Katika zama hizi za digitali, watu hufanya utafiti wa bidhaa wanayotaka kununua kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Utafiti wao mwingi unahusisha kutafuta (Search – au kugugo) kwenye injini za utafutaji pamoja na kusikiliza ushauri wa watu ambao wamewahi kutumia bidhaa hiyo.
Kwa wenye biashara zenye website, ipo njia ya kunasa wateja kwa haraka. Njia hii ni kutumia matangazo mguso (PPC ads). Njia hii huitaji kusubiri miezi kadhaa kuanza kupata watembeleaji kwenye tovuti yako kama ilivyo kwenye mpango wa SEO.
Ukiwa mfanyabiashara, kuonekana kwenye matokeo ya utafutaji (search results) ni fursa kubwa ya kutangaza bidhaa au biashara yako ili watumiaji hawa wa mtandao (internet) waweze kuona biashara yako.
Maana yake kama hauko online, watafutaji hawa watakukosa na mshindani wako aliyeko online atapata fursa ya kunasa hawa wateja.
Injini za utafutaji kama vile Bing, Google na Yahoo zina huduma ya kuweka matangazo kwenye matokeo ya utafutaji (search results)
Kitaalamu inaitwa Paid Per Click Advertising (PPC). Ni aina ya kutangaza bidhaa au huduma kwa kununua maneno maalum (keywords) yanayohusu biasha yako ambapo utaweza kuonekana endapo mtumiaji akitafuta kwa kutumia maneno hayo. Maana ya jina Pay Per Click ni kwamba unalipa endapo mtu atabofya tangazo lako na kuzuru tovuti yako.
Matangazo haya hukaa mwanzoni mwa ukurasa wa matokeo ya utafutaji (search engine result page), yakifuatiwa na matokeo ya kawaida (organic results). Pia yanaweza kuonekana sehemu nyingine ndani ya results page.
Tazama picha ifuatayo:
Ufafanuzi kuhusu picha ya juu.
Ni uwanja wa kutafutia (search bar) ambapo mtu ametafuta ‘stuffed animals’
Vertical navigation (hapa unachagua uone matokeo ya Picha, Bidhaa, Video, Maeneo au Habari)
Taarifa kuhusu matokea ya utafutaji(search results information)
Haya ndiyo matangazo mguso (PPC Ads)
PPC Inafanyaje Kazi?
Matangazo haya hutolewa kwa ushindani au mnada. Wenye biashara hushindania maneno kwa kuweka dau kubwa juu ya mwenzake ili apate kuonekana endapo mtu ‘atagugo’ kwa kutumia maneno hayo.
Hivyo, mambo mawili ni muhimu kuzingatiwa;
Dau lako kulinganisha na dau la mwenzako (auction)
Ubora na uhalisia wa huduma yako (quality and relevance)
Hebu tuangalie mfano ili upate kufahamu zaidi:
Tuseme unamiliki hoteli na unataka kutangaza kupitia matangazo mguso. Washindani wako wengine kama kampuni mbili hivi nazo zinataka kutangaza. Hapo
Best hotels in Serengeti
Serengeti National Park
Tanzania adventures
Best hotels in Tanzania
Luxury resorts in Tanzania
Tuseme wote mmechagua maneno hayo juu. Wewe ukaweka dola mbili per click, mshindani wako akaweka dola nne kwa kila mtu atakapo bofya tangazo. Hapa maana yake mwenzako atakuwa anaonekana zaidi kuliko wewe kwenye paid search results.
Mara nyingi gharama za malipo per click hupanda kutegemea na ushindani na eneo unalotaka kutangaza. Kwa mfano, wewe ni Hosting company au Insurance company katika jiji la New York, hapo ushindani kwenye keywords utakuwa mkubwa hivyo utalazimika kuweka pesa nyingi.
Lakini kwa nchi kama Tanzania, makampuni mengi hawatumii PPC advertising, hivyo linaweza kuwa chimbo zuri kwako wewe kunasa wateja. Unaweza kujikuta ni wewe tu unayetangaza katika sekta yako.
Lakini pia kuna vigezo vya ubora na uhalisia wa maudhui na jinsi tovuti yako ilivyoundwa. Hivi vinaweza kuathiri uwezekano wa kuonekana kwenye matokeo ya utafutaji. Ikumbukwe lengo la google ni kutoa matokeo sahihi kwa watumiaji wake na kuhakikish user experience ni ya kuridhisha. Hivyo unaweza kuwa na dau dogo kuliko mwenzako lakini bado ukaoneka.
Vipi kuhusu ufanisi wake?
Ufanisi wa aina hii ya matangazo ni bora zaidi kwasababu hapa unatangaza kwa watu ambao tayari wako interested na biashara yako. Yaani unalenga wateja ambao tayari wanatafuta huduma yako (customers who are actively searching for your product or service).
Kupata umaarufu (awareness and recogntion) wa biashara yako mtandaoni inachukua muda kutegemea na maarifa na jitihada ulizo wekeza. Lakini kwa kutumia matangazo mguso (PPC) unaweza ukajulikana na kuanza kuvutia wateja kwa muda mfupi sana. Ni jambo la siku au masaa tu.
Unahitaji kufahamu zaidi au kufanyiwa huduma hii kwenye biashara yako? Wasiliana nasi HAPA
Mtandao wa WhatsApp umetutoa mbali sana. Kutoka kwenye status za kuandika mpaka status za picha na video. Kutoka kwenye magrupu yenye ukomo wa watu 60 mpaka sasa magrupu ya watu nyomi hadi 257.
Ni wazi kwamba mtandao wa WhatsApp umezidi kuwa bora ili kuendelea kuwafurahisha watumiaji wake. Bora ukose application zingine kwenye simu lakini si WhatsApp.
WhatsApp imekuwa zaidi ya sehemu ya kuchat na kutumiana jumbe zenye kufurahisha (meme), bali ni fursa ya kibiashara kwa wajanja.
Watu wanataka kuuza, watu wanataka kujiweka karibu na wateja wao. Wengine ndio kwanza wanafungua biashara zao wakitafuta namna ya kujitangaza. WhatsApp imekuwa kimbilio la wajasiriamali wengi wa kitanzania.
Watu wameanzisha magrupu ya WhatsApp kwa lengo la kuendesha semina na mafunzo mbalimbali. Kuendesha vikundi vya kukopeshana, maarufu kama ‘vikoba’. Vilevile magrup haya yanatumika kuhamasisha watu kujumuika kwenye matamasha na warsha mbalimbali.
Siku hizi hata vikao vya Sendoff na harusi vinaendeshwa kwenye magrupu ya WhatsApp. Kama bado umejiunga kwenye magrupu ya kipuuzi, basi umebaki wewe tu na wapuuzi wachache. Wenzako tunasaka fursa!
Yani siku hizi kupata namba ya mtu ni rahisi sana kwa sababu anajua baadaye utaona matangazo ya biashara yake kwenye status. Wala si kwa ubaya, ni katika harakati za kutafuta masoko na kujipatia riziki. Wewe ambaye huna cha kutangaza usione kero.
Hatufahamu ni mazuri yapi mengine wamiliki wa mtandao wa WhatsApp wametuandalia, lakini kizuri kimojawapo ni kuhusu application ya WhatsApp Business.
WhatsApp Business ni nini na ina tofauti gani na WhatsApp ya Kawaida?
Kwanza kabisa, WhatsApp Business ni application halali inayomilikiwa na kampuni ya WhatsApp Inc. Hii sio kama zile WhatsApp GB na zinginezo (not a third-part App) ambazo huwa zinakataliwa. Hii ni maalumu kwa wafanya biashara na wajasiliamali wanaotaka kupromote biashara zao pamoja na kuimarisha mahusiano na wateja wao. Lakini hata wewe usiye na biashara unaweza kuitumia kwa mawasiliano ya kawaida.
Makampuni kama Bloomberg na Mwananchi wanatumia WhatsApp Business API (huduma advanced hii ni huduma ya kulipia) kutuma updates kwa subscribers wao moja moja kwenye inbox zao.
Sasa tuiangalie WhatsApp Business kiundani zaidi. Vitu ambavyo utavipata ndani yake ni kama ifuatavyo;.
Business profile
Ujumbe automatic wa salamu
Customer Management
Takwimu/statistics
Majibu ya haraka (quick replies)
Business Profile
Ukiangalia profile ya mtu anayetumia WhatsApp Business utaona ina muonekano tofauti na ile ya kawaida. Hapa utaona vitu kama jina la biashara, maelezo ya biashara (business description), location pamoja na siku na masaa anayofungua biashara yake. Hivi ni vitu ambavyo huwezi kuviona kwa mtu anayetumia WhatsApp ya kawaida.
Customer Management
Hapa unaweza kuchambua na kupangilia namba za WhatsApp ulizonazo katika makundi mbalimbali ya wateja. Kwa mfano unaweza kumwekea alama (label) kama vile mteja mpya, aliyelipa, asiyelipa, aliyetoa oda mpya na aliyemaliza oda yake.
Ujumbe Automatki wa Salamu
Hapa unaweza kutengeneza ujumbe wa salamu utakao kuwa ukitumwa kwa kila anayekutumia meseji. Ili kuondoa kero na usumbufu, ujumbe huu hutumwa endapo tu hamjawasiliana kwa kipindi cha siku 14. Ujumbe huu wa salamu unaweza kuwa unaelezea kwa ufupi juu ya shughuli unayofanya. Ni namna ambavyo wewe utapenda iwe.
Takwimu
Katika application ya WhatsApp Business, unaweza kupata takwimu kuhusu meseji ulizotuma. Utaweza kuona idadi ya meseji ulizotuma, zilizofika na zilizosomwa.
Quick replies and away message
Sikushauri utumie sana hii feature kwani humfanya mtu ajisikie kama ana wasiliana na roboti badala ya mtu. Kama namba yako ya mawasiliano ya kawaida ndiyo hiyo hiyo unatumia kwa biashara zako bora usitumie hii setting kwani si kila mtu ni mteja wako.
Jinsi ya kuwezesha WhatsApp Business
Ni rahisi sana kuseti business profile kwenye application ya WhatsApp Business. Unachotakiwa kufanya ni kwenda Playstore ama Appstore na kudownload WhatsApp Business. Baada ya hapo fungua application na uende kwenye Settings.
Kama unatumia android bofya kwenya vidoti vitatu upande wa juu kulia >Settings > Business settings > Hapo utaona setting zote unazotaka kufanya.
Mwisho…
Dunia ya sasa ni dunia ya kujiuza (simaanishi kujiuza unakofikiria wewe). It is all about branding yourself. Kama hutokuwa na ujasiri wa kusimama na kuonyesha ujuzi na maarifa yako, unataka nani akufanyie hivyo?
WhatsApp ni moja kati ya jukwaa zuri kuji-brand. Mara moja moja si mbaya kupost utani (meme) lakini isiwe kila siku wewe ni wa kupost upuuzi tu. Usifikiri ni utani tu, people are more likely to associate you with the things you post online. Jenga taswira chanya ili uweze kuvuta fursa zije upande wako.
Teknolojia imeleta mambo mengi. Mojawapo ni kuibuka kwa kazi ambazo hazikuwepo kabla. Vilevile imeweza kubadili namna ya utendaji kazi wa kazi nyingi tulizozizoea na kuzifanya ziwe tofauti kabisa. Teknolojia imeathiri kila kitu.
Moja kati ya taaluma mpya zilizoweza kuibuka kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia ni taaluma ya kutafuta masoko na kuuza bidhaa au huduma kwa njia ya kidigitali (Digital Marketing). Taaluma hii kwa hapa nchini Tanzania bado ni ngeni na wengi hawaifahamu. Hata vyuo vyetu bado havijaanza kufundisha somo hili ipasavyo. Lakini sio jambo la kushangaa kwani ni jambo la kawaida kwa vyuo vyetu kuachwa nyuma na kasi ya mabadiliko ya teknolojia.
Digital Marketing ni nini?
Mara nyingi ninapojitambulisha kwamba ninafanya digital marketing, wengi huniuliza maana ya digital marketing.
Katika makala hii utaweza kufahamu maana ya Digital Marketing pamoja na kufahamu sehemu unayoweza kujifunza elimu hii bure kabisa na kupatiwa cheti kinachotambulika duniani. Kama wewe ni mfanyabiashara unayetamani kuingia kwenye ulimwengu wa kutafuta masoko kidigitali au unataka kujifunza Digital Marketing kama taaluma basi makala hii inakuhusu. Twende sambamba.
Kwa tafsiri ya kawaida, Digital Marketing inaweza kutafsiriwa kama;
Utafutaji masoko, kuuza pamoja na kutangaza bidhaa au huduma kwa kutumia majukwaa ya kidigitali (online platforms) kama vile mitandao ya kijamii na tovuti.
– Tanzlite
Angalia maana kutoka kwenye mtandao hapa chini;
The use of numerous digital tactics and channels to connect with customers where they spend much of their time online
– HubSpot
The marketing of products or services using digital technologies, mainly on the internet, but also including mobile phones, display advertising, and any other digital medium
Digita Marketing kwa majina mengine huitwa Internet Marketing, e-commerce au Online Marketing.
Kwanini digital marketing ni muhimu?
Sababu zinaeleweka. Siku hizi kila mtu yuko online. Kila mtu yuko kwenye mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, Instagram na mingineyo. Mitandao imejaa watu. Wakiwemo wateja wa bidhaa yako.
Hii ina maana gani kwa wafanyabiashara?
Wafanyabiashara na wajasiriamali wanatakiwa kujiongeza. Siku hizi mambo ni digitali, hivyo biashara nazo hazina budi kuendeshwa kidigitali. Hauwezi ukaweka mabango barabarani au kubandika kwenye magari wakati watu wanatumia muda mwingi kutazama kwenye simu janja zao.
Hata redio na televisheni zimekuwa hazitumiwi sana na watu. Siku hizi ni mwendo wa YouTube na muziki wa kudownload. Kila kitu kiganjani.
Kama mfanyabiashara unaekwenda na wakati, ni lazima kuingia kwenye ulimwengu wa uuzaji na utafutaji masoko kidigitali. Wateja wako wapo Instagram na Facebook kwanini wewe usiwepo?
Vipengele vinavyo husisha Digital Marketing
Ukisikia digital marketing, mara nyingi Inahusisha vipengele vifuatavyo;
Kutafuta masoko kupitia mitandao ya kijamii (Social Media Marketing)
Hili ndio swala ambalo watu wengi humaanisha wakiongelea Digital Marketing. Makampuni mengi yamefungua akaunti za mitandao ya kijamii kwa lengo la kujiweka karibu na wateja wao pamoja na kupata wateja wapya, kujenga mahusiano mazuri na wateja wao pamoja na kuzungumza nao wanapokuwa na maswali.
Kupitia mitandao ya kijamii, kampuni hutengeneza maudhui kwa mfumo wa picha, video au maandishi ili kuwafahamisha wateja kuhusu huduma za kampuni, kutoa ofa na promosheni mbalimbali kwa wafuatiliaji wake (followers) Fahamu zaidi kuhusu kazi ya social media na majukumu yake hapa.
Uuzaji kupitia barua pepe (Email marketing)
Umeshawahi kuambiwa Subscribe to our newsletter? Basi hicho ndio kitu tunaongelea hapa kwa haraka haraka. Barua pepe ni mtandao mkongwe ambao umekuwepo kwa miaka mingi sasa. Wafanyabishara huomba kukusanya barua pepe za watembeleaji wa tovuti zao ili baadaye waweze kuwashirikisha juu ya fursa na ofa mbalimbali za kampuni husika.
Kwa kuwa watu wengi wanatumia simu za mkononi, barua pepe hazina budi kuandaliwa katika muonekano unaofaa kwenye simu (mobile friendly). Bila kufanya hivyo ni bora usitumie njiaa hii kwani email zako hazitasomwa na utawafanya wateja kujiondoa (unsubscribe) kwenye orodha ya mawasiliano yako.
Kujitangaza kupitia Tovuti (Website)
Tovuti ndio njia kuu ya kupeleka biashara yako online. Kama ulivyofungua duka la nguo pale Kariakoo, basi unaweza ukalihamisha duka hilo hilo ukalipeleka mtandaoni na wateja wanaweza kukutembelea, kuchagua nguo na kufanya manunuzi bila kufika dukani kwako Kariakoo. Maajabu sio? Fikiria tovuti kubwa kama vile alibaba au eBay. Au hata tovuti za ahapa nyumbani kama vile Kupatana. Jaribu kuwa na tovuti yako ujionee faida zake. Hakikisha website yako ni nyepesi kufunguka, na inapendeza kwenye simu za mkononi.
Matokeo ya haraka (Search Engine Optimization)
Kuweka biashara yako mtandaoni si swala la kufungua tovuti tu. Bali tovuti yenye ubora unaotambuliwa na injini za utafutaji (Search Engines). Hii inajumuisha mambo kama maudhui (content) unayoweka kwenye tovuti na ubora uliotumika kujenga tovuti yako (programming). Tovuti iliyojengwa vibaya haiwezi kuoneshwa kwenye matokeo ya utafutaji (Search Results) hivyo kukufanya usiweze kujulikana na kupelekea kukosa wateja.
Fanya utafiti mdogo kuangalia kama tovuti yako inatambuliwa (indexed) na injini ya utafutaji ya Google kwa kuingiza maneno yafuatayo kwenye sanduku la kutafutia (Search bar) site:yourdomain
Mfano; site:tanzlite.com
Hakikisha matokeo yatakapoletwa na Google yanaonyesha kurasa (pages) zote zilizopo kwenye tovuti yako. Usipoona kitu ujue una kazi ya kufanya.
Matangazo ya Kulipia (Sponsored Ads)
Kama umeshawahi kukutana na post ya page ambayo huja-follow imeandikwa “Sponsored”, basi hayo ndiyo matangazo ya kulipia. Ni aina ya digital marketing ambapo unatumia pesa kufikisha tangazo lako kwa watu wengi zaidi. Hii ni inasadia kwa mwenye biashara ambaye ndiyo anaanza kuweza kufikia wateja kwa muda mfupi sana.
Unaweza kutumia matangazo ya Facebook, matangazo ya Instagram, Google n.k. Habari njema ni kwamba matangazo haya hayana gharama sana; mfano Facebook na Instagram watakudai dola moja tu kwa siku kama kiwango cha chini cha matumizi.
Matangazo mguso (Paid Per Click Ads)
Yanaitwa matangazo mguso kwa sababu malipo hufanyika mara tu mtu anapo bofya tangazo lako. Hii ni aina ya kutangaza bidhaa au huduma kwa kununua maneno maalum (keywords) yanayohusu bidhaa yako ambapo mtu akitafuta kwa kutumia maneno hayo, biashara yako inaweza kuoneka juu kwenye matokeo ya utafutaji (search results)
Graphic design
Ukiingia WhatsApp au kwenye mitandao mingine ya kijamii, utakutana na picha zilizonakshiwa kwa maneno na rangi nzuri. Hii kitaalamu Graphic design (sijui kwa Kiswahili tunaitaje). Basi kila mwenye brand au mwenye event yake anataka kuporomote kwa nakshi zenye kuvutia macho ya watu na kuwashawishi kuisambaza (share) kwa wenzao.
Kutangaza biashara kwa njia ya video (video marketing)
Ukiondoa Google, ni search engine gani nyingine ya pili kwa ukubwa? Je ni Bing? Au Yahoo? Jibu ni YouTube. Watu wanaangalia video kwa wingi sana siku hizi . Kwa mfanyabiashara mjanja hii ni fursa kubwa. Unaweza kutumia video kuonyesha ujuzi wako katika huduma unayofanya au kuwaonyesha watu kuhusu mambo yanayojiri ofisini kwako. Pia kutangaza biashara yako YouTube si lazima uwe na video clip, —nitalifafanua hili kwa undani zaidi katika makala zijazo.
Kutangaza biashara kupitia watu wenye ushawishi mtandaoni (Influencers)
Watu maarufu mtandaoni wana nguvu ya kushawishi na kuweza kubadili mtazamo wa watu juu ya jambo fulani. Hivyo makampuni na brand mbalimbali zinatumia watu kama hawa kutangaza biashara zao na kufikia watu wengi. Hapa Tanzania kuna watu kama Idris Sultani ambaye ni balozi wa kampuni ya Uber.
Kukua kwa influencer marketing kumekuja kwa sababu kuu moja; mitandao ya kijamii ni watu, na watu wanapenda kushiriki (interact) na watu wenzao kuliko kampuni. Hivyo makampuni yanajitahidi kuwa karibu na watu kwa kuwatumia watu maarufu kukuza biashara zao.
Wapi unaweza kujifunza elimu ya Digital Marketing
Elimu ya Digital Marketing ni moja kati ya elimu ambayo mtu hauhitaji kuwa na degree ya miaka mitatu chuoni. Lakini faida zake ni kubwa hasa katika kipindi hiki ambacho wahitimu wanatoka vyuo wasijue nini cha kufanya mtaani. Nikushauri leo, anza kujifunza Digital Marketing. Hapa chini nimeorodheasha sehemu tatu ambazo unaweza kusoma online course za digital marketing na mambo mengine mengi.
Ingia mtandaoni leo, chagua kozi na uanze kusoma. Ukikwama mahali au ukihitaji ufafanuzi zaidi, usisite kuwasiliana nasi. Namba zetu zipo kwenye tovuti hii ukurasa wa mawasiliano. Pia tutaendelea kutoa mafunzo kuhusu Digital Marketing kupitia mfululizo wa makala zetu za Kiswahili na Kiingereza.
Hitimisho
Digital Marketing ni habari njema kwa biashara za karne ya 21. Ni njia rahisi ya kujitangaza, kuuza na kujipatia wateja kwa urahisi. Mara nyingi unaweza kufanya bila hata gharama yoyote. Kwa wewe unayehitaji maarifa mapya yasiyo na ushindani mkubwa kwa sasa, jaribu hii fursa. Makala zinazofuata tutaelezea kiundani kuhusu mambo haya ambayo tumeyagusia kwa muhtasari.
Maisha yanakimbia kwa kasi sana. Miji inazidi kuwa ya kisasa na yenye kupendeza. Umri nao unatutupa mkono vilevile.
Siku hizi ukilala, ukiamka kuna jambo jipya limeibuka. Mitindo tofauti tofauti ya mavazi, muziki na mengine inakuja na kuondoka kama maji yatiririkayo chini ya daraja la mto uendao kasi.
Ukija upande wa teknolojia ndio usiseme kabisa. Leo iPhone imetoka mpya kesho Samsung katoa kitu kikali zaidi. Hujakaa sawa Huawei anamtikisa Mmarekani kwa teknolojia ya 5G. Hapa tunaoteseka ni sisi. Hela zenyewe ziko wapi za kuweza kuwa na kila toleo jipya? Wacha tubaki na tecno zetu bwana!
Ninafahamu unatumia mitandao ya kijamii hasa ile maarufu kama Instagram, Facebook na Twitter. Huenda ukawa umekutana na makala hii kwenye moja ya mitandao hiyo.
Lakini kuna mtandao mmoja unakuja kwa kasi sana kwa sasa. Unaitwa TikTok. Endelea kusoma kuona ni nini kipya juu ya mtandao huu.
Takwimu zinasemaje kuhusu mtandao wa TikTok?
Kwa kipindi cha miaka minne tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, TikTok imeweza kuwa na watumiaji zaidi ya milioni 500 duniani kote. Wengi wa watumiaji hawa wakiwa ni vijana.
Ripoti ya Globalwebindex ya mwaka 2019, inaonyesha asilimia 41 ya watumiaji wa TikTok wana umri kati ya miaka 16 na 24 (Globalwebindex, 2019). Kati ya watumiaji hao, watu zaidi ya milioni 150 hutumia application hiyo kwa siku.
TikTok inawapa watumiaji uhuru wa kutengeneza vipande vifupi vya video (visivyozidi sekunde 15) vikinakshiwa na nyimbo na urembo mwingine (filters) wa kuvutia kwa kutumia simu zao za mkononi. Video hizi zimejaa furaha na ucheshi (funny).
Ukitofautisha na mitandao mingine kama Twitter na Instagram, mitambo (algorithm) ya TikTok inakuonesha vitu unavyovitaka tu. Sio mara unakutana na post ambayo hata hujui imetoka wapi kama inavyotokea huko Twitter na Insta. Pia matumizi ya hashtag yanatamba sana kwenye mitandao huu.
Ukiitizama vizuri application ya TikTok utaona ina muonekano sawasawa na application inayoitwa Musical.ly. Hii ni kwa sababu TikTok ambayo ni kampuni ya Kichina, iliinunua application ya Musical.ly ili kuweza kuwafikia watu wengi hasa vijana wa kimarekani.
Swali; Je TikTok inaweza kuwa fursa mpya kwa wafanyabiashara?
Kwasasa TikTok haina mfumo wowote unaowezesha kuweka matangazo ya kulipia (sponsored ads) kama tunayoyaona huko kwenye mitandao mingine.
Lakini kama tunavyofahamu, hakuna kitu cha bure. Nionavyo mimi, jukwaa hili halitakuwa la bure kwa mda mrefu.
Kwa kuwa mtandao huu unapendwa na vijana wengi ambao ndio wenye nguvu ya ushawishi katika masoko, ninaona kuna kila dalili ya makampuni makubwa (brands) kuishawishi ikubali TikTok ikubali matangazo.
Baadhi ya takwimu zinatabiri mtandao wa TikTok utakuja kuteka na kuizidi mitandao kama vile Instagram na Snapchat.
Changamoto kubwa ya mitandao ya kijamii ni tabia yake ya kubadilika kila mara, kwa kuja na mifumo mipya au kupotea kabisa kama mtandao uliokuwa ukimilikiwa na kampuni ya Google, uliofahamika kwa jina la Google+.
Lakini pia ni lazima tukubaliane na ukweli kwamba hatuwezi kukwepa social media. Mitandao hii imewapa nguvu watumiaji kuwa na uhuru wa kuchagua ni namna gani wanataka kupokea taarifa. Hivyo kama mfanyabiashara unaetafuta kukuza jina la biashara yako na kufikia wateja wengi zaidi, huna budi kuwekeza kwenye moja ya mitandao hii.
Palipo na wengi pana fursa nyingi. Wewe kama mfanyabiashara, unajiona uko tayari kuwafata wateja wako walioko TikTok? Au utawasubiri wakirudi Insta na Fb?
Mwanafalsafa maarufu wa Kijerumani, Karl Marx aliwahi kuonya kwamba teknolojia itakuja kuondoa kazi wanazofanya watu. Kwamba watu watakuwa hawana kazi za kufanya.
Hivi karibuni kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, imedhihirika kuwa maono ya msomi huyu hayakuwa sahihi.
Ni kweli kwamba teknolojia imechukua kazi nyingi zilizokuwa zikifanywa na binadamu hasa zile zenye uhitaji mdogo wa kufikiri kama vile kubeba mizigo viwandani. Siku hizi kuna maroboti yanayofanya kazi kwa ufanisi na kwa muda bila kuchoka kuliko binadamu.
Lakini pia kuna ukweli mwingine. Teknolojia imetengeza na kuboresha kazi nyingi zaidi kulinganisha na zile ilizoziondoa. Mojawapo ni hii kazi inaitwa Social Media Marketing. Mtu anayefanya kazi hii anaitwa Social Media Manager, au Social Media Coordinator.
Ulishawahi kujiuliza ni nani huwa anapost kwenye account ya Instagram ya BBC, Millardayo au account za taasisi kama UNICEF? Basi hiyo ndiyo kazi yenyewe tunayoizungumzia hapa.
Social Media ni kipengele mojawapo muhimu katika suala zima la digital marketing.
Kutokana na kukua kwa matumizi ya mitandao ya kijamii miongoni mwa watu, imeweza kushawishi watu na biashara zao kuingia kwenye Social Media kwa lengo la kushirikiana na kukuza uhusiano na wateja wao pamoja na kupata wateja wapya.
Majukumu ya Social Media Manager
Majukumu ya social media manager ni pamoja na kusimamia na kuendesha akaunti za mitandao ya kijamii ya kampuni au watu maarufu celebrities. Haya ni baadhi ya majukumu muhimu;
Kuandaa maudhui (picha, video, maneno) kwa ajili ya kusambaza kwenye mitandao ya kijamii
Kujibu comments na maswali ya followers
Kushiriki (engage) na wafuatiliaji (followers) kwa niaba ya kampuni
Kuandaa promosheni na matangazo ya kulipia (campaigns) ili kufika watu wengi mtandaoni.
Kukuza jina la brand au kampuni
Kujenga na kuimarisha mahusiano mazuri baina ya kampuni na wateja wake
Kuvutia wateja kufuatilia tovuti za kampuni (lead generation)
Ifahamike kwamba kwenye kazi za Social Media, majukumu ya Social Media Manager, Social Media Specialist na Social Media Strategist yanatofautiana. Lakini kwenye makampuni madogo madogo hasa hap Tanzania unaweza ukajikuta unavaa kofia zote hizi peke yako.
Vigezo na mambo muhimu ya kuzingatia ukiwa Social Media Manager
Hauhitaji kuwa na degree kufanya kazi hii, japo baadhi ya waajiri wanaweza kupendelea mtu mwenye elimu ya juu. Jambo zuri ni kwamba unaweza kujifunza mtandaoni kuhusu maarifa haya na kuwa vizuri katika kazi yako.
Lakini mambo muhimu katika kazi hii ni kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu mitandao mbalimbali ya kijamii. Mitandao hii inatofautiana kuanzia aina ya maudhui na watumiaji wake. Kwa Mfano Instagram ni mtandao unaopendwa na vijana, lakini mtandao kama LinkedIn ni jukwaa la wasomi. Kufahamu tofauti hizi kunakuwezesha kujua mbinu za kuwakilisha maudhui kulingana na jukwaa husika.
Mitandao ya kijamii ni watu. Kama unavotakiwa ujifunze kuishinna watu katika maisha halisi basi ndivyo ilivyo pia ukiwa online. Isiwe kila siku unapost biashara yako tu. Watu hawapendi (don’t be too selly). Kuwa mbunifu.
Jifunze kila siku mambo mapya yanayopendwa huko mitandaoni. Usilenge kupata followers tu, bali followers ambao wako interested na unachokifanya. Ukizingatia haya utaleta matokeo yenye kuridhisha kwa mwajiri wako.
Biashara na matangazo ya karne ya 21 yanategemea sana teknolojia. Tunaishi ulimwengu wa dijitiali hivyo kila kitu hakina budi kufanywa kidijitali.
Unaweza kuwa na biashara yako au kampuni yako inayotoa huduma ama bidhaa imara na uhakika kabisa lakini usipotumia bidii kujitangaza ama kujiweka online, unaweza kuzidiwa na watu ambao huduma zao hazina ubora zaidi yako.
Kujitangaza (au kutafuta masoko) kimtandao ni njia rahisi na isiyo gharama kuwafikia watu wengi zaidi. Ukweli ni kwamba usipofanya matangazo ya biashara yako, yote uyafanyao yataishia kwa watu wachache tu wanaokuzunguka.
Nenda na wakati
Siku hizi mtu akitaka msaada wa jambo fulani wazo la kwanza kumjia ni kushika simu yake na kuperuzi kuhusu akitakacho. Hapo ndipo huweza kukutana na majibu ya swala alitakalo mtandaoni.
Fikiria wewe ndiyo hauko mtandaoni, mtumiaji huyu wa internet atakufahamu vipi? Atafahamu vipi una duka la nguo Kariakoo? Badilika. Nenda na wakati, hamia ulimwengu wa digitali. Wazungu wanaita ‘Digital Marketing’ mbinu ya kutafuta masoko na kujitangaza kupitia majukwaa ya kimtandao kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, email, whatsapp na kadhalika.
Unaanzia wapi?
Ni rahisi. Ingawa waweza kutumia pesa panapohitajika, kujitangaza mitandaoni ni bure kabisa. Ni kama vile ulivyo na akaunti facebook bila malipo yoyote. Cha msingi ni wewe kujifunza mbinu za uendeshaji na kuchagua njia ipi inakufaa zaidi
Miliki tovuti/website yako
Tovuti hasa kwa mashirika, makampuni na biashara kubwa ni kitu cha lazima. Hii huongeza hadhi ya kampuni kwa ujumla. Tofauti kubwa kati ya tovuti ama website na mitandao mingine ya kijamii ni namna ya kuweka maudhui.
Kupitia tovuti, mtu anaweza kupata taarifa kwa kina kuhusu kampuni au bidhaa. Pia kwenye tovuti kunaweza kufanyika shughuli kama manunuzi ya mtandaoni, kuandikisha watu kwa ajili ya program, newsletter na kadhalika.
