda kwenu ambako kupata fedha ya vocha tu ni changamoto!

Hivi unafikiri ukimaliza chuo mambo yatanyooka kama unavyotarajia? hata wao walifikiri vivyo hivyo kilichotokea hawaamini hadi leo.

Haya hapa mambo matano (5) ya kufanya ukiwa chuoni

1. Chagua somo moja utakaloteseka nalo hadi kumaliza chuo.

Ukiwa chuo huwezi kuwa vizuri kwa yale yote yanayofundishwa darasani na pengine usiyafanyie kazi kabisa maishani mwako japo ni vizuri kuyafahamu.

Ukiamua kusoma course fulani chagua kitengo kimoja tu utakachokuwa unasoma kila siku iwe mchana iwe usiku unakomaa nacho mpaka unamaliza chuo mfano ukiamua kuchakalika na network hakikisha network haikupigi chenga, pata taarifa zote zinazohusu network.

Kuanzia mwaka wa kwanza hadi mwaka wa mwisho unakomaa na network ama kwa hakika utakuwa vizuri sana baada ya kumaliza chuo kuliko yule anayehangaika na vyote leo yupo Business management kesho hacking kesho kutwa Software development. Wahenga walisema mtaka yote kwa pupa hukosa yote.

Komaa na kitu kimoja, hayo masomo mengine yasome kwa ajili ya kunawilisha cheti chako.

 

2. Anza kujitolea mapema.

Usisubiri mpaka umalize chuo ndio uanze kutafuta sehemu ya kujitolea. Chuo ndio sehemu nzuri ya kujitolea ikiwa bado unapata fedha ya kujikimu kuliko ile unamaliza chuo ndio unajitolea yaani hata ukipewa pesa kidogo inaishia kununua dagaa na usafiri.

Fanya ufanyavyo ili mradi upate sehemu uanze kujitolea katika kipindi unamaliza chuo pengine waweza kuajiriwa kwenye hiyo taasisi au kampuni kwa kuwa utakuwa tayari unajua ABC kuhusu mambo yanavyofanyika.

Kuna majukwaa pia ya kidigitali ambayo unaweza kujitolea kwenye makampuni ya nje ikiwa bado uko chuo kama vile SkilledUp Life hapa utatengeneza profile yako na kuapply kazi kulingana na field yako.  

Kipindi wenzako wanahangaika kutafuta kazi wewe unahangaika kupanga mafaili. Ukijitolea mapema utapata uzoefu mkubwa utakaokusaidia baadae kujibu lile swali liuzwalo kwenye chumba cha usaili “una uzoefu wa miaka mingapi”.

3. Noa ujuzi wako kila siku.

Usitegemee tu kile unachofundishwa darasani. Mwanafunzi mzuri ni yule anayetaka kujua nyuma ya pazia pakoje.

Siku hizi kuna majukwaa mengi yatoayo kozi za bure na za kulipia mtandaoni ni wewe na bundle lako tu mfano YouTube hapa kuna kila aina ya kozi unayotaka kujifunza, kuna kila suluhu ya matatizo unayoyapitia.

Pia kuna LinkedIn Learning (Free & premium) na HubSpot Free Courses. Kozi zingine za bure uki-search tu google wanakuletea. Ujue kuna watu wengine wamejiajiri kwa kunoa juzi zao kupitia majukwaa haya haya! 

Usiseme huna bundle mbona ukiingia Insta au Tiktok unamaliza masaa mawili na ushee kutizama short videos? Bundle unalo sema bado hujaamua kuwa serious hebu kuwa serious uone kama utakosa pesa ya bundle.

Kama unataka kupata kubali kupoteza. Hakuna kitu cha bure duniani lazima ulipie.

4. Ishi Maisha yako.

Chuo kuna changamoto moja. Kila kijana anataka aonekane yeye ndio yeye si mtoto wa mkulima si mtoto wa Waziri si mtoto wa mfugaji wote wanataka kuishi sawa.

Mwingine akipiga simu nyumbani laki mbili kwake ni pesa ya chai wakati kwako ni pesa ya kula miezi miwili na hapo unalipa na kodi kabisa.

Lakini ukiwa chuo unataka uishi maisha sawa na wao. Fanya ujikubali, usiishi maisha ya kuigiza kumbuka maisha siyo kuigiza, fuata kilichokupeleka chuo hao marafiki unaoshinda nao leo siku mkimaliza chuo kila mtu ataenda kwao na wewe utaenda kwenu.

Kama serikali inakulipia ada na umebahatika kupewa pesa ya kujikimu (BOOM) itumie vizuri pengine inaweza kukusaidia huko mbeleni.

5. Chagua marafiki wa kuishi nao.

Bwana mmoja alisema nikitaka kukujua wewe ni nani na mwelekeo wako ni upi nionyeshe marafiki zako watano kwamba hao marafiki ni nusu ya wewe.

Kama wanapenda mitoko na wewe utakuwa nusu yake, kama wanapenda kusoma na wewe ni nusu yake, kama wanafanya biashara na wewe ni nusu yake, kama wanapenda kucheza PS na wewe ni nusu yake. 

Hebu angalia marafiki ulionao na mambo wanayoyafanya halafu angalia na yako kama yanatofautiana sana.

Kuwa na marafiki ambao hawaendi njia unayotaka Kwenda ni sawa na kujichimbia shimo la kujilaumu baadae.

Bora ujiengue mapema na haimaanisha uachane nao kabisa. Hapana.

Jiweke kando na fanya mambo kivyako vyako mkikutana sehemu bongeni kama hakuna lililotokea huku ukiwa na moja kichwani.

Usiwachukie wala kujiona wewe ndio mwamba wa Lusaka, maisha siyo hivyo ishi nao kwa akili mana hao rafiki zako ndio wanaweza kukuletea michongo mingi endapo utakuwa na ujuzi zaidi kuwazidi wao.

Chuo ni daraja tu unapita tumia muda mwingi kuifikirie sana kesho kuliko leo yako. Nimalize kwa kusema hakuna anayeijua kesho maisha yako yapo mikononi mwako.

Usalama Mtandaoni ni nini? Umuhimu na Jinsi Ya Kuwa Salama.

Usalama Mtandaoni ni nini? Umuhimu na Jinsi Ya Kuwa Salama.

Inawezekana wewe ni mmiliki wa simu janja, kompyuta au kifaa kingine kama hivyo. Kama hivyo lazima unatumia mtandao kwa shughuli zako mbali mbali iwe kupata taarifa, kuwasiliana, kufanya malipo au kutoa au kupata huduma mbalimbali. 

Lakini je unafahamu kuhusu usalama wako wakati wa utumiaji wa mtandao? Wengi hatufuatilii kuhusu usalama wa mtandaoni hasa kwenye kutoa taarifa binafsi ambazo zinaweza kudukuliwa na kumpa mtu nafasi ya kufanya uhalifu mtandaoni. 

Ushasikia stori za watu au makampuni kuibiwa pesa, akaunti za kijamii au taarifa flani nyeti kwa ajili ya kufanyia utapeli mtandaoni?Hii yote inatokana na ukosefu wa uelewa kuhusu usalama mtandaoni. 

Kama wewe ni mtumiaji mzuri wa mtandao basi Makala hii ni maalum kwa ajili yako kupata uelewa kuhusu usalama mtandaoni. Ni nini na jinsi gani unaweza kujiweka salama mtandaoni.

 Usalama mtandaoni ni nini?

 Ni utumiaji wa mtandao unao fuata kanuni, sheria na tahadhari ili kujihakikishia usalama katika matumizi yako ya mtandao. Hatua hizi husaidia katika ulinzi wa taarifa zako binafsi zidi ya hatari zinazoletwa na matumizi teknolojia na intaneti. Hatari hizo hufaamika kama uhalifu wa mtandaoni ‘Cybercrime’.

 Kuna umuhimu gani wa kuwa salama mtandaoni?

 Kwa sababu vifaa vya kidijitali unavyotumia vinabeba taarifa mbalimbali binafsi ambapo mtu mwingine akizipata anaweza kuzitumia kwa uhalifu. Taarifa hizo zinaweza kuwa nywila,  hifadhidata ‘database’ za matukio mbalimbali au ripoti muhimu.

Taarifa hizi zinaweza kuwa za mtu binafsi, taasisi za umma, mashirika binafsi au Serikali. Endapo kifaa chako unachotumia kitaibiwa au kupotea bila kuwa na ulinzi wowote, basi ni rahisi sana mtu kutumia nafasi hiyo kuchukua taarifa muhimu zilizohifadhiwa na kutumia nje ya kusudi lililopangwa.

Ni kwa jinsi gani mtu anaweza kujiweka salama mtandaoni?

  1. Tambua kundi la kifaa unachotumia kuingia mtandaoni.

i. Kundi la vifaa binafsi kama vile simu janja, kompyuta binafsi au saa janja.

Vifaa hivi hubeba taarifa nyingi, programu na data mbalimbali kukuhusu. Hivyo njia ya kujiweka salama ni kufunga kifaa chako kwa njia za kiusalama zinazojulikana mfano pini namba, nywila, kitambua uso au alama ya kidole.

Kutompa mtu nywila yako uliyoweka kwenye kifaa chako. Usipende kuruhusu mtu yoyote kufungua kifaa chako na kuperuzi kifaa chako kwenye program mbalimbali zilizopo kwenye kifaa chako. Kuhakikisha program zako zimesasishwa kwa toleo la sasa.

ii. Kundi la vifaa vya umma/ ushirika

Hivi vinaweza kua vya ofisini, nyumbani au kwenye sehemu za kutolea huduma ya intaneti kama intaneti café. Mara nyingi huwa ni komputya za mezani na hujumuisha watumiaji Zaidi ya mmoja. Hivyo umakini unatakiwa zaidi.

Kuwa salama kwenye vifaa hivi ni kuhakikisha unatoka kwenye wasifu wako kila baada ya kumaliza matumizi yako. Kutoruhusu eneo la kujaza nywila liwe automatiki kwani litafanya yoyote yule aweze kuingia kwenye akaunti yako bila kizuizi. Pia unaweza kufuta historia yako baada ya kumaliza kutumia. 

2.   Tambua aina ya mtandao umeunganishwa nayo (Binafsi au Pamoja)

Kuna wanaotumia mtandao wa Binafsi na kuna wanaotumia mtandao usio na waya ‘wi-fi’. Mtandao usiokua na waya huruhusu watumiaji zaidi ya mmoja kuunganishwa. Hivyo kuhitaji umakini Zaidi na kujilinda kuepusha kudukuliwa.

Mtandao usio na waya ‘Wi-Fi’ Ukitumia na kujiunganisha ni vyema ukabadilisha jina la kifaa chako na nywila ili watu wasiweze kujiunga bila ruhusa yako.

3.   Uhakiki wa Programu unazotumia

a.       Programu za simu – Programu nyingi huhitaji kujaza taarifa zako ili uweze kutumia. Pia programu nyingine huunganishwa na program nyingine kupata taarifa zako mbalimbali hivyo kuwa salama unahitaji kupakua program kutoka kwa mtengenezaji anayetambulika.

b.       Linki za kuingia tovuti mbalimbali- muhimu ni kuhakiki jina sahihi la tovuti ‘domain name’. Kwani wahalifu wengi hubadili jina halisi na kuweka tofauti ndogo ambayo sio rahisi kugundulika.

Hakikisha unafungua linki yenye https mwishoni kuashiria usalama wako. Na sio yenye http maana taarifa zako zitakua wazi.

Unaweza kutumia kifaa chako katika hali ya faragha, hii huzuia kuweka historia ya matumizi. Lakini pia epuka kufanya malipo mbalimbali hasa ya kifedha kwa kutumia kifaa cha umma, kwani ni rahisi kudukuliwa.

Usalama mtandaoni hasa kwa watumiaji wa mitandao kama sehemu yao ya kazi ni muhimu zaidi. Inawezekana ulikua hujui umuhimu wake.

Bado hujachelewa, Anza sasa! Makala hii iwe muongozo wa usalama wa matumizi yako mbalimbali ya mtandao ili kuepukana na uhalifu.  

Faida 5 za Kutumia Mtandao Wa LinkedIn Mbali na Kutafuta Kazi

Faida 5 za Kutumia Mtandao Wa LinkedIn Mbali na Kutafuta Kazi

Linkedin ni jukwaa lenye jumla ya watu wapatao milioni 950 kutoka nchi zaidi ya 200 ulimwenguni. Mtandao huu unakua kwa kasi sana kutokana na fursa mbalimbali ambazo watu wanapata hasa wanaotafuta kazi na watangaza biashara.

Kuna faida gani za kutumia mtandao wa LinkedIn?  Katika makala hii nimeelezea faida tano za kutumia mtandao wa LinkedIn mbali na kutafuta kazi kama ilivyozoeleka kwa wengi.

Kujifunza.

Watu wengi wanajiunga LinkedIn kwa lengo la kutafuta kazi tu hasa vijana wanaomaliza vyuo, jambo ambalo linafanya baadhi yao kuja na mabango ya “Hi everyone, I am looking for new role and would appreciate your support. Thank you in Advance for any connection” baada ya hapo haonekani tena.

LinkedIn ni jukwaa linalokuwezesha wewe kujifunza mambo mengi yamkini hata yale uliyokuwa huyajui kutoka kwa wataalamu tofauti tofauti mfano HR, Engineer, Writers, Consultants, Career coach, Doctors, Marketers n.k wote hawa wako Linkedin. 

Uzuri ni kwamba watu hawa hufundisha mambo kadha wa kadha ikiwemo mambo gani ufanye na yapi usifanye kulingana na tasnia zao. 

Mfano HR wanafundisha jinsi ya kujibu maswali ya interview ambayo mara nyingi watahiniwa huulizwa wakiwa kwenye chumba cha mahojiano (Interview)  kama vile “Unafikiri ni kwa nini wewe unafit kwenye hii kazi, tueleze wewe ni nani, tuulize swali kama una swali n.k”

Career Coach wanafundisha vitu ambavyo unatakiwa kujua kabla ya kwenda kwenye interview mfano “Jinsi ya kuelezea ujuzi wako, namna gani unaweza kuhama kutoka kitengo kimoja kwenda kitengo kingine bila kwenda kuongeza Masters wala kwenda kukisomea hicho kitu chuoni”.

Ukiachilia mbali hayo, Linkedin learning inakupa free courses kwa mwezi mzima wa mwanzo baada kujiunga (kusubscribe) Linkedin Premium. Ofa hii ni kwa mwezi mmoja tu baada ya hapo utatakiwa kusitisha au kulipia ili uendelee na huduma (premium). 

Haya yote utajifunza huko huko LinkedIn, ni wewe na utayari wako wa kujifunza. 

Kuongeza marafiki wapya.

Marafiki hawa wanaweza kuwa ni wataalamu wanaokuzidi kimaarifa na kiujuzi, mnaendana au unawazidi kwa lengo la kubadilishana mawazo chanya katika tasnia zenu na pengine kufanya kazi pamoja. 

Mara nyingi urafiki huu waweza kukusaidia kutatua changamoto mbalimbali usizoweza iwe kwa kuongea nao kwenye simu, message au kukutana sehemu ili kujadili zaidi baada ya kujuana huko LinkedIn.

Amini kwamba, milima haikutani lakini ninyi mnaweza kukutana katika namna ambao hukuitengemea, “aah! Kumbe ndo wewe sikutegemea kama tutakutana”. Leo mtakutana linkedIn kesho mtakutana Arusha live, uso kwa uso na huyo ndio anaweza kuwa mwenyeji wako. 

Leo mnaweza kuchati na kushiriki kwenye mijadala yenu pale LinkedIn lakini kesho inawezekana mkafanya kazi kwenye ofisi moja.

Kukuza Jina.

Kama hujulikani kuanzia ngazi ya wilaya, mkoa, kitaifa basi Linkedin inakupa fursa ya kujulikana siyo tu ngazi ya kitaifa bali ngazi za kimataifa. Linkedin inakufungulia dunia kuwa unachotaka.

Huhitaji kukwea pipa mpaka marekani ili ujulikane unahitaji kuandaa maudhui yako yenye mvuto, yenye kutatua tatizo fulani, yenye kufundisha au yenye kuburudisha. Kwa kufanya hivi watu watapata kukujua wewe ni nani na unafanya nini.

Hivyo itakuwa rahisi kwako kupewa fursa za kazi kutokana na kile unachokiandika LinkedIn kwa sababu watu tayari watakuwa wanakujua. Hiyo ndiyo maana ya kukuza jina LinkedIn.

Watu hununua kwa watu wanaowajua. Vile watu hawaamini sana mitandao itakuchukua miezi, mwaka mpaka watu waanze kukuamini na kukupa fursa au ufanye nao kazi. Kuza jina lako mtandaoni kwanza watu wakufaamu fursa za kazi zitakuja baadae. 

Kukuza uandishi wako.

Baada ya kumaliza mtihani wa mwisho chuoni suala la kuandika huishia papo hapo. Pengine uandishi kwako ni changamoto sana je, ni sehemu gani unaweza kufanya mazoezi ya kujiendeleza kuandika au kufanya uandishi wako uwe umenyooka, fasaha?

Ukiniuliza mimi nitakwambia ni linkedin, kwa nini? Kwa sababu inakupa nafasi kubwa ya kuandika maneno mengi kadri uwezavyo, kuna sehemu ya posts na newsletter ambapo unaweza kuandika na kukuza uandishi wako siyo kama ilivyo X (Twitter).

Wengi hushindwa kujitosa na kiingereza chao cha you know kisa wataonekana si wasomi sana au utasikia ni vigumu sana kukaa na kuandaa maudhui kwa kuandika, practice makes more perfect anza hivyo hivyo mwisho wa siku mambo yatakaa mkao. Mchicha nao ulianza kama ua mdogo mdogo unajifunza itafika wakati wewe mwenyewe utaoni kama mchezo tu.

Ikumbukwe: Mipaka ya lugha yako mipaka ya ulimwengu wako. Kingereza ni lugha ya kimataifa, kibiashara hivyo kwa namna yoyote ile inabidi uijue. 

Kutunza kumbukumbu. 

Nadhani ulishawahi kuweka kumbukumbu zako kwenye diary, notebook au kwenye application mbali mbali pia hata Linkedin yaweza kutumika kwa miradi hiyo. Ukiweka post yako kule itakaa milele mpaka utakapoamua kuifuta mwenyewe.

Muda wowote waweza kuirejea, kujikumbushia au kutunza mawazo yako kule iwe kwenye post yako au kwa kuacha comment kwenye post za watu wengine.

LinkedIn is a note taking app.  

Mwisho, LinkedIn ni mtandao wenye faida kedekede hasa kwa mtu mmoja na kampuni kwa ujumla.

Usijifungie ghetoni au kukaa offline kisa hujapata kazi, ukiwa LinkedIn utajifunza mengi sana.

Siri Ya Mafanikio Mtandaoni, Nunua Kitabu Hiki

Siri Ya Mafanikio Mtandaoni, Nunua Kitabu Hiki

Naitwa Shukuru Amos. Kabla sijakudokezea siri ya mafanikio mtandaoni, naomba nikupe stori yangu fupi: Hapo Mwanzo hapakuwa na jina Shukuru Amos kwenye uso wa dunia ya digital marketing. Yote yalianza mara baada ya mimi kutangaziwa kwamba nina wiki mbili zimebaki nifanye mtihani wa mwisho chuoni.

