Jinsi ya Kutumia BOOM la Chuo Vizuri Kwa Manufaa Yako Baadae

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted October 15, 2023

BOOM linatoka lini? Hili ni moja ya swali ambalo wanafunzi wanaodhaminiwa na serikali hujiuliza sana hasa wakati wanaanza shahada zao au pindi BOOM linapochelewa kutoka.

BOOM ni nini? 

BOOM ni fedha ya kujikimu inayotolewa na serikali kwa wanufaika wote wa mkopo kupitia Bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB -High Education Student’s Loans Board). 

Makato ya Mshahara baada ya kuajiriwa.

Wanafunzi wengi wamekuwa wakitumia fedha hiyo yamkini hata hawajui madhira watakayokuja kukutana nayo hapo mbeleni.

Hasa asilimia kumi na tano ya makato (15%) ya mshahara wao kutoka Bodi ya mikopo HESLB mara baada ya kuajiriwa, bado hujaweka NSSF, PSSSF, kodi ya nyumba, chakula n.k

Walioko maofisini wanaelewa vizuri athari za kukatwa kwa mshahara wao kila baada ya mwisho wa mwezi. Mshahara wa laki saba ukitoa makato makato unabakiwa na laki sita. Changamoto zingine pia huwa hazikosekani.

Ninachojaribu kusema ni kwamba ewe mwanafunzi uliyeko chuo na umebahatika kupata fedha ya kujikimu ali maarufu kwa jina la BOOM, itumie vizuri muda huu kwani kuna wengine hawapewi kabisa hiyo fedha, kila kukicha wanahangaika, leo kwa mjomba kesho kwa shangazi. 

Fedha hiyo inaweza kuwa msaada mkubwa katika maisha yako endapo utaitumia katika muktadha nzuri. 

ALSO READ:  Je, ChatGPT Inaweza Kudukua Taarifa Zako?

Cha kusikitisha wengi huwa hatujali nini kitatokea huko mbeleni ilimradi tu umepata BOOM na maisha yanaenda. “Kula bata mpaka kuku aone wivu” ni sauti kutoka kwa vijana baadhi baada ya kupata BOOM.

Usishangae sana kuona mhitimu siku anamaliza chuo hata ile pesa ya kumrudisha nyumbani hana. Haya mambo yapo.

Kila mtu ana malengo yake chuoni, usiwe bendera kufuata upepo

Ndiyo, najua kila mtu chuoni huwa ana malengo yake, yawezekana kwao zipo, yupo chuo kukamilisha ngazi za elimu. Je, wewe kijana mwenzangu kutoka ndani ndani huko Ifunde unataka uishi kama wao!.  

Kuna maana gani ya kununua rundo la nguo, nguo za bei ghari wakati hata maarifa ya kukusaidia kuiishi kesho yako huna? Ni kwa kuwa BOOM limetoka au ni kwa sababu marafiki zako wanafanya hivyo?.

Wengine wanashindana kuvaa vizuri, kutafuta pisi kali (msichana) kisa wamepata BOOM. Jiulize, mpaka sasa umefanya nini cha maana kutokana na hilo BOOM unalopewa?

Kumbuka chuo ni daraja tu unapita, bado una safari ndefu ya kutembea na inawezekana hao vijana wenzako unaokula nao bata chuoni usiwaone tena katika maisha yako. Usiwe bendera kufuata upepo.

ALSO READ:  Ajira Ni Tatizo: Fanya Mambo Haya Ukiwa Chuoni

Wakati mwingine huwa ni vigumu sana kwenda kinyume na marafiki zako uliozoeana nao toka mwanzo. Lakini ukweli ni kwamba mwisho wa siku kila mtu atashika njia yake. 

Chaguo ni lako uishi maisha ya kuigiza ili uendane na wenzako au ukubali kuishi maisha yako – ujikubali. Kingine, usiangalie tu miaka utakayokuwepo chuoni bali miaka baada ya kumaliza chuo.

BOOM ni mtaji. 

Kama wewe ni kijana kutoka familia ya wakulima, Boom ni fedha unayoweza kuitumia kuwekeza katika kilimo, kununua ardhi, ufugaji au kuwasaidia wazazi wako kuliko kula bata chuoni. 

Kununua vifaa mbalimbali vitakavyokupa sehemu ya kuanzia baada ya kumaliza chuo mfano computer, kamera, vifaa vya stationary n.k. 

Jifunze maarifa mapya mtandaoni yatakayokuongezea ujuzi wa kile unachokisomea kuliko kuchoma pesa kwa ajili ya kuangalia short videos Tiktok. 

Kuanzisha biashara ndogo ndogo kama kuuza karanga, vifaa vya kieletroniki, nguo au chochote kitakachokuwa ndani ya uwezo wako, maarifa utakayoyapata hapa ni sawa na mtu anayefanya internship kwenye kampuni fulani.   

Hujawahi kuona mwanachuo anauza karanga, popcorn, simu + covers? Naam, tumia BOOM katika miradi hiyo. 

Siku njema huonekana asubuhi.

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite