Jinsi AI Inavyoweza Kutumia Sauti Yako Kuzungumza na Mtu Mwingine

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted May 21, 2023

Baada ya Yombo kusikia neno AI linatamkwa sana huku mtaani ikabidi  amuulize jamaa yake Kadozo ili apate kujua zaidi. 

Hivi ndivyo Mazungumzo yalivyokuwa.

(Kadozo na Yombo ni vijana wanaosoma chuo, BBM)

Yombo: Je, unafahamu chochote kuhusu teknolojia ya AI?

Kadozo: Ndiyo, na nimekuwa nikisoma vizuri kuhusu maendeleo ya kuvutia yanayoletwa na AI, kama ulishawahi kusoma the discovery of fire basi hii ni discovery of AI.

Labda kabla hatujaendelea nikuulize, hivi unajua kwamba AI sasa inaweza kutumia sauti yako kuanzisha mazungumzo na mtu mwingine?

Yombo: Hapana? Mbona hii ni ya kushangaza! Inakuwaje na Inafanyaje kazi?

Kadozo: Vizuri, mifumo ya AI inaweza kuchambua, kuiga sauti ya binadamu au rekodi za sauti ili kuunda mfano wa sauti itayotumika na AI.

Mfano, sauti hii ninayoitoa kama itarekodiwa, AI inaweza kukopi na kutumia sauti hii hii kuzalisha maneno yaliyosanifishwa ambayo katika kuongewa kwake yatafanana sana na sauti yangu.

Yombo: Oooh! Very interesting, Lakini inaanzishaje mazungumzo na mtu mwingine?

Kadozo: Mara tu AI inapokuwa imesanifisha sauti, inaweza kutumia algorithms za usindikaji wa lugha asili kuchambua na kuelewa maudhui ya mazungumzo yenu kisha kuzalisha majibu yanayofaa na kushiriki katika mazungumzo na mtu mwingine. Yaani kama AI itaanza kwa kusema hello! na wewe ukajibu-

Hapo ndipo mazungumzo yanapoanzia kwa sababu itakuwa inajibu na kuuliza maswali kulingana na majibu yako. Kumbuka hapa itatumika tu kama imetengenezwa kwa lengo la kuongea na mtu mwingine.

ALSO READ:  Je, ChatGPT Inaweza Kudukua Taarifa Zako?

Cha kuongezea tu ni kwamba ni kivipi sauti yako inaweza kuchukuliwa na AI?

Moja kati ya njia ni kutumia kumbukumbu za sauti yako iliyonakiliwa awali, kama vile sauti zilizorekodiwa za mahojiano au hotubaKisha, AI inatumia teknolojia ya kujifunza ili kujenga mfano wa sauti yako na kuitumia.

Moja ya njia zinazotumika kurekodi sauti yako ni voice cloning . Njia nyingine ni kutumia sauti yako inayopatikana kwenye mitandao ya kijamii.

Kadozo: Kwa hivyo, AI inaweza kimsingi kutumia sauti ya mtu na kuwa na mazungumzo yenye maana na watu wengine?

Kadozo: Ndio, hilo halina ubishi. Unaambiwa huwezi kumnasa samaki aliyefumba mdomo kwa kutumia ndoano.

Kwa hiyo AI inaweza kusikiliza kile mtu anasema, kuiga habari hiyo na kujibu kwa njia ambayo inasimulika kama mazungumzo yanayofanana na ya binadamu.

Yombo: Duh! hii mpya, Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza. Napata kujiuliza maswali mengi sana ya usalama?

Kadozo: Maswali gani hayo tena Mr. Yombo?

Yombo:  Sasa kama ni hivyo mfano si AI inaweza kutumiwa ili kupata taarifa zangu binafsi za shule kama itaiga sauti ya registration officer?

Kadozo: Bila shaka. Matumizi ya AI kufananisha sauti ya mtu yanazua wasiwasi kuhusu faragha, wizi wa utambulisho, na matumizi mabaya ya habari binafsi.

ALSO READ:  Jinsi ya Kupata Wateja Mtandaoni Kupitia Matangazo Mguso (PPC Advertising)

Lakini nikwambie kwamba katika ulimwengu tuliopo usimwamini mtu yeyote anayehitaji taarifa zako, pia tumia “multifactor authentication” ili kama humwelewi umwambie atumie njia ya pili kuwasiliana na wewe.

Kwa kawaida AI ukiiuliza wewe ni ni nani itasema Mimi ni kompyuta program niliyeundwa blablaa.

Hapa chini tulipata kumuuliza ChatGPT na alitoa majibu yafuatayo.

Sasa karibia kila aina ya AI huweza kujitabulisha kulingana na ilivyopangiliwa. Hapa ni rahisi sana kujua kumbe unaongea na AI. 

Mfano, Assume ChatGPT ingebatizwa kwa jina lako la Yombo, hapo juu ingesema “Mimi ni Yombo blablaa” chukulia ndiyo unaongea nayo kwenye simu, hapo si ni rahisi kuamini unaye ongea nae ndiye bwana Yombo? Hivyo ndivyo mambo yanavyoenenda ndugu yangu.

Tunaishi katika wakati ambapo teknolojia inabadilika kwa kasi, na AI inachukua jukumu kubwa katika mapinduzi hayo. Lazima tuwe wazi na tayari kukabiliana na changamoto na masuala mengine yanayoweza kujitokeza.

Yombo:  Hiyo ni uhakika. Nashukuru sana ndugu yangu kwa kunitoa gizani, siku nyingine nitakutafuta tuangazie mambo mengine kwa undani zaidi.

Kadozo: Haina noma mshikaji wangu.

Unaweza ukawa unajua kuwa watu wote wanajua kumbe hawajui. Kama una swali lolote dondosha coment yako hapo chini utajibiwa.

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite