Je ni Nini Hatima ya Wale Wanaocode Kwenye Ulimwengu wa AI?

Je ni Nini Hatima ya Wale Wanaocode Kwenye Ulimwengu wa AI?

Kila sehemu AI, AI, AI inaenda kuchukua nafasi za wale wanaocode (Developers). Hata kipindi google inaanza watu walitabiri kuwa developers wengi watakosa kazi. 

Je, developers walikosa kazi? AI ni kama google tu. Kwa nini uogope wakati maendeleo ya sayansi na technolojia yanaibua fursa zingine mpya ambapo developers wanahitajika ili kurahisisha zaidi maisha ya watu waendane na ulimwengu wa IoT? 

Mfano. Mobile Application (siku hizi kila mtu anasimu), Integrated secured system (kuunganisha mifumo miwili Mfano, idara ya maji na TRA), IoT (Internt of Things), software, web based system na zingine nyingi zinazotatua changamoto mbalimbali kwenye jamii. 

AI yupo anaweza kunisaidia kufanya vyote hivyo

Ndiyo, lakini kama huna ujuzi wa kucode huwezi fanya kitu chochote kwa sababu vitu vinahitaji uelewa mpana wa source code zinazotumika kutengeneza application, mifumo pamoja na kuhakikisha usalama wa data (encryption). 

Hakuna AI ambayo itaweza kumwondoa developer kwenye nafasi yake, bali itamsaidia asipoteze muda mwingi katika kutengeneza programu zake. 

Mtaalamu wa Ethical hacking occupytheweb aliyeandika kitabu cha Linux Basics for Hackers anasema “AI is not perfect, yet not smarter than you. It’s not going to put you out of job if you’re studying a career in tech. You need to embrace AI as tool, use it like how you use google, or else you’re going to be left behind”.   

Kama ushatumia AI katika coding zako utagundua kuwa, AI inatoa data kulingana na wewe unavyotaka. 

Ubora wa uulizaji wako ndio ubora wa AI kukupa taarifa sahihi vinginevyo itakupa source code tofauti na unavyohitaji, hapo utakomaa na debugging mpaka basi, hata ukiirudishia ili idebug inakuzalishia error zingine kumi.

Wale wanaosema AI inaenda kuchukua nafasi za madeveloper wengi wao hawacode, ndio wapya kwenye game (beginners), wanaoona coding ni ngumu, tena hawa ndiyo wanaopiga makelele balaa.

Wale wanaofaidi matunda ya kucode ni wale wenye title kuanzia nne yaani ni (Front-end and Back-end Developer, Network Administrator, content writer, security expert etc).

Sio lazima ujue vyote kwa ufasaha, vingine ni vizuri ukawa na basic understanding ya ni kivipi zinatumika. Usikae na kitu kimoja tu jaribu kuwa two in one (department).

Saivi kuna AI zinazotengeneza website, Apps je, madevelopers tutakaa wapi?

Je kuna AI inayotengeneza mifumo?

Iko hivi, hiyo ndiyo kazi yako jifunze pia jinsi ya kuzitumia hizo AI na ukiwa kama developer jitahidi kujua vitu kwa undani zaidi, ili hata mtu akikupa kazi uifanye kwa weledi. 

Watu wengi wako shallow. Kama unajua coding na unajua kutumia AI vizuri sisi siyo wenzako tena.

Lugha. Kuwa vizuri kwenye uandishi unaoshawishi, andika content ambazo zitamfanya mtu aseme au ajisemee huyu kijana au huyu binti anajua. Iwe kwenye website, application, software au branding. 

Wengi wanafeli katika eneo hili, lugha ndio itakayokutofautisha kati yako na wengine ikiwemo AI. 

Kuna siku utaajiriwa au utaitwa kufanya marekesho kwenye system ya kampuni fulani, sijui utamuuliza AI? Kumbuka AI ziko limited na hauwezi kuipa source code zote za system ya kampuni hiyo ili itambue tatizo ni nini. Ni wewe na uelewa wako.

Je Chagpt anaweza kuchukua kazi za  Software developers?

