Je ni Nini Hatima ya Wale Wanaocode Kwenye Ulimwengu wa AI?

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted June 25, 2023

Kila sehemu AI, AI, AI inaenda kuchukua nafasi za wale wanaocode (Developers). Hata kipindi google inaanza watu walitabiri kuwa developers wengi watakosa kazi. 

Je, developers walikosa kazi? AI ni kama google tu. Kwa nini uogope wakati maendeleo ya sayansi na technolojia yanaibua fursa zingine mpya ambapo developers wanahitajika ili kurahisisha zaidi maisha ya watu waendane na ulimwengu wa IoT? 

Mfano. Mobile Application (siku hizi kila mtu anasimu), Integrated secured system (kuunganisha mifumo miwili Mfano, idara ya maji na TRA), IoT (Internt of Things), software, web based system na zingine nyingi zinazotatua changamoto mbalimbali kwenye jamii. 

AI yupo anaweza kunisaidia kufanya vyote hivyo

Ndiyo, lakini kama huna ujuzi wa kucode huwezi fanya kitu chochote kwa sababu vitu vinahitaji uelewa mpana wa source code zinazotumika kutengeneza application, mifumo pamoja na kuhakikisha usalama wa data (encryption). 

Hakuna AI ambayo itaweza kumwondoa developer kwenye nafasi yake, bali itamsaidia asipoteze muda mwingi katika kutengeneza programu zake. 

Mtaalamu wa Ethical hacking occupytheweb aliyeandika kitabu cha Linux Basics for Hackers anasema “AI is not perfect, yet not smarter than you. It’s not going to put you out of job if you’re studying a career in tech. You need to embrace AI as tool, use it like how you use google, or else you’re going to be left behind”.   

Kama ushatumia AI katika coding zako utagundua kuwa, AI inatoa data kulingana na wewe unavyotaka. 

ALSO READ:  Jinsi Ya Kumsaidia Mjasiriamali Mdogo Kukuza Biashara Yake Mtandaoni

Ubora wa uulizaji wako ndio ubora wa AI kukupa taarifa sahihi vinginevyo itakupa source code tofauti na unavyohitaji, hapo utakomaa na debugging mpaka basi, hata ukiirudishia ili idebug inakuzalishia error zingine kumi.

Wale wanaosema AI inaenda kuchukua nafasi za madeveloper wengi wao hawacode, ndio wapya kwenye game (beginners), wanaoona coding ni ngumu, tena hawa ndiyo wanaopiga makelele balaa.

Wale wanaofaidi matunda ya kucode ni wale wenye title kuanzia nne yaani ni (Front-end and Back-end Developer, Network Administrator, content writer, security expert etc).

Sio lazima ujue vyote kwa ufasaha, vingine ni vizuri ukawa na basic understanding ya ni kivipi zinatumika. Usikae na kitu kimoja tu jaribu kuwa two in one (department).

Saivi kuna AI zinazotengeneza website, Apps je, madevelopers tutakaa wapi?

Je kuna AI inayotengeneza mifumo?

Iko hivi, hiyo ndiyo kazi yako jifunze pia jinsi ya kuzitumia hizo AI na ukiwa kama developer jitahidi kujua vitu kwa undani zaidi, ili hata mtu akikupa kazi uifanye kwa weledi. 

Watu wengi wako shallow. Kama unajua coding na unajua kutumia AI vizuri sisi siyo wenzako tena.

ALSO READ:  Jinsi Nilivyopata Mteja Linkedin Nikiwa Bado Mwanafunzi

Lugha. Kuwa vizuri kwenye uandishi unaoshawishi, andika content ambazo zitamfanya mtu aseme au ajisemee huyu kijana au huyu binti anajua. Iwe kwenye website, application, software au branding. 

Wengi wanafeli katika eneo hili, lugha ndio itakayokutofautisha kati yako na wengine ikiwemo AI. 

Kuna siku utaajiriwa au utaitwa kufanya marekesho kwenye system ya kampuni fulani, sijui utamuuliza AI? Kumbuka AI ziko limited na hauwezi kuipa source code zote za system ya kampuni hiyo ili itambue tatizo ni nini. Ni wewe na uelewa wako.

Je Chagpt anaweza kuchukua kazi za  Software developers?

Kama utaacha kucode, ukajiunga na kundi la watu wanaosifu na kupiga makelele kwamba AI inaenda kuchukua nafasi za developers. Ni kweli hao hao developers ndio watakaochukua nafasi yako.

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite