Fahamu Mambo Matano Kuhusu Internship

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a young Web Designer and Developer | Content Writer. Helping Individuals escape unemployment, SMEs grow their visibility online.

Posted October 7, 2023

Internship au tarajali imekuwa ni kimbilio kubwa la vijana wengi wanaohitimu chuo baada ya kukosa kazi.

Lakini ukweli kuhusu internship, vijana wengi wamekuwa wakiamini watapewa kazi moja kwa moja baada ya muda wa internship kuisha bila kujali upande wa pili. 

Hivyo wengi wanaishia kuendelea kupewa nafasi za kujitolea miaka hadi miaka. Kwa nini hawaajiriwi na ni nini hasa wanatakiwa kufanya?

Nimekusogezea mambo matano muhimu kuhusu internship.

Njia inayotumika kupata interns.

Mara nyingi nafasi za internship zinazotangazwa na makampuni hutumia njia zinazofanana sawa na zile zinazotumika kupata wafanyakazi wa kawaida japo interview zao zinatofautiana. Wote mtatuma maombi, mtaitwa kwenye interview na pengine kazi mtakazokuwa mnafanya zitakuwa ni sawa.  

Kwanini mtu wa intern/volunteer usilipwe hata pesa kidogo kiasi cha kuweza kumudu maisha yako ya kila siku? Wengi huenda kujitolea kwa lengo la kupata CV, uzoefu yaani ile dhana ya ili uajiriwe mpaka uwe na experience ya mwaka mmoja au zaidi. Wanasahau thamani yao katika kufanya hizo internship. 

Muda mwingine baadhi ya makampuni hayakupi pesa ya kujikimu kisa huna uzoefu wa kutosha, unajikaza kisabuni kwa imani ya kwamba siku moja utaajiriwa, kumbuka mambo yanabadilika inawezekana kazi uliyoisotea miaka ikaja kuchukuliwa na teknolojia. 

Zingatia haya maswali mawili ukiwa intern, lengo lako haswa la internship ni lipi ukiachilia mbali kuajiriwa kwenye hiyo kampuni?  Uhakika wa kupata kazi  baada ya internship upo au utaendelea kujitolea?

ALSO READ:  Jinsi ya Kupata Wateja Mtandaoni Kupitia Matangazo Mguso (PPC Advertising)

Ukiona kampuni haikuajiri ng’atuka wala usiendelee kujitolea labda kama wanakulipa pesa inayokidhi mahitaji yako kipindi unajitafuta. 

Muda uliowekwa kwa ajili ya internship

Internship ikidhidi miezi sita inaadha kupoteza ukweli wake yaani unaanza kuwa mfanya kazi wa bure au mwenye ujira mdogo. Makampuni mengine yanatumia mbinu hii kama fursa, utakuta mtu anajitolea miaka na miaka kisa zile pesa za kuitwa chimbo unapewa laki mbili maisha yanasonga. 

Ukweli kuhusu maisha haya wengi huumia ndani kwa ndani na kuona hakuna kazi zingine za kufanya, ndugu yangu kama upo kwenye hii hali chagua moja utafute maarifa mengine yatakayokuweka mjini au uendelee kung’ang’ana na internship ambazo hufurahishwi nazo.

Dhana ya Waajiri wengi nchini

Baadhi ya taasisi na makampuni mengi nchini yamegundua internship ni njia rahisi ya kupata wafanyakazi wengi hasa wahitimu vyuo “hapa tukimweka intern si itakuwa poa”.

Ni kweli kwamba wanaohitimu mavyuoni wengi wao hawana uzoefu wa kutosha kwenye hizo kazi. Inakuwaje mtu amefanya internship halafu asiajiriwe (nidhamu mbovu au)

Maofisini kuna changamoto zake, kwa unayetamani kufanya kazi kwenye makampuni ya aina hii hauna budi kuwa na nidhamu ya hali ya juu, ujitume ili uonekane la sivyo waajiri hawana msaada na wewe.

Internship ni kwa ajili ya wanafunzi

Kwa kawaida internship inabidi ziwahusu sana wanafunzi walioko elimu ya kati na juu. Na hili jukumu si la kutegemea sana serikali, Mwanafunzi mwenyewe yampasa atafute kampuni au taasisi kwa ajili ya kujitolea (internship) kadri iwezekanavyo kabla hajahitimu. Anaweza kufanya kazi either kwa kuhudhulia mguu kwa mguu kwenye hiyo taasisi au kupitia mtandao (virtual internship).

ALSO READ:  Ifahamu kazi ya Social Media Manager na majukumu yake

Hii itamsaidia kupata uzoefu wa kazi ili kipindi atakapomaliza masomo asianze kuhangaika kutafuta nafasi za kujitolea bali kutafuta kazi. 

Sanjali na hilo kuna kujiajiri, hapa nazungumzia uwezo wa kufanya kazi zako binafsi kwa kutumia uzoefu ulioupata mfano kuanzisha internet cafe, kufungua biashara, kusimamia mitandao ya kijamii ya kampuni husika au kutengeneza mifumo kwa watu wa coding(programming).

Je Unatakiwa kufanya nini?

Kuna njia mbili za kufanya kwa kijana unayetazamia kuiona kesho yako yenye mafanikio.

  1. Fanya internship ambayo utakuwa unalipwa angalau kiasi fulani cha pesa huku ukiweka malengo yako sawa, usiwe mtu wa internship kila siku na ikitokea,kupata kazi kwenye makampuni imekuwa ni changamoto fikiri point ya pili.
  1. Mjenzi wa maisha yako ni wewe mwenyewe, umetafuta kazi kwenye makampuni, taasisi na umekosa. Ni muda sasa wa kukaa na kutafakari kazi binafsi zitakazokuingizia kipato, unaweza kujaribu mtandaoni  kazi za freelancing.

Hayo ndiyo mambo muhimu ya kuzingatia katika safari yako ya kuitengeneza kesho.

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.

You May Also Like

Products From Tanzlite