Kama utaacha kucode, ukajiunga na kundi la watu wanaosifu na kupiga makelele kwamba AI inaenda kuchukua nafasi za developers. Ni kweli hao hao developers ndio watakaochukua nafasi yako.

Mambo Matano Mwanachuo Anaweza Kufanya ili Kukwepa Unemployed Baadae

Mambo Matano Mwanachuo Anaweza Kufanya ili Kukwepa Unemployed Baadae

Hakuna muda mzuri wa kukabiliana na unemployment kama muda ambao uko chuo.

Wengi huja kulifahamu hili tayari jua limeshazama, muda huo upo nyumbani, pengine hata kupata fedha ya kujikimu au ya vocha ni kipengele yaani kuipata ile buku mbili mpaka uende ukafanye kazi za vibarua ndio uipate.

Kitu kizuri ni kwamba leo hii upo chuo, unapokea boom, tukiongelea suala la bando kwako saivi siyo shida basi tumia muda huu kufanya mambo ambayo baada ya kumaliza chuo usihangaike kutafuta kazi.

Haya ndiyo mambo matano ambayo Mwanachuo unaweza kufanya ili kukwepa Unemployed baadae

1. Jiunge na mitandao ya kijamii muhimu kama vile Linkedin na Twitter

Linkedin au Twitter ndiko maarifa yalipo, huko utakutana na waajiri mbalimbali (Recruiters/Employers). Watu kama hawa inawezekana usiwaone kipindi unaanza ila jinsi utakavyozidi kuonyesha uwepo wako kwenye majukwaa hayo, ndivyo utakavyojiweka katika nafasi nzuri ya kupata fursa. 

Huko utapata kujifunza mambo kadha wa kadha yanavyoenenda kwenye tasnia yako, pia itakusaidia kuelewa mapema ni nini ufanye ili baadae usije kupishana na gari la mshahara.

Itakusaidia kuelewa jinsi mambo yanavyofanyika kwenye industry unayosomea. Siyo unamaliza chuo, unaambiwa nafasi zipo na zinahitaji mtu anayejua vizuri Microsoft Access, ndiyo ukute na wewe ulivipuuzia kipindi upo chuo.

Katika ulimwengu tuliopo simu au laptop yako ni siraha tosha inayoweza kubadilisha historia ya maisha yako, itategemea tu unaitumia kwa namna gani. Jambo la kufanya install app ya Linkedin na Twitter sasa hivi.

2. Ongeza maarifa kupitia Online Courses

Internet imerahisisha maisha, leo hii unaweza kusoma popote ulipo na cheti ukitaka unapewa.

Course yoyote unayoitaka inapatikana mtandaoni ni suala la kuchukua simu na kuingia youtube, andika course unayotaka usome, mfano, Project Management full course, kwa click moja unamaliza course ukiwa na maarifa ya kutosha. Youtube inatoa course bure kabisa.

Pia kuna majukwaa mengi ambayo unaweza kuchukua course unayoitaka kama vile Linkedin learning, simplilearn, CompTIA+, Udemy, Coursera n.k huku unafundishwa real life experience tofauti na mwalimu darasani anaekufundisha ili amalize syllabus.

3. Kuwa vizuri kwenye lugha (written and spoken)

Asilimia 90% ya mazungumzo mtandaoni hufanyika kwa njia ya maandishi, hivyo ni vizuri ukajinoa zaidi katika kuandika na kuwasilisha maudhui/ujuzi wako kwa watu.

Njia nzuri ya kujinoa ni kuanza leo kwa kuandika mawazo uliyonayo kichwani kwenye notebook au applikesheni yoyote ikiwezekana uwe unapost hata kama kiingereza au kiswahili kimekaa upande. Practice makes more perfect.  

Ukiwa chuoni jitahidi kupost kila siku au mara mbili kwa wiki kama vipindi vitakuwa vimebana, ule muda unamaliza chuo, utakuwa na kundi kubwa la watu wanaokuhitaji ufanye nao kazi au uwafanyie baadhi ya kazi zao.

Muhimu: Post vitu vya msingi ambavyo mtu akisoma aseme kweli huyu kijana au huyu dada anajua.

4. Anza kufanya kazi ukiwa bado upo chuo (freelancing au virtual internship)

Tafuta kazi ambazo unaweza kufanya ingali bado unasoma, huu ndio muda wa kujitolee kwenye taasisi, kampuni mbalimbali. Fanya kazi as a freelancer kwenye majukwaa mbalimbali kama vile Upwork, Freelancer, Fiverr, Remototask.

Muda mwingine vitu unavyofundishwa darasani nitofauti kabisa na vile vinavyofanyika kwenye industry, hivyo ni bora kuyajua haya mapema na kuyafanyia kazi ili pindi utakapomaliza chuo isiwe changamoto kwako. 

Usisubiri mpaka umalize chuo ndio uanze kuomba kazi, najua unajua kule nyumbani hali ilivyo yaani kupata kazi ni mtiti, ukimaliza chuo ukaenda nyumbani, ndiyo imeisha hiyo.

5. Kuwa mtu mwenye haiba (personality) ili umma wa digitali uvutiwe na wewe

Kila siku jitahidi kuwa mtu wa tofauti na wengine, fanya vitu ambavyo watu wengi hawavifanyi ilimradi unaviamini, ni halali na hivyo utaonekana kuwa ni mtu wa pekee, na kwa upekee huo utajinyakulia fursa kedekede. Kuwa mtu wa kujifunza kila kukicha kwa kusoma vitabu, articles, hudhuria mikutano, seminar au online events. 

Hakuna chuo kinachoweza kukufanya ukwepe unemployed baadae, zaidi ya kuweka juhudi zako binafsi katika kuitengeneza kesho yako. Hatima ya maisha yako ipo mikononi mwako.

Jinsi Nilivyopata Mteja Linkedin Nikiwa Bado Mwanafunzi

Jinsi Nilivyopata Mteja Linkedin Nikiwa Bado Mwanafunzi

Sikuwahi kuamini kama Linkedin ingeweza kunisaidia kupata mteja kwani wanafunzi wengi tunaamini mtandao pekee hauwezi kukufanya upate kazi zenye maana mpaka uajiliwe kwenye makampuni au taasisi.

Jambo ambalo linatufanya tuwe na mawazo mgando na hatimae tukose fursa zilizo ndani ya uwezo wetu.

Ilikuwaje mpaka nikapata mteja?

Kitu kilichonisadia hadi nikapata mteja ni kupitia posting zangu ambazo nilikuwa nikipost kila mara huko linkedin kulingana na tasnia yangu. 

Hali yangu ya kupost mara kwa mara ndiyo iliyojenga uaminifu, kutosahaulika na kuonekana kuwa mtu ambaye ninaweza kufanya kitu fulani. 

Hivyo, siku moja nimejichokea zangu ghafula napigiwa simu, “Hello! wewe ndiye Anthony? Yes (nilijibu), nimekuona linkedin unazungumzia mambo ya ………. Na nimeangalia kwenye profile yako umejitambulisha kama web developer, hivyo unaweza kunitengenezea website? ….”

Kuanzia hiyo siku nikaamini mambo yanawezekana endapo tu utaweka juhudi, uvumilivu na nguvu katika kile unachokipambania. Linkedin ni mtandao unaoweza kumfanya mwanafunzi apate fursa za kazi as a freelancer hata kama bado anasoma.

Ninawezaje kushiriki katika jumuiya ya Linkedin hali ya kwamba mimi ni Mwanafunzi?

Kama ninaweza kuwa online masaa mawili Instagram au facebook nikiscroll up and down, nashindwaje kuutumia muda huo kuandaa maudhui au kushiriki na wenzangu katika jukwaa la Linkedin? Ule mda ambao wewe uko Tiktok, Facebook, mimi ndo naandaa maudhui halafu baadae naingia kwenye kipindi kama kawaida.

Naweza kusema kwamba kama wewe ni mwanafunzi basi unaweza kujisogeza taratibu kwenye jukwaa hili la Linkedin, mtandao ambao unakufungulia dunia kuwa unachotaka. 

Bila shaka unatamani kujua website niliyomtengeneza mteja, haikiuchukua muda website ikakamilika nayo ni  Better Careers. Tofauti na hilo kuna watu wengi pia walionitafuta inbox hivyo kutokana na uzoefu wangu mchanga baadhi ya fursa nilichengana nazo.

Tofauti na hayo jukwaa hili limenisaidia kujifunza mambo kadha wa kadha kwa kusoma post za watu wengine, kuangalia mabadiliko ya teknolojia yanavyokwenda mbio (AI), kupitia Linkedin learning huwezi amini linkedin ndiyo mtandao ambao mimi nilianzia kusoma Web Development kipindi hicho hata opening tag <> or </> sizijui. 

Linkedin ni mtandao wa watu wenye vyeo vyao, watu wanaojua kingereza vizuri

Kipindi najiunga linkedin sikuwa naelewa wapi nianzie na wapi niishie kwa sababu ukiangalia kila mmoja kwenye post zake alikuwa anatema ng’eng’e hatari. Nikawa najisemea kimoyo moyo aisee huu utakuwa ni mtandao wa watu fulani fulani hivi wenye vyeo vyao.

 Kwa kuwa mwanzo huwa ni mgumu nikiwa kule nilikuwa kama mtazamaji, mzee wa kuscroll down and up yaani nikitaka kuandika post, hizo ng’eng’e kuzipangilia ilikuwa ni issue. 

Mdogo mdogo we mwendo, ayeeya mwendo nikaanza kuandika na kusoma vitabu, unaambiwa mazoea hujenga tabia, ee bwana tabia yangu ya kuandika ilianza kukua taratibu na ndipo upweke wa kusema linkedin ni mtandao wa watu wenye vyeo vyao ukanitoka. 

Unajua kule LinkedIn watu wengi wanatumia kingereza kwa sababu watumiaji wengi wa Linkedin hawajui Kiswahili lakini sasa hivi unaweza kutambaa na Kiswahili kuiteka hadhira unayoilenga.

Njia pekee itakayokusaidia wewe usiteseka na barua za internship wala usisumbuke na ajira baada ya kumaliza chuo ni Linkedin inaweza kuwa miongoni mwake.

Naitwa Anthony Charles natengenza tovuti mbalimbali | Mwandishi, pia nasaidia wanafunzi wenzangu walioko chuo kuhusu namna mbalimbali za kukabiliana na unemployment.

Ifahamu LinkedIn na Jinsi ya Kutengeneza Profile Itakayokupatia Fursa

Ifahamu LinkedIn na Jinsi ya Kutengeneza Profile Itakayokupatia Fursa

Linkedin ni mtandao wa kidigitali ambao unaunganisha watu wa kila aina kutoka pande zote za dunia hasa vijana wanaotafuta kazi, wajasiriamali wanaotaka kukuza biashara zao, kuboresha kazi zao na makampuni yanayotafuta wafanyakazi nayo pia yapo Linkedin.

Unaweza kuchukulia masihara ila wataalamu wengi wako kule yakiwemo makampuni, kule watu waliotengeneza jina wanaingiza pesa bila hata kwenda ofisini kuomba kazi, wengi wanafanya kazi kama freelancer.

Jinsi ya kujiunga linkedin

Kuna namna mbili za kujiunga linkedin, namna ya kwanza ni kusanikisha/kuinstall linkedin app kupitia playstore.  Andika Linkedin app kwenye search bar bonyeza iyo application ya blue kisha install. Baada ya kuinstall endelea na usajili, Linkedin app itaonekana kama hapo chini.

Namna nyingine ni kujisajili kupitia website ya linkedin, bonyeza Linkedin signup jaza taaarifa zinazohitajika, kuwa na kumbukumbu juu ya taarifa unazoziweka ili kuondoa usumbufu unaoweza kujitokeza baadae kama utasahau neon siri.


Sasa tumeweza kujiunga na kusign in, Linkedin watakutumia ujumbe kwenye email yako ili kuthibitisha kama gmail yako iko active, kinachofuata ni kumalizia usajili kwa kujaza taarifa zako ipasavyo kwani hizo taarifa ndizo zitakazokaa kwenye profile yako ya Linkedin

Tayari Tumeshatengeneza Akaunti, Sasa Twende Tukaifanye Profile Yako Iwe ya Kitaalamu.

Awali ya yote Linkedin siyo facebook, huku kidogo inabidi ujiweke katika mazingira mazuri uonekana as a professional, huku ndiko wateja wako walipo na ndiko utakapopata fursa mbalimbali za kukutana na watu, kushare idea, kubadilishana mawazo na watu mbalimbali kulingana na tasnia uliyopo.

Bila kupoteza wakati haya ni mambo muhimu inabidi uyafanye ili kuboresha profile yako.

1.Profile picture.

Hakikisha picha unayoweka kwenye profile inakutambulisha kama mtaalamu kwenye tasnia yako. siyo unapiga selfie ndio unatuwekea kwenye profile, Recruiters, wateja watakuona hauko serious. Picha hiyo iwe karibu na kamera, ionekane vizuri. Picha yako ndiyo utambulisho wako.

2. Banner.

Hapa utaweka background picture, texts au quote inayoendana na fani yako. Size ya background image huwa ni 1128 x 191. Wengine pia huweka namba zao za simu na email. Ni vizuri ukachagua kipi kinafaa uweke kuliko kuacha blank. Angalia mfano hapa chini.

3. Kichwa cha profile yako.

Hapa nazungumzia jina lako kamili na headline title ambayo itaonekana mwanzoni kabisa mwa profile yako. Hakikisha headline inajibu wewe ni nani, unasaidia nini?

Kufanikisha hili angalia hapo juu kushoto kuna kitufe kama kalamu bonyeza hicho na jaza taarifa zinazohitajika. Mfano Headline* yangu ni Built my brand while in college from 500+ to 7k people. Helping you do the same. Web developer & designer | Content Writer.

4. Kazi na Elimu.

Ili kuifanya profile yako inawili vizuri, hapo hapo kwenye profile kuna sehemu imeandikwa Open to work bonyeza hicho kipenseli, halafu weka cheo cha kazi unayofanya (job title) n.k 

Ukishafika kwenye visibility ruhusu recruiters only, hiyo nyingine siyo nzuri kuitumia kama kweli wewe unataka uonekane mtaalamu katika tasnia yako.

5. Experience/uzoefu

Pia utashuka chini kwenye Experience, hapo utaweka shule, makampuni au taasisi ambazo umeshawahi kufanyanayo kazi. Elezea kwa kiasi gani umeshiriki katika kuongeza ujuzi wako, vitu gani ulifanya n.k.

6. About

Hapa inatakiwa uelezee fani yako japo kwa kifupi, weka bayana nafasi uliyopo kwa sasa, unafanya nini, unatatua changamoto zipi, kwa namna gani, uzoefu wako ni upi kisha unaweka vitu ambavyo unaweza kuwasaidia watu wengine. Angalau ianzie aya mbili.

7. Mpangilio/Setting.

Mkono wa kulia juu kwenye profile yako kuna ikoni ya setting, ibonyeze shuka chini kidogo showing profile photo ruhusu kwa linkedin members wote. 

8. Usisahau kuwasha creator mode.

Hapa utaweka vitu utakavyokuwa unaongelea katika machapisho yako ya kila siku. Kwa kufanya hivi naamini kwa asilimia 90 profile yako itaonekana bora na ya kiprofessional zaidi.

Tumalizie, Linkedin pia inatoa fursa ya kujifunza course mbalimbali bure ndani ya mwezi mmoja. Je unapataje ofa hii?

 Ni rahisi tu, pale unapoingia linkedin home page kwa juu mkono wa kushoto kunaonekana profile picture yako, ibonyeze halafu angalia chini wameandika activate premium, pabonyeze halafu endelea na maelekezo. 

Baada ya hapo unaweza kujiunga linkedin learning ukapiga course mbali mbali ukishamaliza unapewa na cheti kabisa, ni wewe tu kufanya maamuzi leo. 

Muhimu: Kuwa makini kwenye Akaunti utakayotumia kwenye premium kama unaona siyo vizuri kutumia kadi yako ya bank unaweza kutengeneza M-Pesa VISA Card bure ndani ya dakika moja.

Baada ya kufanya hivyo inabaki kazi ya kujimwanga kwenye jukwaa kuwakilisha kile ulicho nacho hapa naongelea kupost, kushiriki kwenye mazungumzo na jumuiya ya Linkedin, kuendelea kuwa hai. 

Jinsi AI Inavyoweza Kutumia Sauti Yako Kuzungumza na Mtu Mwingine

Jinsi AI Inavyoweza Kutumia Sauti Yako Kuzungumza na Mtu Mwingine

Baada ya Yombo kusikia neno AI linatamkwa sana huku mtaani ikabidi  amuulize jamaa yake Kadozo ili apate kujua zaidi. 

Hivi ndivyo Mazungumzo yalivyokuwa.

(Kadozo na Yombo ni vijana wanaosoma chuo, BBM)

Yombo: Je, unafahamu chochote kuhusu teknolojia ya AI?

Kadozo: Ndiyo, na nimekuwa nikisoma vizuri kuhusu maendeleo ya kuvutia yanayoletwa na AI, kama ulishawahi kusoma the discovery of fire basi hii ni discovery of AI.

Labda kabla hatujaendelea nikuulize, hivi unajua kwamba AI sasa inaweza kutumia sauti yako kuanzisha mazungumzo na mtu mwingine?

Yombo: Hapana? Mbona hii ni ya kushangaza! Inakuwaje na Inafanyaje kazi?

Kadozo: Vizuri, mifumo ya AI inaweza kuchambua, kuiga sauti ya binadamu au rekodi za sauti ili kuunda mfano wa sauti itayotumika na AI.

Mfano, sauti hii ninayoitoa kama itarekodiwa, AI inaweza kukopi na kutumia sauti hii hii kuzalisha maneno yaliyosanifishwa ambayo katika kuongewa kwake yatafanana sana na sauti yangu.

Yombo: Oooh! Very interesting, Lakini inaanzishaje mazungumzo na mtu mwingine?

Kadozo: Mara tu AI inapokuwa imesanifisha sauti, inaweza kutumia algorithms za usindikaji wa lugha asili kuchambua na kuelewa maudhui ya mazungumzo yenu kisha kuzalisha majibu yanayofaa na kushiriki katika mazungumzo na mtu mwingine. Yaani kama AI itaanza kwa kusema hello! na wewe ukajibu-

Hapo ndipo mazungumzo yanapoanzia kwa sababu itakuwa inajibu na kuuliza maswali kulingana na majibu yako. Kumbuka hapa itatumika tu kama imetengenezwa kwa lengo la kuongea na mtu mwingine.

Cha kuongezea tu ni kwamba ni kivipi sauti yako inaweza kuchukuliwa na AI?

Moja kati ya njia ni kutumia kumbukumbu za sauti yako iliyonakiliwa awali, kama vile sauti zilizorekodiwa za mahojiano au hotubaKisha, AI inatumia teknolojia ya kujifunza ili kujenga mfano wa sauti yako na kuitumia.

Moja ya njia zinazotumika kurekodi sauti yako ni voice cloning . Njia nyingine ni kutumia sauti yako inayopatikana kwenye mitandao ya kijamii.

Kadozo: Kwa hivyo, AI inaweza kimsingi kutumia sauti ya mtu na kuwa na mazungumzo yenye maana na watu wengine?

Kadozo: Ndio, hilo halina ubishi. Unaambiwa huwezi kumnasa samaki aliyefumba mdomo kwa kutumia ndoano.

Kwa hiyo AI inaweza kusikiliza kile mtu anasema, kuiga habari hiyo na kujibu kwa njia ambayo inasimulika kama mazungumzo yanayofanana na ya binadamu.

Yombo: Duh! hii mpya, Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza. Napata kujiuliza maswali mengi sana ya usalama?

Kadozo: Maswali gani hayo tena Mr. Yombo?

Yombo:  Sasa kama ni hivyo mfano si AI inaweza kutumiwa ili kupata taarifa zangu binafsi za shule kama itaiga sauti ya registration officer?

Kadozo: Bila shaka. Matumizi ya AI kufananisha sauti ya mtu yanazua wasiwasi kuhusu faragha, wizi wa utambulisho, na matumizi mabaya ya habari binafsi.

Lakini nikwambie kwamba katika ulimwengu tuliopo usimwamini mtu yeyote anayehitaji taarifa zako, pia tumia “multifactor authentication” ili kama humwelewi umwambie atumie njia ya pili kuwasiliana na wewe.

Kwa kawaida AI ukiiuliza wewe ni ni nani itasema Mimi ni kompyuta program niliyeundwa blablaa.

Hapa chini tulipata kumuuliza ChatGPT na alitoa majibu yafuatayo.

Sasa karibia kila aina ya AI huweza kujitabulisha kulingana na ilivyopangiliwa. Hapa ni rahisi sana kujua kumbe unaongea na AI. 

Mfano, Assume ChatGPT ingebatizwa kwa jina lako la Yombo, hapo juu ingesema “Mimi ni Yombo blablaa” chukulia ndiyo unaongea nayo kwenye simu, hapo si ni rahisi kuamini unaye ongea nae ndiye bwana Yombo? Hivyo ndivyo mambo yanavyoenenda ndugu yangu.

Tunaishi katika wakati ambapo teknolojia inabadilika kwa kasi, na AI inachukua jukumu kubwa katika mapinduzi hayo. Lazima tuwe wazi na tayari kukabiliana na changamoto na masuala mengine yanayoweza kujitokeza.

Yombo:  Hiyo ni uhakika. Nashukuru sana ndugu yangu kwa kunitoa gizani, siku nyingine nitakutafuta tuangazie mambo mengine kwa undani zaidi.

Kadozo: Haina noma mshikaji wangu.

Unaweza ukawa unajua kuwa watu wote wanajua kumbe hawajui. Kama una swali lolote dondosha coment yako hapo chini utajibiwa.

Mbinu Mpya Ya Kupata Kazi Ukihitimu Chuo

Mbinu Mpya Ya Kupata Kazi Ukihitimu Chuo

Soko la ajira ni changamoto kubwa inayosumbua vichwa vya wanafunzi wengi hasa wale wanaohitimu vyuo vikuu katika nyakati hizi. Jambo ambalo linafanya vijana wengi wakose imani ya kufanikiwa tena.

Kwanza ijulikane kuwa degree peke yake sio kigezo cha mhitimu kupata kazi kwa sababu wengi huamini akimaliza chuo kazi ni yake. Sasa hivi bila kujiandaa mapema mambo ni magumu sana, soko la ajira ni gumu.

Hata hivyo, kupenya kwenye soko la ajira ni jambo linalohitaji juhudi, ujuzi na utayari wa mtu mwenyewe. Katika makala hii, tutaangazia jinsi mwanachuo anavyoweza kupenyeza kwenye soko la ajira.

Je, ni nini unachoweza kufanya kama mwanachuo ili kuongeza uwezekano wa kupata kazi?

Mchakato wa kutafuta kazi unapaswa uanze mapema, hata kabla ya kuhitimu. Je wewe ni mwanachuo?

Kama jibu ni Ndiyo, basi unaweza kuanza kutafuta fursa za kazi mapema mtandaoni au kwa kushiriki katika programu, miradi, semina, kuandaa projects na kujitolea katika makampuni.

Kwa kushiriki na watu wengine utapata kuongeza marafiki wapya (connection) ambao baadae wanaweza kuwa ndio daraja lako la kupata kazi.

Pia ukianza kujitolea mapema ukiwa chuo utapata uzoefu wa kazi mapema through internship/freelancing ambao utakusaidia kuwa na ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira pindi tu umalizapo chuo.

Ivi ulishawahi kusikia au kuulizwa hili swali, unauzoefu wa miaka mingapi? chukulia ndio tu umemaliza chuo halafu unaingia interview kuulizwa hilo swali, utajibu nini? Hivyo anza mapema kutafuta makampuni ujitolee au ufanye freelancing ili baadae swali hili lisikusumbue.

Ni nini kinachotarajiwa kutoka kwako katika soko la ajira?

Unaweza kujenga mtandao wako wa kijamii (networking) kwa kuwa na mahusiano mazuri na walimu, wanafunzi wenzako na wataalamu wa tasnia yako. Kupitia mtandao huu, utaweza kupata taarifa za kazi pale zinapopatikana.

Hapa nina maanisha uwe na watu ambao watakuwa wana-support kile unachokifanya. Ukiishi na watu ambao hawasupport unachokifanya maana yake hakuna kazi utapata kupitia wao.

Muhimu: Kwa dunia tuliyopo, kama mwanachuo ataamua kuitumia vizuri mitandao ya kijamii yaani social media platforms kama Linkedin katika kujiuza (personal branding) basi mtu huyu;

Hatakuwa anatafuta kazi bali kazi zitakuwa zinamtafuta yeye by Shukuru Amos.

Soko linahitaji vijana wenye maarifa ya kufanya kazi fulani, kuna kazi zingine hata hazihitaji cheti kikubwa uwe na uwezo wa kutatua changamoto za kampuni husika au uwezo wa kuisadia kampuni ikaongeza mauzo au kupandisha hadhi yake?

Jinsi gani unaweza kuboresha ujuzi wako, kupata maarifa yanayohitajika katika tasnia uliyopo?

Technolojia inabadilika kwa kasi sana hivyo unaweza kutumia mitandao ya kijamii kufuatilia mabadiliko yanayotokea katika tasnia yako na kujifunza ujuzi mpya kupitia kozi mbalimbali mtandaoni ikiwemo Marketing.

Chuoni utapewa Mwongozo tu hivyo kuna kila sababu za kutafuta maarifa zaidi. “Kama elimu ya chuo itashindwa kukufanya kuwa unachotaka basi Professor Youtube na msaidizi wake Google wanaweza”.

Utajiuliza ni kivipi Youtube au google inaweza kukusaidia kutimiza ndoto zako? Unahitaji tu kujua unataka usome nini then weka bundle YouTube anakufungulia dunia kuwa unachotaka.

Je ni sahihi kuweka wasifu wako mtandaoni?

Kutengeneza wasifu wako mtandaoni kunaweza kukusaidia sana katika harakati za kutafuta kazi. Wasifu huo utakuwa hewani 24/7 unasomwa na watu wa aina tofauti tofauti ikiwemo waajiri wako baadae, wateja wako.

Hivyo ni vyema kuweka mawasiliano yako, barua pepe na nambari ya simu katika kurasa zako ili watu wakikuhitaji iwe rahisi kukupata.

Wasifu wako mtandaoni unaweza kuwa fursa nzuri kwa wateja au waajiri wanaotafuta talents mtandaoni kujua zaidi kuhusu wewe, uwezo wako na kitu unachoweza kuwasaidia.

Iwe ni Twiter, Facebook, au LinkedIn we jiweke as a professional wa kitu fulani huwezi kujua huko mbeleni ni fursa gani unaweza kuipata. Who knows what will happen tomorrow?

Nifanye nini ili nitambulike na niweze kupata kazi?

Kujitangaza ni muhimu sana katika ulimwengu wa kidigitali hasa unapokuwa kwenye harakati za kutafuta kazi.

Wewe Mwanachuo unapaswa kuwa na ujuzi wa kujielezea mwenyewe katika majukwaa ya aina yoyote iwe kwa maandishi au kwa kuongea.

Kujifunza jinsi ya kuwa mbele kiujuzi na kimaarifa kunaweza kukusaidia kuwa na ujasiri, uwezo wa kuwasilisha mawazo, kushawishi waajiri wakupe kazi.

Asilimia 90 ya mazungumzo mtandaoni huwa ni kwenye maandishi hivyo ni bora kuwa vizuri zaidi kwenye uandishi.

Bonus: Mtu awaye yote, mwenye kutafuta afueni ya maisha yake, yambidi afanye bidii na juhudi zote katika kutatua matatizo yanayoisibu tasnia yake.