Digital Marketing ni nini? Haya hapa mambo muhimu ya kufahamu

Teknolojia imeleta mambo mengi. Mojawapo ni kuibuka kwa kazi ambazo hazikuwepo kabla. Vilevile imeweza kubadili namna ya utendaji kazi wa kazi nyingi tulizozizoea na kuzifanya ziwe tofauti kabisa. Teknolojia imeathiri kila kitu. 

Moja kati ya taaluma mpya zilizoweza kuibuka kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia ni taaluma ya kutafuta masoko na kuuza bidhaa au huduma kwa njia ya kidigitali (Digital Marketing). Taaluma hii kwa hapa nchini Tanzania bado ni ngeni na wengi hawaifahamu. Hata vyuo vyetu bado havijaanza kufundisha somo hili ipasavyo. Lakini sio jambo la kushangaa kwani ni jambo la kawaida kwa vyuo vyetu kuachwa nyuma na kasi ya mabadiliko ya teknolojia.

Digital Marketing ni nini? 

Mara nyingi ninapojitambulisha kwamba ninafanya digital marketing, wengi huniuliza maana ya digital marketing. 

Katika makala hii utaweza kufahamu maana ya Digital Marketing pamoja na kufahamu sehemu unayoweza kujifunza elimu hii bure kabisa na kupatiwa cheti kinachotambulika duniani. Kama wewe ni mfanyabiashara unayetamani kuingia kwenye ulimwengu wa kutafuta masoko kidigitali au unataka kujifunza Digital Marketing kama taaluma basi makala hii inakuhusu. Twende sambamba. 

Kwa tafsiri ya kawaida, Digital Marketing inaweza kutafsiriwa kama;

Utafutaji masoko, kuuza pamoja na kutangaza bidhaa au huduma kwa kutumia majukwaa ya kidigitali (online platforms) kama vile mitandao ya kijamii na tovuti. 

– Tanzlite

Angalia maana kutoka kwenye mtandao hapa chini;

The use of numerous digital tactics and channels to connect with customers where they spend much of their time online

– HubSpot

The marketing of products or services using digital technologies, mainly on the internet, but also including mobile phones, display advertising, and any other digital medium

Wikipedia

Digita Marketing kwa majina mengine huitwa Internet Marketing, e-commerce au Online Marketing.

Kwanini digital marketing ni muhimu? 

Sababu zinaeleweka. Siku hizi kila mtu yuko online. Kila mtu yuko kwenye mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter, Instagram na mingineyo. Mitandao imejaa watu. Wakiwemo wateja wa bidhaa yako. 

Hii ina maana gani kwa wafanyabiashara? 

Wafanyabiashara na wajasiriamali wanatakiwa kujiongeza. Siku hizi mambo ni digitali, hivyo biashara nazo hazina budi kuendeshwa kidigitali. Hauwezi ukaweka mabango barabarani au kubandika kwenye magari wakati watu wanatumia muda mwingi kutazama kwenye simu janja zao. 

Hata redio na televisheni zimekuwa hazitumiwi sana na watu. Siku hizi ni mwendo wa YouTube na muziki wa kudownload. Kila kitu kiganjani. 

Kama mfanyabiashara unaekwenda na wakati, ni lazima kuingia kwenye ulimwengu wa uuzaji na utafutaji masoko kidigitali. Wateja wako wapo Instagram na Facebook kwanini wewe usiwepo? 

Vipengele vinavyo husisha Digital Marketing

Ukisikia digital marketing, mara nyingi Inahusisha vipengele vifuatavyo;

Kutafuta masoko kupitia mitandao ya kijamii (Social Media Marketing) 

Hili ndio swala ambalo watu wengi humaanisha wakiongelea Digital Marketing. Makampuni mengi yamefungua akaunti za mitandao ya kijamii kwa lengo la kujiweka karibu na wateja wao pamoja na kupata wateja wapya, kujenga mahusiano mazuri na wateja wao pamoja na kuzungumza nao wanapokuwa na maswali. 

Kupitia mitandao ya kijamii, kampuni hutengeneza maudhui kwa mfumo wa picha, video au maandishi ili kuwafahamisha wateja kuhusu huduma za kampuni, kutoa ofa na promosheni mbalimbali kwa wafuatiliaji wake (followers) Fahamu zaidi kuhusu kazi ya social media na majukumu yake hapa. 

Uuzaji kupitia barua pepe (Email marketing) 

Umeshawahi kuambiwa Subscribe to our newsletter? Basi hicho ndio kitu tunaongelea hapa kwa haraka haraka. Barua pepe ni mtandao mkongwe ambao umekuwepo kwa miaka mingi sasa. Wafanyabishara huomba kukusanya barua pepe za watembeleaji wa tovuti zao ili baadaye waweze kuwashirikisha juu ya fursa na ofa mbalimbali za kampuni husika. 

Kwa kuwa watu wengi wanatumia simu za mkononi, barua pepe hazina budi kuandaliwa katika muonekano unaofaa kwenye simu (mobile friendly). Bila kufanya hivyo ni bora usitumie njiaa hii kwani email zako hazitasomwa na utawafanya wateja kujiondoa (unsubscribe) kwenye orodha ya mawasiliano yako. 

Kujitangaza kupitia Tovuti (Website) 

Tovuti ndio njia kuu ya kupeleka biashara yako online. Kama ulivyofungua duka la nguo pale Kariakoo, basi unaweza ukalihamisha duka hilo hilo ukalipeleka mtandaoni na wateja wanaweza kukutembelea, kuchagua nguo na kufanya manunuzi bila kufika dukani kwako Kariakoo. Maajabu sio? Fikiria tovuti kubwa kama vile alibaba au eBay. Au hata tovuti za ahapa nyumbani kama vile Kupatana. Jaribu kuwa na tovuti yako ujionee faida zake. Hakikisha website yako ni nyepesi kufunguka, na inapendeza kwenye simu za mkononi. 

Matokeo ya haraka (Search Engine Optimization) 

Kuweka biashara yako mtandaoni si swala la kufungua tovuti tu. Bali tovuti yenye ubora unaotambuliwa na injini za utafutaji (Search Engines). Hii inajumuisha mambo kama maudhui (content) unayoweka kwenye tovuti na ubora uliotumika kujenga tovuti yako (programming). Tovuti iliyojengwa vibaya haiwezi kuoneshwa kwenye matokeo ya utafutaji (Search Results) hivyo kukufanya usiweze kujulikana na kupelekea kukosa wateja.

Fanya utafiti mdogo kuangalia kama tovuti yako inatambuliwa (indexed) na injini ya utafutaji ya Google kwa kuingiza maneno yafuatayo kwenye sanduku la kutafutia (Search bar)  site:yourdomain

Mfano; site:tanzlite.com

Hakikisha matokeo yatakapoletwa na Google yanaonyesha kurasa (pages) zote zilizopo kwenye tovuti yako. Usipoona kitu ujue una kazi ya kufanya. 

Matangazo ya Kulipia (Sponsored Ads)


Kama umeshawahi kukutana na post ya page ambayo huja-follow imeandikwa “Sponsored”, basi hayo ndiyo matangazo ya kulipia. Ni aina ya digital marketing ambapo unatumia pesa kufikisha tangazo lako kwa watu wengi zaidi. Hii ni inasadia kwa mwenye biashara ambaye ndiyo anaanza kuweza kufikia wateja kwa muda mfupi sana.

Unaweza kutumia matangazo ya Facebook, matangazo ya Instagram, Google n.k. Habari njema ni kwamba matangazo haya hayana gharama sana; mfano Facebook na Instagram watakudai dola moja tu kwa siku kama kiwango cha chini cha matumizi.

Matangazo mguso (Paid Per Click Ads) 

Yanaitwa matangazo mguso kwa sababu malipo hufanyika mara tu mtu anapo bofya tangazo lako. Hii ni aina ya kutangaza bidhaa au huduma kwa kununua maneno maalum (keywords) yanayohusu bidhaa yako ambapo mtu akitafuta kwa kutumia maneno hayo, biashara yako inaweza kuoneka juu kwenye matokeo ya utafutaji (search results) 

Graphic design

Ukiingia WhatsApp au kwenye mitandao mingine ya kijamii, utakutana na picha zilizonakshiwa kwa maneno na rangi nzuri. Hii kitaalamu Graphic design (sijui kwa Kiswahili tunaitaje). Basi kila mwenye brand au mwenye event yake anataka kuporomote kwa nakshi zenye kuvutia macho ya watu na kuwashawishi kuisambaza (share) kwa wenzao. 

Kutangaza biashara kwa njia ya video (video marketing) 

Ukiondoa Google, ni search engine gani nyingine ya pili kwa ukubwa? Je ni Bing? Au Yahoo? Jibu ni YouTube. Watu wanaangalia video kwa wingi sana siku hizi . Kwa mfanyabiashara mjanja hii ni fursa kubwa. Unaweza kutumia video kuonyesha ujuzi wako katika huduma unayofanya au kuwaonyesha watu kuhusu mambo yanayojiri ofisini kwako. Pia kutangaza biashara yako YouTube si lazima uwe na video clip, —nitalifafanua hili kwa undani zaidi katika makala zijazo. 

Kutangaza biashara kupitia watu wenye ushawishi mtandaoni (Influencers) 

Watu maarufu mtandaoni wana nguvu ya kushawishi na kuweza kubadili mtazamo wa watu juu ya jambo fulani. Hivyo makampuni na brand mbalimbali zinatumia watu kama hawa kutangaza biashara zao na kufikia watu wengi. Hapa Tanzania kuna watu kama Idris Sultani ambaye ni balozi wa kampuni ya Uber. 

Kukua kwa influencer marketing kumekuja kwa sababu kuu moja; mitandao ya kijamii ni watu, na watu wanapenda kushiriki (interact) na watu wenzao kuliko kampuni. Hivyo makampuni yanajitahidi kuwa karibu na watu kwa kuwatumia watu maarufu kukuza biashara zao. 

Wapi unaweza kujifunza elimu ya Digital Marketing 

Elimu ya Digital Marketing ni moja kati ya elimu ambayo mtu hauhitaji kuwa na degree ya miaka mitatu chuoni. Lakini faida zake ni kubwa hasa katika kipindi hiki ambacho wahitimu wanatoka vyuo wasijue nini cha kufanya mtaani. Nikushauri leo, anza kujifunza Digital Marketing. Hapa chini nimeorodheasha sehemu tatu ambazo unaweza kusoma online course za digital marketing na mambo mengine mengi.

  1. LinkedIn Learning 
  2. Google Digital Skills for Africa 
  3. HubSpot Academy 
  4. The Future Learning

Ingia mtandaoni leo, chagua kozi na uanze kusoma. Ukikwama mahali au ukihitaji ufafanuzi zaidi, usisite kuwasiliana nasi. Namba zetu zipo kwenye tovuti hii ukurasa wa mawasiliano. Pia tutaendelea kutoa mafunzo kuhusu Digital Marketing kupitia mfululizo wa makala zetu za Kiswahili na Kiingereza. 

Hitimisho

Digital Marketing ni habari njema kwa biashara za karne ya 21. Ni njia rahisi ya kujitangaza, kuuza na kujipatia wateja kwa urahisi. Mara nyingi unaweza kufanya bila hata gharama yoyote. Kwa wewe unayehitaji maarifa mapya yasiyo na ushindani mkubwa kwa sasa, jaribu hii fursa. Makala zinazofuata tutaelezea kiundani kuhusu mambo haya ambayo tumeyagusia kwa muhtasari.

Bofya HAPA kutazama huduma zetu au HAPA kuwasiliana nasi kama unataka kufahamu zaidi. Pia unaweza ku-share makala hii kwa mwingine.

Je mtandao wa kijamii wa TikTok waweza kuwa fursa kwa biashara?

Je mtandao wa kijamii wa TikTok waweza kuwa fursa kwa biashara?

Maisha yanakimbia kwa kasi sana. Miji inazidi kuwa ya kisasa na yenye kupendeza. Umri nao unatutupa mkono vilevile. 

Siku hizi ukilala, ukiamka kuna jambo jipya limeibuka. Mitindo tofauti tofauti ya mavazi, muziki na mengine inakuja na kuondoka kama maji yatiririkayo chini ya daraja la mto uendao kasi. 

Ukija upande wa teknolojia ndio usiseme kabisa. Leo iPhone imetoka mpya kesho Samsung katoa kitu kikali zaidi. Hujakaa sawa Huawei anamtikisa Mmarekani kwa teknolojia ya 5G. Hapa tunaoteseka ni sisi. Hela zenyewe ziko wapi za kuweza kuwa na kila toleo jipya? Wacha tubaki na tecno zetu bwana! 

Turudi kwenye mada yetu;

Tunapozungumzia biashara za karne ya 21, tunagusa moja kwa moja maswala ya digitali, likiwemo suala la mitandao ya kijamii. Mitandao hii imekuwa nguzo muhimu kwa wafanyabiashara kuweza kutangaza bidhaa na huduma zao pamoja na kujenga mahusiano mazuri na wateja wao. 

Ninafahamu unatumia mitandao ya kijamii hasa ile maarufu kama Instagram, Facebook na Twitter. Huenda ukawa umekutana na makala hii kwenye moja ya mitandao hiyo. 

Lakini kuna mtandao mmoja unakuja kwa kasi sana kwa sasa. Unaitwa TikTok. Endelea kusoma kuona ni nini kipya juu ya mtandao huu. 

Takwimu zinasemaje kuhusu mtandao wa TikTok?

Kwa kipindi cha miaka minne tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, TikTok imeweza kuwa na watumiaji zaidi ya milioni 500 duniani kote. Wengi wa watumiaji hawa wakiwa ni vijana. 

Ripoti ya Globalwebindex ya mwaka 2019, inaonyesha asilimia 41 ya watumiaji wa TikTok wana umri kati ya miaka 16 na 24 (Globalwebindex, 2019). Kati ya watumiaji hao, watu zaidi ya milioni 150 hutumia application hiyo kwa siku. 

Aidha, imeripotiwa kuwa application ya TikTok imeongoza kwa kupakuliwa (downloaded) kwenye App Store ya Apple mwaka huu wa 2019. Kuhusu takwimu zaidi, tembelea chapisho la Kiingereza kupitia kiungo hiki

TikTok ina kipi cha tofauti?

TikTok inawapa watumiaji uhuru wa kutengeneza vipande vifupi vya video (visivyozidi sekunde 15) vikinakshiwa na nyimbo na urembo mwingine (filters) wa kuvutia kwa kutumia simu zao za mkononi. Video hizi zimejaa furaha na ucheshi (funny). 

Ukitofautisha na mitandao mingine kama Twitter na Instagram, mitambo (algorithm) ya TikTok inakuonesha vitu unavyovitaka tu. Sio mara unakutana na post ambayo hata hujui imetoka wapi kama inavyotokea huko Twitter na Insta. Pia matumizi ya hashtag yanatamba sana kwenye mitandao huu. 

Wanasema utamu wa ngoma ingia mwenyewe ucheze. Pakua application ya TikTok uonje utamu wake.

Ukiitizama vizuri application ya TikTok utaona ina muonekano sawasawa na application inayoitwa Musical.ly. Hii ni kwa sababu TikTok ambayo ni kampuni ya Kichina, iliinunua application ya Musical.ly ili kuweza kuwafikia watu wengi hasa vijana wa kimarekani. 