Hapo ndipo nikagundua ninaelekea mtaani nikiwa jobless and unemployed. “Nikimaliza chuo nitafanya nini?” nilijiuliza.

Nikisema nirudi kwetu kijijini, hakukuwa na ishu ya kufanya. Nikisema nibaki ndani ya jiji la Dar es Salaam, hapa pia hakukuwa na ishu ya kufanya.

Je, nilimua lipi? Nilianzaje? Nimejifunza yapi ndani ya miaka mitano kufikia hatua ya kazi kunifatuta mimi na si mimi kutafuta kazi? Yote haya nimeeleza ndani ya kitabu changu kiitwacho; MBELE YA MUDA: Kama Unataka Mali, Utaipata Shambani.

Tunakoelekea, kila mtu atalazimika kuingia kwenye uchumi wa digitali. Ndipo kutakuwapo kilio na kusaga meno kama hujajiandaa.

Shukuru Amos

Tatizo la Vijana wengi Tanzania ukiwemo wewe

Vijana wengi wana shida ya kujiwasilisha kizembe kwenye maombi ya kazi. Tatizo hili linajidhihirisha pia wanapoingia kwenye soko la uchumi wa digitali.

Haiwezekani mtu una followers 10,000 halafu bado unalalamika kuhusu kukosa kazi. Haiwezekani! Lakini ndiyo shida waliyonayo Freelancers wa Kitanzania. Wengi hawana jina lenye hadhi.

Pamoja na ukweli kwamba uchumi wa digitali unaweza kutufanya kuondokana na ukosefu wa ajira na umasikini, inasikitisha kwamba vijana wengi hawajawahi kupata pesa mtandaoni.

Kama unachangamoto hii, una matatizo manne. Nitakupa mawili hapa (mengine ndani ya kitabu):

  1. Unashindwa kuandika kwa sauti yenye mamlaka.
  2. Unashindwa kuonyesha ukomavu wa fikra kupitia maandishi.

Hapo zamani za kale, walikuwepo watu wanaitwa Alchemists. Hawa walikuwa wanajaribu kubadili madini ya risasi kuwa dhahabu. Lakini mwishowe walikata tamaa. It was impossible turning lead into gold. Mimi sitaki wewe ukate tamaa.

Unaweza kubadili content kuwa jina lenye hadhi na kufanya fursa zikutafute. Siyo wewe kuhangaika kutafuta fursa muda wote.Kufahamu tatizo la 3 na la 4, pamoja nini cha kufanya —nunua kitabu changu.

Maoni ya baadhi ya waliosoma kitabu hiki

Je, Mitandao inalipa au hailipi?

Hebu Fikiria Upo Kwenye Stage Hii:Huna wasiwasi juu ya wapi na namna gani utapata mteja, au ajira. Unapata meseji (qualified leads) 4-9 kwa wiki za watu ambao wako interested kufanya kazi nawewe.

Uko vizuri kwenye kushawishi mkikutana au kwenye simu. Watu ni wengi kuliko unavyoweza ku-handle. Huna tena habari za kuandaa CV, kujitolea au kwenda kuongeza mastaz. Unafanya kazi ukiwa nyumbani au popote. Foleni za Jiji tena basii.

Hayo yote yanawezekana. Mimi mwandishi wa kitabu hiki nipo kwenye stage hii sasa. Sitafuti kazi. Kazi zinanitafuta! Kama mimi kijana kutoka uskumani ndani ndani nimeweza, hata wewe unaweza. Mitandao inalipa ndugu yangu!

Umechoka kuandika Dear Sir/Madam bila kupata majibu?

Kama kutuma maombi ya kazi umeshatuma sana. Vyeti unavyo vya kutosha. Pengine umejaribu mitandao lakini unaona kama wembe ni ule ule. No job!

Ndani ya MbeleYaMuda, nimeandika “Usiwe mtafuta kazi maarufu” kwani hakuna mtu anasema “Muone fulani huwa anatafuta kazi”. Watu husema “Muone fulani huwa anafanya hicho kitu.”

Mbele Ya Muda ni kitabu chenye MADINI yatakuyokufanya ujione ULICHELEWA kuanza kufaidika na NGUVU ya Mtandao.

Kimeandikwa na mimi, the most followed Tanzanian marketer on LinkedIn. Ambaye uandishi na uwasilishaji wangu unafuatiliwa sana kwenye mtandao huo.

Moja kati ya mada zilizomo ndani ya MbeleYaMuda, utajifunza Personal Branding, Uandishi na Uwasilishaji unaoleta Pesa na KUHESHIMISHA Jina. Pia utajifunza kuhusu Biashara Mtandaoni, Saikolojia ya Maudhui na mengine tufanye siri yako. Maana yana ukakasi kidogo kuyasema hadharani. Lakini ndiyo siri ya mafanikio mtandaoni.

Majibu, Maujuzi na Maujanja YOTE Utayapata ndani ya kitabu hiki.

Kitabu hiki kwasasa kinapatikana kwa mfumo wa soft copy pekee. Bei ni Tsh 29,900/=

BOFYA HAPA kununua kitabu, au BOFYA HAPA kunicheki WhatsApp. Au nipigie 0742 085 089.

Scam Alert: Tanzlite is NOT hiring online employees for part-time, and we don’t have any foreign representative

Scam Alert: Tanzlite is NOT hiring online employees for part-time, and we don’t have any foreign representative

Attention: During the week starting 13th of November 2023, many people in Tanzania received WhatsApp messages from a foreign number. The person identified to be a representative of an agency from Tanzania.

Our agency, Tanzlite Digital was among the brand names these automated messages used. Some of the messages read:

My name is Ayanna, I am a Senior Representative Officer at Tanzlite Digital Marketing agency . Our company is recruiting part-time/full-time online employees, Our job is very simple, May I take a few minutes of your time? I would like to share a job offer for you.

FAKE!

Hello Hello I am Cynthia a Senior Representative of of Tanzlite Digital Ltd . Our company is hiring online employees for part-time. Can I share salary and job details?

FAKE!

And another similar message came from Vinza Masana

First of all, this is a PURE Scam. Just look at it yourself. It’s bullshit.

People have already lost money!

Our response to this fraud

Let us reiterate what we posted on all of our social media channels:

First: There are no titles or hierarchical structures at Tanzlite Digital. If you receive a message that sounds corporatey, like some senior somebody from us —that’s NOT us. We don’t have Vinza Masana, Ayanna, or any representative with a foreign number.

Second: Tanzlite doesn’t reach out to anyone. People reach out to us.

Third: We single out talent from LinkedIn only. Not in your WhatsApp app.

Fourth: There’s no one in a foreign country with a foreign number representing us.

And lastly: You’re too smart to be scammed by this automated WhatsApp message. It’s the AI version of “Ile hela tuma kwenye namba hii.”

What should you do when you receive such a scam message?

Block and report that number to WhatsApp IMMEDIATELY. Don’t even waste time to reply because it is probably not a human on the other side. Just automated messages reaching you by guessing random numbers. They will probably come with a different name and company but, you have been warned.

Jinsi ya Kutumia BOOM la Chuo Vizuri Kwa Manufaa Yako Baadae

Jinsi ya Kutumia BOOM la Chuo Vizuri Kwa Manufaa Yako Baadae

BOOM linatoka lini? Hili ni moja ya swali ambalo wanafunzi wanaodhaminiwa na serikali hujiuliza sana hasa wakati wanaanza shahada zao au pindi BOOM linapochelewa kutoka.

BOOM ni nini? 

BOOM ni fedha ya kujikimu inayotolewa na serikali kwa wanufaika wote wa mkopo kupitia Bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB -High Education Student’s Loans Board). 

Makato ya Mshahara baada ya kuajiriwa.

Wanafunzi wengi wamekuwa wakitumia fedha hiyo yamkini hata hawajui madhira watakayokuja kukutana nayo hapo mbeleni.

Hasa asilimia kumi na tano ya makato (15%) ya mshahara wao kutoka Bodi ya mikopo HESLB mara baada ya kuajiriwa, bado hujaweka NSSF, PSSSF, kodi ya nyumba, chakula n.k

Walioko maofisini wanaelewa vizuri athari za kukatwa kwa mshahara wao kila baada ya mwisho wa mwezi. Mshahara wa laki saba ukitoa makato makato unabakiwa na laki sita. Changamoto zingine pia huwa hazikosekani.

Ninachojaribu kusema ni kwamba ewe mwanafunzi uliyeko chuo na umebahatika kupata fedha ya kujikimu ali maarufu kwa jina la BOOM, itumie vizuri muda huu kwani kuna wengine hawapewi kabisa hiyo fedha, kila kukicha wanahangaika, leo kwa mjomba kesho kwa shangazi. 

Fedha hiyo inaweza kuwa msaada mkubwa katika maisha yako endapo utaitumia katika muktadha nzuri. 

Cha kusikitisha wengi huwa hatujali nini kitatokea huko mbeleni ilimradi tu umepata BOOM na maisha yanaenda. “Kula bata mpaka kuku aone wivu” ni sauti kutoka kwa vijana baadhi baada ya kupata BOOM.

Usishangae sana kuona mhitimu siku anamaliza chuo hata ile pesa ya kumrudisha nyumbani hana. Haya mambo yapo.

Kila mtu ana malengo yake chuoni, usiwe bendera kufuata upepo

Ndiyo, najua kila mtu chuoni huwa ana malengo yake, yawezekana kwao zipo, yupo chuo kukamilisha ngazi za elimu. Je, wewe kijana mwenzangu kutoka ndani ndani huko Ifunde unataka uishi kama wao!.  

Kuna maana gani ya kununua rundo la nguo, nguo za bei ghari wakati hata maarifa ya kukusaidia kuiishi kesho yako huna? Ni kwa kuwa BOOM limetoka au ni kwa sababu marafiki zako wanafanya hivyo?.

Wengine wanashindana kuvaa vizuri, kutafuta pisi kali (msichana) kisa wamepata BOOM. Jiulize, mpaka sasa umefanya nini cha maana kutokana na hilo BOOM unalopewa?

Kumbuka chuo ni daraja tu unapita, bado una safari ndefu ya kutembea na inawezekana hao vijana wenzako unaokula nao bata chuoni usiwaone tena katika maisha yako. Usiwe bendera kufuata upepo.

Wakati mwingine huwa ni vigumu sana kwenda kinyume na marafiki zako uliozoeana nao toka mwanzo. Lakini ukweli ni kwamba mwisho wa siku kila mtu atashika njia yake. 

Chaguo ni lako uishi maisha ya kuigiza ili uendane na wenzako au ukubali kuishi maisha yako – ujikubali. Kingine, usiangalie tu miaka utakayokuwepo chuoni bali miaka baada ya kumaliza chuo.

BOOM ni mtaji. 

Kama wewe ni kijana kutoka familia ya wakulima, Boom ni fedha unayoweza kuitumia kuwekeza katika kilimo, kununua ardhi, ufugaji au kuwasaidia wazazi wako kuliko kula bata chuoni. 

Kununua vifaa mbalimbali vitakavyokupa sehemu ya kuanzia baada ya kumaliza chuo mfano computer, kamera, vifaa vya stationary n.k. 

Jifunze maarifa mapya mtandaoni yatakayokuongezea ujuzi wa kile unachokisomea kuliko kuchoma pesa kwa ajili ya kuangalia short videos Tiktok. 

Kuanzisha biashara ndogo ndogo kama kuuza karanga, vifaa vya kieletroniki, nguo au chochote kitakachokuwa ndani ya uwezo wako, maarifa utakayoyapata hapa ni sawa na mtu anayefanya internship kwenye kampuni fulani.   

Hujawahi kuona mwanachuo anauza karanga, popcorn, simu + covers? Naam, tumia BOOM katika miradi hiyo. 

Siku njema huonekana asubuhi.