Fahamu Namna Nzuri Ya Kutumia Mitandao Ya Kijamii?

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted August 6, 2023

Je, mitandao inakutumia zaidi kuliko unavyotakiwa kuitumia?. Leo hii mtu akinunua simu kubwa (smartphone) kitu cha kwanza anachokimbilia ni kujipost mtandaoni hata kama yuko kitandani, je hivi ndivyo tunavyotakiwa tuitumie mitandao?

Kuwa kwenye ulimwengu wa kidigitali kunafanya watu wengi washindwe kuzikabili hisia zao. Pia wengi hawana uelewa kuhusu namna nzuri ya kuitumia mitandao hii.

Unajipost kila siku mtandaoni, unaeleza hisia zako kuhusu wewe, angali bado kijana ambaye hujui hata kesho yako itakuwaje. Picha isiyo na maadili ukishaipost mtandaoni hiyo imeenda, watu wataiona  na itahifadhiwa kwenye algorithms.

Basi, hata kama unajipost hakikisha hiyo picha inatunza heshima yako na inaleta mantiki kwa mtu yeyote. Muda huo angalau jifunze skills zitakazokusaidia kutengeneza ajira yako mwenyewe.

Mfano, Tuseme kampuni fulani inataka ikuajiri je, ikiangalia picha zako mtandaoni utafaa kweli kupewa hiyo kazi? Kwa sababu jinsi unavyojipost ndivyo unavyojielezea zaidi kuwa wewe ni nani, ni wa aina gani, unafanya nini, unapenda nini, uko makini kiasi gani?

Picha zako mtandaoni ni ushahidi tosha watu kukujua vizuri kuliko unavyojijua.

Mitandao ni sehemu ambayo unaweza kutafuta kupata fursa, kujifunza maarifa mbali mbali kutoka kwa watu wengine.

ALSO READ:  Fahamu Makundi Matatu ya Wateja Mtandaoni (na Jinsi ya Kuwapata)

Itumie mitandao katika miradi hiyo na si kuvimbiana au kujionyesha kana kwamba upo kwenye maonyesho.

Ndiyo maana ni ngumu sana vijana kutoboa kupitia mitandao ya kijamii. Ukiangalia wanigeria au wakenya wanakimbiza soko kimataifa kupitia hii hii mitandao. 

Ziko wapi ajira? Ni sauti ya kila kijana baada ya kuhitimu chuo. Mitandao ni fursa shituka, tangaza kitu kinacholeta mantiki kwa watu usitangaze hisia zako.

Unaweka nini kwenye akili za watu pale wanapoona ulichokipost? Ifikie mahari uwe na fikra za mbali baada ya miaka mitano mbele, kile ulichokipost kitakutambulisha kama nani? 

Tunaishi kwenye ulimwengu wa kidigitali ambao mtu anaweza kufanya kazi remotely, itafika muda baadhi ya ajira kama siyo zote zitakuwa zinatolewa baada ya waajiri kukuona mtandaoni unafanya kitu fulani ambacho wanauhitaji nacho.

Soko la kimataifa linahitaji watu wanaoweza kufanya kazi kama freelancer (mtendaji huria).

Na atakayepata bahati hii ni yule ambae account zake za mitandao ya kijamii inajieleza yenyewe vizuri kuhusu yeye, na yuko active. Hakuna kutuma maombi wala interview labda iwe ni lazima. Mtu huyu atashuhudia message ikiingia au akipigiwa simu zikisema

ALSO READ:  Jinsi ya kukuza biashara yako kupitia mtandao (Digital Marketing)



Habari,

Nimekuona kwenye mitandaoni ukielezea zaidi kuhusu blablaa ah! nimekuwa nikikufuatilia toka muda …, vipi unaweza kunisaidia kufanya hili jambo fulani?

Noah Harari Alisema “We are going to believe more on algorithms than we believe in ourselves”.

Japo watu wengi hawajui ni kwa namna gani google hacking inaweza kutumika kupata taarifa zako nyeti binafsi, ni kwa namna gani active attack inaweza kufanyika kwa mtu binafsi au kwenye taasisi?. Na kibaya zaidi watu wengi hawaamini haya mambo utasikia, hii technolojia bado sana kwetu, nani atani-hack mimi wakati hata pesa sina? Ni sawa lakini haya pia yanaweza kutokea.

Tabia ya kupost maisha yako au familia yako kwenye mitandao siyo nzuri na inaweza kukugharimu baadae.

Si kuna watu wanasoma cybersecurity nchi hii, subiri baada ya miaka mitano tutakuwa na vijana wengi ambao hawana ajira na kazi yao itakuwa ndiyo hiyo KUHACK.

Tumia mitandao ya kijamii katika namna ambayo haitakuja kuharibu heshima yako. Ahsante ndugu.

1 Comment

  1. Michael kwaruga

    Meenda sana ahsante Kwa mafundisho yenu

    Reply

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite