Fahamu Namna Nzuri Ya Kutumia Mitandao Ya Kijamii

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. He Creates Clean, Responsive, and Converting Websites for Business Growth.

Posted August 6, 2023

Je, mitandao inakutumia zaidi kuliko unavyotakiwa kuitumia?. Leo hii mtu akinunua simu kubwa (smartphone) kitu cha kwanza anachokimbilia ni kujipost mtandaoni hata kama yuko kitandani, saa ngapi hajajipost mtandaoni ili wamuone!. Je hivi ndivyo tunavyotakiwa tuitumie mitandao?

Kuwa kwenye ulimwengu wa kidigitali kunafanya watu wengi washindwe kuzikabili hisia zao, jambo lolote linalofaa machoni pake anaona ni vyema kulipost mtandaoni. Wengi hatuna uelewa hasa vijana kuhusu namna nzuri ya kuitumia mitandao ya kijamii katika miradi ya kutusaidia baadae.

Sasa wewe unajipost kila siku mtandaoni aisee, angali sana ujue u bado kijana ambaye hujui hata kesho yako itakuwaje. Picha yoyote unayopost mtandaoni hiyo imeenda, watu wataiona  na itahifadhiwa kwenye algorithms milele na milele hata wajukuu zako ipo siku wataiona.

Hivyo jitahidi sana unapo-post kitu chochote kwenye social media angalau kiwe chenye maadili na inatunza heshima yako na inaleta mantiki kwa mtu yeyote. Kuna siku watu watakujaji kupitia picha hizo ulizopost huko Instagram au Twitter.

Ubaya zaidi saivi mambo yapo kidigitali zaidi kwamba mtu akitaka kukujua zaidi anakusearch mtandaoni akikutana na mambo yako ambayo siyo mazuri basi utapishana na gari la mshahara.

Kuliko kupost picha ya mpenzi wako, familia au kuonyesha maisha yako kwa njia ya picha ni bora ukatumia muda huo angalau kujifunze digital skills zitakazokusaidia kutengeneza ajira yako mwenyewe.

Chukulia mfano huu, kampuni fulani inataka ikuajiri je, ikiangalia picha zako mtandaoni utafaa kweli kupewa hiyo kazi? au watakuona kama mhuni fulani? Hii ni kwa sababu jinsi unavyojipost ndivyo unavyojielezea zaidi kuwa wewe ni nani, ni wa aina gani, unafanya nini, unapenda nini, uko makini kiasi gani?

Picha zako mtandaoni ni ushahidi tosha watu kukujua vizuri kuliko unavyojijua.

Mitandao ni sehemu ambayo unaweza kutafuta fursa za kazi, kujifunza maarifa mbali mbali kutoka kwa watu wengine. Lakini kaa ukijua mtandaoni kuna kila aina ya watu kuna watu kazi yao ni kutoa taarifa za upotoshaji, uchi na nyingine amabazo si rasmi hivyo huko mtandaoni chagua watu wa kuwafollow ili usichanganye mafaili ukaingia kwenye mtego wa panya.

ALSO READ:  Faida 5 za Kutumia Mtandao Wa LinkedIn Mbali na Kutafuta Kazi

Ukiona unapata taarifa ambazo siyo nzuri kwenye feed yako, fanya kuwa unfollow, kuwa block watu wote ambao maudhui yao hupendezwi nayo. Ikiwezekana zima notification za mitandao ya kijamii unayotumia kwenye simu yako ili isikuletee shida, kila dakika notification zinatokeza pale juu kwa hali hii si utakosa f ocus sasa!.

Itumie mitandao katika miradi hiyo na si kuvimbiana au kujionyesha kana kwamba upo kwenye maonyesho.

Ziko wapi ajira? Ni sauti ya kila kijana baada ya kuhitimu chuo. Mitandao ni fursa shituka, tangaza kitu kinacholeta mantiki kwa watu usitangaze hisia zako.