Swali; Je TikTok inaweza kuwa fursa mpya kwa wafanyabiashara? 

Kwasasa TikTok haina mfumo wowote unaowezesha kuweka matangazo ya kulipia (sponsored ads) kama tunayoyaona huko kwenye mitandao mingine. 

Lakini kama tunavyofahamu, hakuna kitu cha bure. Nionavyo mimi, jukwaa hili halitakuwa la bure kwa mda mrefu.

Kwa kuwa mtandao huu unapendwa na vijana wengi ambao ndio wenye nguvu ya ushawishi katika masoko, ninaona kuna kila dalili ya makampuni makubwa (brands) kuishawishi ikubali TikTok ikubali matangazo. 

Baadhi ya takwimu zinatabiri mtandao wa TikTok utakuja kuteka na kuizidi mitandao kama vile Instagram na Snapchat.

Changamoto kubwa ya mitandao ya kijamii ni tabia yake ya kubadilika kila mara, kwa kuja na mifumo mipya au kupotea kabisa kama mtandao uliokuwa ukimilikiwa na kampuni ya Google, uliofahamika kwa jina la Google+

Lakini pia ni lazima tukubaliane na ukweli kwamba hatuwezi kukwepa social media. Mitandao hii imewapa nguvu watumiaji kuwa na uhuru wa kuchagua ni namna gani wanataka kupokea taarifa. Hivyo kama mfanyabiashara unaetafuta kukuza jina la biashara yako na kufikia wateja wengi zaidi, huna budi kuwekeza kwenye moja ya mitandao hii. 

Palipo na wengi pana fursa nyingi. Wewe kama mfanyabiashara, unajiona uko tayari kuwafata wateja wako walioko TikTok? Au utawasubiri wakirudi Insta na Fb? 

The Ultimate Guide to Social Media Marketing for Your Business [15 Tips]

The Ultimate Guide to Social Media Marketing for Your Business [15 Tips]

As a company owner, you can’t avoid social media. Social media is a business goldmine.  You only need to learn how to dig it properly. This article will tell you how.

Your customers spend most of their time on social media and as a serious business, you need to spend as much time with them as you can on the channels they like. 

Social media is where people talk about their favorite brands and products. It is also where people go to complain about a certain service or company. You need to be there to listen to all these conversations and learn the sentimental language people use to talk about you. 

Many companies find it difficult to have a successful social media presence. Without knowing what you’re doing online, it is easy to ruin your business reputation just in minutes. Here are the best tips to stay on top of the social media game. Without further ado, let’s dive in;

Be familiar with social media platforms and their users 

Social media networks are not interchangeable. They’re different platforms with different content types and different types of people. 

For example;

  • Instagram and Pinterest are highly visual mostly used by young people. So you need to be visually creative. 
  • LinkedIn is a career based platform joining professionals
  • Twitter is a microblogging platform which is perfect for texts than images 

Knowing the differences among these channels will help you to better navigate and engage people within each channel. 

Be human, not a company 

Many companies have no idea what they are doing on social media. They usually make a terrible mistake of making these social platforms all about themselves —posting about programs launching, talking to people instead of talking with people. Or even worse, going silent for weeks and only come to post when they have something nice about themselves to say. 

Social media marketing is not about great advertising and branding, it is about building meaningful relationships with your followers. You can make your social media channels feel more human by doing the following;

  • Talk with people, don’t talk to people.
  • Make your followers matter, listen to them carefully
  • Take time to interact and respond to their comments
  • Create a comment response chart for frequently asked questions

Social media is human and that’s exactly how you should approach it. Don’t be a company speaking in tones that limit your followers from interacting with you. 

Do you prefer a professional and authoritative tone? Then you might consider using it on LinkedIn. Is your tone light and friendly? Then social networks like Instagram and Facebook are perfect for you. 


Do not spam

Just because you have that great product or service you offer, it doesn’t mean you have the right to cluster your feed with the same product every post you make. That is spamming. Using too many hashtags is also spamming.

cluttered Instagram feed
Do not clutter you feed with the same images

Let’s say you run a smartphone shop at Kariakoo and you have decided to open an Instagram account to find more customers online. You really don’t have to post smartphones every time you make a post. You won’t last long. 

You can be creative with your feed by making it more interesting. On certain days you can post customer testimonial videos, how-to tips, offers, quotes, tips, facts, funny memes and many more. Be creative. 


Don’t be too selly 

No one goes on social media to buy. People go on social media to socialize. There’s a reason it was called social media in the first place. While you are there, don’t be overly promotional or too selly. Be strategic. Hang out with people while you are pushing your agenda. There is no need to be aggressively promoting your business because people who follow you, are already interested in your product or service


Do not lie!

It takes years to build a company’s reputation. However, with the rise of online conversations, it only takes minutes for a company to suffer. Always be authentic. People can smell it when it’s fake. 

Have a plan

Make things easier for you by having a plan to act on. Without a clear thought out plan, social media is going to be tough for you. Try to use a content calendar that will guide you. With a calendar, you will know when and what to post.

A good content calendar should answer the following questions;

  • What type of content are you going to share? 
  • At what time you’re going to share the content and how much time you will spend on social networks? 
  • How often are you going to post on a specific channel? 

Stay updated and motivated

Social media isn’t something you learned three years ago and keep believing you know it. Being a social media enthusiast means being a lifelong learner. These platforms are constantly evolving —adding in new hashtags, new tools, and features. You need to be alert when these new features arrive and use them to your advantage.


Content is king

Without great content, the window to succeeding on social media is very narrow. Connect with your audience with great content such as video clips, infographics, images, and eBooks. Create content that will build trust, help people answer their questions and establish yourself as an authority in your field. 

Use videos often 

If a picture says a thousand words, a video says a million. Video has become the most important part of the online experience. Internet speed is getting faster and our devices are getting smarter. All these factors contribute to the booming of video marketing. Use video to tell a story, to showcase your store or sharing helpful tips —or anything. With the help of video editing apps, you can create great videos at any budget. 

Tell moving stories

This should be on number one. Storytelling, the oldest form of art has proven to be at the core of every successful marketing strategy. This is because there is nothing more powerful that can unite people than a good story. Remember the ‘Dream Crazier’ advertisement by Nike? or the ‘No Human Is Limited’ story? That’s what we are talking about.

Use employees advocacy

The easiest way to grow your visibility on social media is by using your employees as brand champions. Make sure you empower your team so that they understand and live the brand in online and offline life. If your employees love their job, they will surely become brand protectors and promoters online.


Try influencer marketing

We live in a world where people are becoming brands while brands are trying to be people. You can use influencers to skyrocket your brand’s awareness or grow your sales. Influencers are affordable and provide social proof because they have the capacity to affect people’s opinions about a certain topic, service or product. 

Pay attention to metrics and KPIs

There is no planning without measuring. The good thing about digital marketing is that we can’t wait for people to inform us about our mistakes. We can use data to make educated decisions about our online strategy. Social networks know a lot about their users and you can use the analytics they provide to gain insights about your followers. 

To measure your KPIs (Key Performance Indicators), you need to set clear and attainable goals. Start with the question; what do you want to accomplish in social media. See the metrics chart obtained from HubSpot below;

Social media table
Image by HubSpot

Find inspiration from other brands 

Here are my favorite brands on Instagram. Check them out and learn how they are engaging their audience by creating content that is more than just their products. 

Keep your eye on your competitors 

When you look at your competitors’ social media channels, do you feel proud? Or you feel jealous? If you feel jealous, then there are things you really need to improve on your strategy. 

It is no doubt that social media is among the new ways of serving the 21st-century business. The internet has given customers the power to choose the way they want to receive information. Business owners no longer have the luxury to choose advertising methods as they used to with traditional marketing.

Whether you choose to be on social media or not, people are already talking about you there. It is up to you to join these conversations or start your own conversation and empower your followers to do the marketing for you.

Jinsi ya kukuza biashara yako kupitia mtandao (Digital Marketing)

Jinsi ya kukuza biashara yako kupitia mtandao (Digital Marketing)

Biashara na matangazo ya karne ya 21 yanategemea sana teknolojia. Tunaishi ulimwengu wa dijitiali hivyo kila kitu hakina budi kufanywa kidijitali.

Unaweza kuwa na biashara yako au kampuni yako inayotoa huduma ama bidhaa imara na uhakika kabisa lakini usipotumia bidii kujitangaza ama kujiweka online, unaweza kuzidiwa na watu ambao huduma zao hazina ubora zaidi yako.

Kujitangaza (au kutafuta masoko) kimtandao ni njia rahisi na isiyo gharama kuwafikia watu wengi zaidi. Ukweli ni kwamba usipofanya matangazo ya biashara yako, yote uyafanyao yataishia kwa watu wachache tu wanaokuzunguka.

Nenda na wakati

Siku hizi mtu akitaka msaada wa jambo fulani wazo la kwanza kumjia ni kushika simu yake na kuperuzi kuhusu akitakacho. Hapo ndipo huweza kukutana na majibu ya swala alitakalo mtandaoni.

Fikiria wewe ndiyo hauko mtandaoni, mtumiaji huyu wa internet atakufahamu vipi? Atafahamu vipi una duka la nguo Kariakoo? Badilika. Nenda na wakati, hamia ulimwengu wa digitali. Wazungu wanaita ‘Digital Marketing’ mbinu ya kutafuta masoko na kujitangaza kupitia majukwaa ya kimtandao kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, email, whatsapp na kadhalika.

Unaanzia wapi?

Ni rahisi. Ingawa  waweza kutumia pesa panapohitajika, kujitangaza mitandaoni ni bure kabisa. Ni kama vile ulivyo na akaunti facebook bila malipo yoyote. Cha msingi ni wewe kujifunza mbinu za uendeshaji na kuchagua njia ipi inakufaa zaidi

Miliki tovuti/website yako

Tovuti hasa kwa mashirika, makampuni na biashara kubwa ni kitu cha lazima. Hii huongeza hadhi ya kampuni kwa ujumla. Tofauti kubwa kati ya tovuti ama website na mitandao mingine ya kijamii ni namna ya kuweka maudhui.

Kupitia tovuti, mtu anaweza kupata taarifa kwa kina kuhusu kampuni au bidhaa. Pia kwenye tovuti kunaweza kufanyika shughuli kama manunuzi ya mtandaoni, kuandikisha watu kwa ajili ya program, newsletter na kadhalika.

Unatengenezaje tovuti? Ni rahisi. Kuna watu na makampuni mengi yapo kukusaidia kufungua tovuti yako. Sisi Kampuni ya Tanzlite Digital tunatengeneza website za kisasa kwa bei nafuu ili kukusaidie wewe na biashara yako katika ulimwengu wa digitali.

Mitandao ya kijamii

Karibia kila mtu yuko Facebook au Instagram. Maana yake ni kwamba soko liko huko kwa sababu ndiko watu waliko. Cha kufanya ni kupeleka biashara yako huko. Fungua akaunti kwa jina la biashara au kampuni yako na uanze kujitangaza.

Nini cha kupost ukiwa huko? Hapa ndipo wengi hukosea. Makampuni mengi hapa nchini hayafahamu namna ya kutumia mitandao ya kijamii.

Mitandao ya kijamii ni watu, hivyo wewe kama kampuni unatakiwa ufahamu namna ya kuishi na watu. Fahamu namna ya kushirikiana na watu. Isiwe kila siku unapost kuhusu wewe na bidhaa zako tu. Utawachosha watu. Kuwa mbunifu.

Unaweza ukawa unapost picha za bidhaa zako, picha za wateja wenye nyuso za kuridhika na huduma yako. Kama utakuwa mtundu zaidi waweza tengeneza vipande vifupi vya video. Kumbuka pia hautakiwi kupost mara kwa mara ikawa too much.

Jambo la msingi kuzingatia ni kwamba mitandao ya kijamii ni majukwaa tofauti tofauti yenye maudhui na makundi ya watu tofauti. Ni muhimu kulifahamu hili ili aweze kutambua kipi cha kufanya ukiwa kwenye haya majukwaa.

Boosti tangazo lako kupitia Sponsored Ads

Kama ndiyo kwanza unaanza na wateja hawakuji na huna followers wengi, njia rahisi ya kufikia watu ili waone unachouza ni kulipia tangazo. Kama huwa unaona post ya page ambayo huja-follow imeandikwa “Sponsored”, basi hayo ndiyo matangazo ya kulipia. Bei ya kutangaza ni rahisi tu; kwa upande wa Facebook na Instagram kiwango cha chini ni dola moja tu (Tsh 2400*)

WhatsApp pia ni fursa kubwa

Kwa kaiwaida WhatsApp hujumuishwa kwenye kundi la mitandao ya kijamii. Lakini kiuchambuzi zaidi, WhatsApp pamoja na majukwaa mengine kama Telegram na Messenger yanaitwa private messaging platforms. WhatsApp imekuwa kimbilio la wajasiriamali wengi wa kitanzania. Kupitia magrupu na status whatsapp, watu wanatangaza bidhaa zao na kupata wanunuzi. Soma zaidi jinsi ya kutumia WhatsApp Business hapa

Weka biashara yako kwenye Google My Business

Kampuni ya Google wana mfumo wa kukuwezesha kuweka biashara yako kwenye ramani ya Google ili watu wa karibu na eneo lako waweze kukuona wakitafuta huduma au bidhaa inayoendana na yako. Pia wanaweza kuacha maoni kama vile kukupa five star rate ili kuongeza visibility yako mtandaoni.

Pia zipo tovuti zingine zinazokuwezesha kuorodhozesha biashara au bidhaa yako kama vile Kupatana, na Zoom Tanzania.

Kuwa mbunifu katika maudhui (Content Marketing)

Karibia kila mtu anaandika maudhui mtandaoni. Iwe ni mstari mmoja kama status za facebook na whatsapp laikini yote ni maudhui. Kinachokuja kutofautisha kati ya maudhui mengi yanayoandikwa kila siku mtandaoni ni aina na stadi za uandaaji maudhui hayo.

Nichukulie mfano wa mchekeshaji maarufu nchini, Idris Sultani, kuna wakati huandika posts kwenye ukurasa wake wa instagram akitangaza makampuni kama Uber. Uandishi wake ni mwepesi na wenye ucheshi, lakini hapo ameweza kutangaza biashara.

Kwa makampuni na taasisi mbalimbali unaweza kuajiri muandaa maudhui na mwongozaji wa akaunti za kijamii za kampuni. Hili ni jambo muhimu sana katika ulimwengu wa mawasiliano ya kidigitali.

Kampuni yetu ina wataalamu wa masuala ya Digital Marketing ambao wanaweza kukurahishia kazi kuandaa yote haya. Kazi yako ni kufanya biashara, sisi tunaimarisha uwepo wako mtandaoni (online visibility)

Amua sasa!

Siku hizi mambo yanaenda kidigitali, hivyo hata biashara yako haina budi kuenda na wakati.

Kama uliwahi kujaribu tovuti au mitandao ya kijamii na haukupata matokeo mazuri basi kuna mahali haukufanya kwa usahihi. Tafuta wataalamu wakusaidie. Unapitwa wateja kwa kushindwa kuwa online. Amua sasa!

TANGAZO: Tumeanzisha group la WhatsApp kuwapa USHAURI Wajasiariamali wanaouza bidhaa mtandaoni kama vile Instagram, Facebook na WhatsApp. Bofya picha hapo chini.