Unatengenezaje tovuti? Ni rahisi. Kuna watu na makampuni mengi yapo kukusaidia kufungua tovuti yako. Sisi Kampuni ya Tanzlite Digital tunatengeneza website za kisasa kwa bei nafuu ili kukusaidie wewe na biashara yako katika ulimwengu wa digitali.
Mitandao ya kijamii
Karibia kila mtu yuko Facebook au Instagram. Maana
yake ni kwamba soko liko huko kwa sababu ndiko watu waliko. Cha kufanya ni
kupeleka biashara yako huko. Fungua akaunti kwa jina la biashara au kampuni
yako na uanze kujitangaza.
Nini cha kupost ukiwa huko? Hapa ndipo wengi hukosea. Makampuni mengi hapa nchini hayafahamu namna ya kutumia mitandao ya kijamii.
Mitandao ya kijamii ni watu, hivyo wewe kama kampuni unatakiwa ufahamu namna ya kuishi na watu. Fahamu namna ya kushirikiana na watu. Isiwe kila siku unapost kuhusu wewe na bidhaa zako tu. Utawachosha watu. Kuwa mbunifu.
Unaweza ukawa unapost picha za bidhaa zako, picha za wateja wenye nyuso za kuridhika na huduma yako. Kama utakuwa mtundu zaidi waweza tengeneza vipande vifupi vya video. Kumbuka pia hautakiwi kupost mara kwa mara ikawa too much.
Jambo la msingi kuzingatia ni kwamba mitandao ya kijamii ni majukwaa tofauti tofauti yenye maudhui na makundi ya watu tofauti. Ni muhimu kulifahamu hili ili aweze kutambua kipi cha kufanya ukiwa kwenye haya majukwaa.
Boosti tangazo lako kupitia Sponsored Ads
Kama ndiyo kwanza unaanza na wateja hawakuji na huna followers wengi, njia rahisi ya kufikia watu ili waone unachouza ni kulipia tangazo. Kama huwa unaona post ya page ambayo huja-follow imeandikwa “Sponsored”, basi hayo ndiyo matangazo ya kulipia. Bei ya kutangaza ni rahisi tu; kwa upande wa Facebook na Instagram kiwango cha chini ni dola moja tu (Tsh 2400*)
WhatsApp pia ni fursa kubwa
Kwa kaiwaida WhatsApp hujumuishwa kwenye kundi la mitandao ya kijamii. Lakini kiuchambuzi zaidi, WhatsApp pamoja na majukwaa mengine kama Telegram na Messenger yanaitwa private messaging platforms. WhatsApp imekuwa kimbilio la wajasiriamali wengi wa kitanzania. Kupitia magrupu na status whatsapp, watu wanatangaza bidhaa zao na kupata wanunuzi. Soma zaidi jinsi ya kutumia WhatsApp Business hapa
Weka biashara yako kwenye Google My Business
Kampuni ya Google wana mfumo wa kukuwezesha kuweka biashara yako kwenye ramani ya Google ili watu wa karibu na eneo lako waweze kukuona wakitafuta huduma au bidhaa inayoendana na yako. Pia wanaweza kuacha maoni kama vile kukupa five star rate ili kuongeza visibility yako mtandaoni.
Pia zipo tovuti zingine zinazokuwezesha kuorodhozesha biashara au bidhaa yako kama vile Kupatana, na Zoom Tanzania.
Kuwa mbunifu katika maudhui (Content Marketing)
Karibia kila mtu anaandika maudhui mtandaoni. Iwe ni mstari mmoja kama status za facebook na whatsapp laikini yote ni maudhui. Kinachokuja kutofautisha kati ya maudhui mengi yanayoandikwa kila siku mtandaoni ni aina na stadi za uandaaji maudhui hayo.
Nichukulie mfano wa mchekeshaji maarufu nchini, Idris Sultani, kuna wakati huandika posts kwenye ukurasa wake wa instagram akitangaza makampuni kama Uber. Uandishi wake ni mwepesi na wenye ucheshi, lakini hapo ameweza kutangaza biashara.
Kwa makampuni na taasisi mbalimbali unaweza kuajiri muandaa maudhui na mwongozaji wa akaunti za kijamii za kampuni. Hili ni jambo muhimu sana katika ulimwengu wa mawasiliano ya kidigitali.
Kampuni yetu ina wataalamu wa masuala ya Digital Marketing ambao wanaweza kukurahishia kazi kuandaa yote haya. Kazi yako ni kufanya biashara, sisi tunaimarisha uwepo wako mtandaoni (online visibility)
Amua sasa!
Siku hizi mambo yanaenda kidigitali, hivyo hata biashara yako haina budi kuenda na wakati.
Kama uliwahi kujaribu tovuti au mitandao ya kijamii na haukupata matokeo mazuri basi kuna mahali haukufanya kwa usahihi. Tafuta wataalamu wakusaidie. Unapitwa wateja kwa kushindwa kuwa online. Amua sasa!