Saa nyingine huwa nasema hata WhatsApp kwa mwanafunzi ni sehemu nzuri ya kujitangaza kuhusu ujuzi wake you never know mtu anayeangalia status yako huenda siku moja atakuwa anafanya kazi sehemu na akakuita kufanya kazi na wewe sababu tu anajua una ufahamu wa mambo fulani. Usipost tu memes fikiria hilo pia.

Kwenye game ya kutafuta kazi mtandaoni huwa iko katika swali hili “unaweka nini kwenye akili za watu pale wanapoona ulichokipost?” Yaani mtu atafikiria nini kuhusu wewe kulingana na ulichokipost. Ifikie mahari uwe na fikra za mbali baada ya miaka mitano mbele, kile ulichokipost kitakutambulisha kama nani? 

Tunaishi kwenye ulimwengu wa kidigitali ambao mtu anaweza kufanya kazi remotely, itafika muda baadhi ya ajira kama siyo zote zitakuwa zinatolewa baada ya waajiri kukuona mtandaoni unafanya kitu fulani ambacho wanauhitaji nacho.

Kutafuta kazi ni kazi. Saivi soko linakoelekea ni kwamba watu wengi watakuwa wanafanya kazi remotely, kama ambavyo freelancer wanavyotafuta kazi akishaipata na kuifanya ndo imeisha.

ALSO READ:  Ifahamu kazi ya Social Media Manager na majukumu yake

Na atakayepata bahati hii ni yule ambae account zake za mitandao ya kijamii inajieleza yenyewe vizuri kuhusu yeye, na yuko active. Hakutakuwa na kutuma maombi wala interview labda iwe ni lazima. Mtu huyu atashuhudia message ikiingia au akipigiwa simu zikisema



Habari,

Nimekuona kwenye mitandaoni ukielezea zaidi kuhusu blablaa ah! nimekuwa nikikufuatilia toka muda …, vipi unaweza kunisaidia kufanya hili jambo fulani?

Noah Harari Mwanahistoria alisema “We are going to believe more on algorithms than we believe in ourselves”.

Wengi bado hawaamini katika hili lakini ndo tunakoelekea miaka mitano ijayo digital platforms zitakuwa ndio kimbilio kwa makampuni, agencies na watu binafsi.

Wewe bado kijana jitahidi profile za akaunti zako ziko safi huku mtandaoni halafu kujipost siyo issue achana nayo.

Kuna kitu kinaitwa Social media profiling hutumiwa sana na wadukuzi wa taarifa mtandaoni, watu wa IT na cybersecurity wanaelewa vizuri, hii inaweza kutumika kupata taarifa zako nyeti, Vitu unavyopost Instagram, Twitter, Tiktok, vinaweza kumpa mdukuzi taarifa nyingi kuliko unavyofikiria japo wewe huwezi elewa.

Na kibaya zaidi saivi watu hawaamini udukuzi, hawaamini kabisa haya mambo ya kuhakiwa utasikia “hii technolojia bado sana kwetu, nani atani-hack mimi wakati hata pesa sina?” siku yakikutokea mimi sitakuwepo lakini nimekwambia haya mambo yapo.

Tabia ya kupost maisha yako au familia yako kwenye mitandao siyo nzuri na inaweza kukugharimu baadae.

Halafu kuna watu wanasoma cybersecurity nchi hii, subiri baada ya miaka mitano tutakuwa na vijana wengi ambao hawana ajira na kazi yao itakuwa ndiyo hiyo KUHACK maybe sharia (Cybercrime Act 2015) iwekewe mkazo.

Tumia mitandao ya kijamii katika namna ambayo haitakuja kuharibu heshima yako bali itakutangaza vyema kwenye digital world.

1 Comment

  1. Michael kwaruga

    Meenda sana ahsante Kwa mafundisho yenu

    Reply

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

Products From Tanzlite